MAFUNZO MAALUMU JUU YA MATAYARISHO YA KUSTAAFU KWA WATUMISHI WA UMMA YATOLEWA NA ZSSF KWA KUSHIRIKINA NA TCB BANK.
NA AMINA AHMED MOH’D, PEMBA.
WATUMISHI wa umma wanaotarajiwa kustaafu kisiwani Pemba wameaswa kujiwekea malengo ambayo yatawasaidia kuendeleza vyema maisha yao na kuwaondoshea usumbufu unaowapata wastaafu wengi mara baada ya kumaliza muda wa utumishi na kurudi katika jamii.
Ushauri huo umetolewa na Afisa mdhamini Wizara ya Nchi ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, utumishi na utawala bora Halima Khamis Ali Alipokuwa akifungua mafunzo ya siku moja kwa watumishi wanaitarajiwa kustaafu juu ya maandalizi ya kustaafu yaliofanyika katika ukumbi wa ZSSF Tibirinzi Chake Chake .
Amesema iwapo maandalizi ya mapema katika kuyakabili maisha baada ya utumishi yatafanyika changamoto za maisha afya ugonjwa na mengineyo ambazo zinawakabili wastaafu wengi wanaomaliza muda wa utumishi maisha bila ya utumishi yatakuwa ya kawaida yenye utaratibu unaoendana na jamii .
Akizungumza na watumishi hao wanaotarajiwa kustaafu Mkurugenzi wa Zssf Pemba Said Maalim Said amesema lengo la kutoa mafunzo hayo ni kuwasadia watumishi wa umma kuwa na uelewa juu ya matumizi sahihi ya hakiba zao walizoweka katika Mifuko ya hakiba mbali mbali ikiwemo zssf na kuweza kuendesha maisha yao watakapomaliza utumishi.
Kwa upande wake Meneja wa TCB tawi la Pemba Shomari Mrisho Amewaasa watumishi hao wanaotarajiwa kustaafu kuitumia benk hiyo katika kuendeleza vipaji vyao na fursa walizokuwa wameziwacha kutokana na kutumikia Taifa ikiwemo kufanya Biashara.
Nao baadhi ya watumishi hao wanaotarajiwa kustaafu wameishukuru Zssf pamoja na benk hiyo kwa kuwapa mafunzo hayo ya kujiandaa ambapo wamesema kutawasaidia kuondokana na changamoto na kujua namna ya kuzitumia hakiba zao katika kuendeleza maisha yao ya kila siku.
Mafunzo hayo ya siku Moja kwa watumishi wanaotarajiwa kustaafu yamekusanya watumishi kutoka taasisi za serikali mashirika pamoja na taasisi za umma ambapo mada juu ya matayarisho baada ya kustaafu, Namna ya kutumia hakiba na nywngizo zimewasilishwa kutoka kwa wakufuzi kutoka chuo cha Uhasibu Tanzania TIRA, Pamoja na Bank ya TCB.
Mwisho
Comments
Post a Comment