NAIBU WAZIRI AGUSWA CHANGAMOTO ZA WANANCHI
WANANCHI wenye mahitaji m, pamoja na wazee wameiomba serekali ya mapinduzi ya Zanzibar kuwaona pamoja na kuwafiriji ili kuondokana na hali duni walizonazo .NA AMINA AHMED MOH'D PEMBA.
Wameyasema hayo mara baada ya kutembelewa na naibu Waziri wizara ya maji nishati na madini Zawadi Amour Nassor ikiwa ni katika ziara yake ya kuwatembelea na kuwafiriji wananchi hao .
Wamesema kuwa viongozi hawaoneshi kuwajali mara baada ya Kufikiwa na matatizo mbali mbali hivyo kuimba serekali kuwakumbuka ili kupata faraja .
Katika hatua nyengine wameiomba serekali kulichukulia hatua suala la kesi za udhalilishaji ili kupunguza matendo hayo.
Akizungumza mara baada ya kumalizika Kwa ziara hio Zawadi Amour Nassor amesema lengo la ziara hio ni kuwatembelea wananchi wanaokabiliwa na changamoto mbali mbali pamoja na kuwafiriji ili kupata faraja katika nyoyo zao .
Mwanakombo Omar Ali kutoka konde amesema ni vyema serekali kuwaangalia watu wenye mahitaji maalum Kwa upeekee ili waweze kunufaika na serekali Yao .
Comments
Post a Comment