KAMBI YA WIKI 3 JUU YA UCHUNGUZI WA SARATANI YA SHINGO YA MLANGO WA KIZAZI KWA KINA MAMA KISIWANI PEMBA YAZINDULIWA RASMI LEO AKINA MAMA WAASWA KUJITOKEZA .
AMINA AHMED MOH'D
WANANCHI kisiwani Pemba wametakiwa kujitokeza kwa wingi katika kambi za uchunguzi wa saratani ya shingo ya mlango wa kizazi zilizofunguliwa tena leo kisiwani humo ili kuweza kuchunguzwa afya zao na watakaobainika kuweza kupatiwa matibabu dhidi ya ugonjwa huo kwa kufuata utaratibu maalum wa utolewaji wa huduma hizo uliowekwa na madaktari katika wilaya zote nne .
Kambi hiyo ya madaktari 36 kutoka Jasmin Clove nchini China kwa kushirikiana na serikali ya mapinduzi ya Zanzibar ambayo imedhamiria kutoa huduma hizo kwa makundi maalum ya wanawake ambao ni wenye umri kati ya miaka 19 hadi 69 kutoka maeneo mbali mbali ya kisiwa cha Pemba lengo ikiwa ni kusaidia jamii ya wanawake na wasichana kisiwani humo kuwa na afya bora.
Kauli hiyo imetolewa na Afisa mdhamini wizara ya nchi ofisi ya rais kazi uchumi na uwekezaji Pemba Fadhila Hassan Abdalla alipokuwa akizungumza na akina mama kutoka maeneo mbali mbali waliofika katika hospitali ya Chake chake katika ufunguzi wa kambi hiyo ya uchunguzi ambayo inatarajiwa kutoa huduma hizo kwa muda wa wiki 3 katikamaeneo mbali mbali ya hosptali ikiwemo Abdalla Mzee Wete, Micheweni pamoja na chake chake.
Akizungumza kwa niaba ya madaktari hao mkuu wa kambi hiyo Xiaomin Qi kutoka kampuni ya Jasmine clove amesema kuwa lengo la kuweka kambi hiyo kisiwani Pemba ni kusaidia kutoa huduma ya matibbu kwa akina mama kutokana na kuwepo kwa uhitaji mkubwa katika suala hilo .
Kwa upande wake afisa mdhamini wizara ya afya Pemba ameishukuru serikali ya china kwa kuendelea kutoa mashirikiano na wizara ya afya katika kusaidia kuimarisha huduma za matibabu mbali mbali kisiwani pemba ikiwemo suala hilo la uchunguzi wa magonjwa dhidi ya saratani ya shingo ya mlango wa kizazi.
Kambi hiyo ya wiki 3 kisiwani humo inatarajiwa kutoa huduma hizo za uchunguzi kwa wanawake Zaidi ya wagonjwa elfu 34 miatano ambapo hadi kufikia awamu hii ya 6 ya utekelezaji wa mradi huo wagonjwa 2 elfu 20 tayari wameshafanyiwa uchunguzi huku wagonjwa elfu 3000 wakionekana kuwa na magonjwa mbali mbali huku 561 wakigundulika kuwa na saratani ya shingo ya mlango wa kizazi kwa hatua za awali na wagonjwa 72 wakigundulika kuwa na ugonjwa huo katioka hatua ya 3.
MWISHO.
Comments
Post a Comment