WANAWAKE WAASWA KUGOMBEA MAJIMBONI BILA WOGA 2025 ,NA KUACHA KUSUBIRI NAFASI ZA KUTEULIWA.
NA AMINA AHMED, PEMBA.
KUFUATIA kutokuwepo kwa Usawa wa kijinsia katika vyombo vya kutolea maamuzi Wanawake wameaswa kugombea nafasi za uongozi wa majimbo katika uchaguzi mkuu 2025 bila kuogopa vitisho vinavyotolewa na watu wachache na wasiopenda kuona wanafika mbali katika maendeleo na kuishia katika nafasi za kuteuliwa kila siku.
Kauli hiyo ya kuwahamasisha imetolewa na aliewahi kuwa Mbunge wa Chonga Chake Chake Leila Nassor Khamis alipokuwa akizungumza na Mwandishi wa habari hizi maalum za uongozi kwa wanawake aliefika nyumbani kwake Chanjaani.
Alisema iwapo watafanya maamuzi juu ya jambo hili kutasaidia kufikia usawa wa kijinsia katika vyombo vya maamuzi ambao bado haujafikiwa kutokana na waliowengi kuziogopa nafasi za majimboni ambazo zina fursa zaidi.
Aidha aliwataka wanawake kujitokeza kuwania nafasi mbali mbali zitakapotangazwa ikiwemo nafasi ya ubunge uwakilishi na udiwani katika majimbo na kuacha kuwaachia wanaume peke yao kuitumia fursa hiyo kwa kuogopa vitisho.
" Jimboni hakuna kikubwa kinachitufanya wanawake tushindwe kuongoza sheria ndio zile zile kanuni ndio zile zile siku zote, kufanya jambo kwa maslahi ya unaowaongoza bila ya upendeleo au ubaguzi wa aina yeyote tuzifuate fursa za majimboni tunaziweza, tusisubiri za kuteuliwa kila siku.
" Wanawake wenyewe ndio ambao tutaweza kuzisemea haki zetu na ni kwa kiasi gani tunaweza kuzitetea ni kugombea kwa wingi kupitia nafasi za majimboni ili tuweze kufika katika vyombo vyakutolea maamuzi.
" Changamoto ni za kawaida , tunatakiwa tujiamini na kujua tunachotakiwa kukifanya inatosha wewe kuingia jimboni tuzichangamkie fursa hususan ni wanawake vijana".
" Hakuna chochote kibaya endapo mwanamke atakuwa kiongozi kuombwa rushwa au kuwa na tabia mbaya ni mtu mwenyewe tu na endapo hautokuwa tayari kufanya hivyo wala hakuna atakaekulazimisha."Alisma bi Leila Aliwahi kushika nafasi mbali mbali za uongozi ikiwa ni pamoja na Ubunge wa jimbo Chonga Wilaya ya Chake Chake.
Hadi kumalizika uchaguzi mkuu mwaka 20220 Idadi ya wabunge wanawake
Comments
Post a Comment