MAMLAKA YA MAPATO ZANZIBAR ZRA YAFUNGUA JENGO JIPYA LA OFISI MKOA WA KASKAZINI PEMBA, IKIWA NI MUENDELEZO WA SHAMRA SHAMRA ZA MIAKA 3 YA UONGOZI WA DK MWINYI.


NA AMINA AHMED MOH’D- PEMBA.
WANANCHI Mkoa wa Kaskazini Pemba wametakiwa kuzidisha uzalendo katika ulipaji wa kodi mbali mbali ili  kuisaidia serikali kupanga mipango mbali mbali ya maendeleo ya nchi. 

Ameyasema  hayo mkuu  wa wilaya  ya Micheweni Mgeni Khatib Yahya alipokuwa akizungumza na wananchi wa Wete  kwa niaba ya  Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha na Mipango Sada Mkuya  Salum katika ghafla ya Ufunguzi wa  Jengo la   Mamlaka ya Mapato Zanzibar ZRA  Mkoa wa kikodi  Kaskazini Pemba  . 

Amesema   wapo baadhi ya wananchi  hususan ni wafanya biashara wamekuwa wakiidanganya serikali  na kufanya malipo yasiostahili wakati wa uuzaji  na utowaji wa risiti jambo huku baadhi yao wakishindwa kuzitoa kwa wateja wao  , hivyo ni vyema kuwacha tabia  hiyo na kushirikiana na serikali kupitia mamlaka hiyo katika kuongeza mapato  yatakayosaidia kutumika katika uletaji wa maendeleo. 

 Aidha Mkuu huyo amesema kuwa Serikali ya mkoa itaendelea kuinga mkono mamlaka ya mapato Zanzibar ZRA katika kuhamasisha ulipaji wa kodi   ikiwa ni pamoja na  wafanya biashara kutoa na wanunuzi kudai risiti za kielectronic   kwa wanaonunua bidhaa mbali mbali sambamba na kutowafumbia macho wale wenye dhamira ya kuihujumu serikali kwa kukwepa kodi.

Akizungumza Mwenyekiti bodi ya wakurugenzi  kutoka mamlaka hiyo Pr. Rashid Hemed  Hikman amesema mafanikio hayo ya kuongeza ofisi  katika mkoa  huo  ni katika kusaidia kufanyika kwa ufanisi kazi za ukusanyaji wa kodi mbali mbali kisiwani Pemba . 

 Akizungumza Kamishna mkuu wa Mamlaka ya Mapato Zanzibar ZRA Yussuf Juma Mwenda  Amesema ufunguzi wa ofisi hiyo  ni muendelezo wa  kusherehekea  miaka mitatu ya uongozi wa Rais wa  Zanzibar Dk Hussein Ali Mwinyi  katika kujenga  mfumo wa kodi  ambao ni rahisi  kwa walipa kodi wake. 

Aidha amesema  mamlaka hiyo itaendelea  kutoa huduma bora  kwa wananchi  sambamba na kuimarisha wafanya biashara  ili ziendelee  kukua  na kuongeza mapato yatakayosaidia kufikia malengo ya serikali kuimarisha maendeleo ya nchi. 

kwa Upande wake Mkurugenzi wa ZRA Pemba Jamal Hassan Jamal amesema kufunguliwa kwa jengo  kutasaidia kuwaondoshea usumbufu  waliokuwa wanaupata walipa kodi mkoa wa kikodi kaskazini kwa muda mrefu kutokana na kukosekana  kwa ofisi hiyo ambapo  amewataka wananchi wa mkoa huo   kuitumia ofisi hiyo  ili kujipatia huduma  zote za kikodi . 

Uzinduzi wa ofisi hiyo   umeambatana na shamra shamra mbali mbali ikiwemo ukatajai keki, ngoma, utenzi  maigizo ambapo inatarajiwa kuanza rasmi kazi zake kuanzia leo hii kwa kutoa huduma mbali mbali ikiwemo huduma za ulipaji wa ushuru wa stamp, mashine za kielectronic, Ulipaji wa kodi za majengo, Leseni, pamoja na kodi nyengine mbali mbali. 
Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

BAJAJI WAMLILIA RAIS DK MWINYI PEMBA ,WAOMBA MSAADA KWAKWE WASEMA WAMECHOSHWA NA HILI KUTOKA MAWASILIANO

Masheha wanawake wa Wilaya ya Magharib B walivyoleta mabadiliko na maendeleo kwenye shehia zao.

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.