WATU WENYE ULEMAVU WA AKILI PEMBA WAFUTARISHWA WAZIRI HARUSI ATUMA UJUMBE HUU KWA WANANCHI .
NA -AMINA AHMED MOHD ,PEMBA.
WAZIRI wa Nchi ofisi ya Makamu wa kwanza wa Rais Zanzibar Harusi Said Suleiman amewataka wazazi wakike na wakiume pamoja na wadau wa kutetea haki za watu wenye ulemavu kuongeza umakini katika kusimamia malezi ya watoto na watu wenye ulemavu wa akili zaidi katika katika kipindi kijacho cha msimu wa siku kuu ili kuwaepusha na vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia.
Kauli hiyo ameitoa leo katika ukumbi wa Tibrinzi Chake Chake mara baada ya kumaliza ghafla ya Iftari ya pamoja kati ya watu weye ulemavu wa akili,wazee walezi wasimamizi wadau na watetezi wa haki za watu hao iliyoandaliwa na Jumuia ya watu wenye Ulemavu wa Akili Zanzibar upande wa Pemba .
Amesema jukumu la kuwatunza na kuwalinda watu wenye ulemavu wa akili dhidi ya vitendo vya udhalilishaji linahitaji umakini zaidi kwa vile wao ndio waathirika zaidi katika matendo hayo.
" Tunaelekea katika siku kuu nawaomba wazazi akina baba na akina mama tuwaangalie sana watu wetu hawa tuweke jicho lenye uangalizi maalum huu sio wakati wa kuwaacha peke yao ".
" Tusije tukwaachia tu kama Mbuzi au Ngo'mbe waliokatwa kamba wakawa wanazurura tu mitaani na tuhakikishe tunatoka nao na kurudi nao mkononi ili wasije wakapatwa na majanga haya yaliotawala duniani kote ya unyanyasaji ambayo ni hatari zaidi kwa upande wao".
Waziri Harusi pia amewaasa wananchi kuendelea kuwatunza kuwajali kutetea haki zao pamoja na kuwathamini watu wenye ulemavu kwa vile suala hilo linaweza kumfika mtu yeyote .
Aidha Waziri huyo ameipongeza jumuia ya watu wenye ulemavu wa akili kwa upande wa Pemba kwa kuwakutanisha watu wenye ulemavu wa akili kutoka sehemu mbali mbali katika futari ya pamoja ambapo ameziasa jumuia nyengine kuiga suala hilo .
Hata hivyo waziri huyo amewaasa waumini wa dini ya kiislam Zanzibar kuendeleza matendo mazuri wanayoyafanya katika mwezi mtukufu wa ramadhan ikiwemo kusoma qur -an ,mashirikiano kusaidiana na pamoja na kumuamudu mwenyezimungu katika miezi mengine ili kupata ujira zaidi .
Kwa Upande wake Mkubwa Ahmed Omar ambae ni Mjumbe wa kamati tendaji wa jumuia hiyo Zanzibar amesema kuwa jumuia hiyo itaendelea kutetea haki za watu wenye ulemavu wa akili pamoja na kuzisimamia ipasavyo kwa maslahi na maendeleo ya watu hao.
Akizungumza katika ghafla ya iftari hiyo mlezi wa jumuia ya watu wenye ulemavu wa akili kwa upande wa Pemba Sheh Said Ahmad Muhamed amesema suala hilo liliofanywa na jumuia hiyo ni miongoni mwa mambo yaliyohimizwa katika Uislam ni pamoja na kuwatendea wema watu wenye mahitaji maalum ambapo amewaasa waislam wote kuendelea kuwatendea weka watu hao.
Akitoa neno la shukurani kwa wanajumuia hiyo Afisa mdhamini Wizara ya Utalii na Mambo ya kale Zuhura Mgeni Othman ameishukuru jumuia hiyo kwa kuandaa ifatari hiyo ambapo amesema kuwa wadau wa kutetea haki za watu wenye uleamavu wataendelea kushirikiana vyema na jumuia hiyo katika kuona wanshiriki ipasavyo katika fursa mbali mbali .
Jumla ya watu wenye ulemavu wa akili 90,wazazi walezi wasimamizi wa watu hao pamoja wadau kutoka maeneo mbali mbali kisiwani humo wameshiriki katika iftari hiyo maalum iliyoandaliwa na Jumuia ya watu wenye ulemavu wa akili ofisi ya Pemba kwa kushirikiana na ofisi ya Makamu wa kwanza wa rais na wadau wengine mbali mbali.
mwisho
Comments
Post a Comment