WANAWAKE KISIWANI PEMBA WALILIA MILA ,DESTURI,MAVAZI YASIO RAFIKI KUENDELEA KUWA KIZINGITI USHIRIKI WA MICHEZO MBALI MBALI








Na,AMINA AHMED PEMBA .
BAADHI ya wanawake kisiwani Pemba Akiwemo Halima Juma Shehani,Pamoja na Zulfa Shaame Ali wote wakaazi wa Madungu  wameeleza mitazamo yao juu ya kutokushiriki  michezo mbali mbali ikiwemo mpira wa miguu  , pamoja na mazoezi ya viungo katika viwanja mbali mbali vya michezo  ambapo wamesema kuwa  mila na desturi zao zinawawia ugumu kushiriki  katika harakati hizo.

 Wamesema mavazi  yasio  rafiki  endapo yatavaliwa na wanawake   ikiwemo suruali  ni kuenda  kinyume na mila silka pamoja na  utamaduni wa jamii kisiwani humo .
Aidha wameeleza kuwa maadili ya jamii nyingi kisiwani Pemba yanakwenda sambamba na mfumo wa miongozo yq  maisha  dini waliyokulia hivyo suala hilo  ni changamoto kwa upande wao.
Wamesema iwapo kutawekwa mavazi maalum  ya kuvaliwa na wanawake  watakaoamua  kushiriki michezo ambayo yatazingatia staha na heshima ya mwanamke huenda ushiriki wao utaongezeka  katika tasnia hiyo ya michezo.

Aidha wakatumia fursa hiyo kuwaomba viongozi wa dini  kutoa elimu juu ya suala hili  ili iwezo kuwasaidia kuongeza ushirimi wao bila  kuendana kinyume na mafundisho ya kidini.


 Wakizungumzia suala hili la ushiriki mdogo  wa wanwake rika mbali mbali katika michezo baadhi ya vijana wanaofanya mazoezi  katika uwanja wa Polisi  Madungu  wametoa maoni yao na kusema kuwa  kutokushiriki michezo kwa wasichana kisiwani humo ni kutokana na utamaduni  aibu ya mavazi ya suruali,pamoja na kutokuwepo kwa viwanaja vya michezo ambavyo vya wanawake. 

  Wamesema  licha ya wengi kujua umuhimu wa mazoezi kwa afya zao lakini suala hilo la mavazi ni miongoni mwa changamoto wanayohisi  ni kikwazo  inayowakosesha kushiriki fursa hiyo .

 Kwa mujibu wa  Sera ya Michezo  suala hili la  la ushiriki wa  michezo limewekwa kwa  wote wote  ambapo harakati za kuzungumza na viongozi  wa michezo juu ya masuala  haya  zinaendelea .



Comments

Popular posts from this blog

BAJAJI WAMLILIA RAIS DK MWINYI PEMBA ,WAOMBA MSAADA KWAKWE WASEMA WAMECHOSHWA NA HILI KUTOKA MAWASILIANO

Masheha wanawake wa Wilaya ya Magharib B walivyoleta mabadiliko na maendeleo kwenye shehia zao.

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.