BONANZA LA 5 LA UTALII PEMBA KURUDI TENA, WANANCHI WAASWA KUJITOKEZA KUSHIRIKI KATIKA MICHEZO MBALI MBALI.


Na Amina Ahmed Moh’d, Pemba.
BONANZA la 5 la  Utalii Pemba (Pemba Tourisport Bonanza) kuanza Rasmi Tarehe 28 Mwezi huu wa 11  na kufikia Tamati Tarehe 3 Disemba ambapo wananchi kutoka maeneo mbali mbali Tanzania wameaswa kujitokeza kuchukua fomu  za ushiriki wa michezo mbali mbali    bila malipo yeyote.

Akitoa Taarifa  kwa wananchi kupitia vyombo vya habari mbali mbali  Mratibu wa kamisheni ya Utalii Pemba Hamad Amini  Ali  amesema lengo la bonanza hilo ni  kuunga mkono juhudi zinazoendelea kufanywa na rais wa Zanzibar Dk Hussein Ali Mwinyi katika kufanya utalii wa Kisiwa hicho kuwa endelevu pamoja  kutangaza vivutio na michezo mbali mbali   ya asili Iliyopo ndani ya kisiwa   hicho  na kuongeza idadi ya wageni wanaoingia kisiwani humo kwajili ya shughuli za utalii. 
  HAMAD AMINI ALI- MRATIBU KAMISHENI YA UTALII                                                     PEMBA. 

 Amesema   tayari maandalizi kupelekea bonanza hilo    maalum  la kuhamasisha utalii  wa kisiwa cha Pemba ambalo litafanyika katika wilaya zote kisiwani  humo yameshakamilika   ambapo jumla ya michezo   15 ya Asili inatarajiwa  kuhamasishwa katika bomamza hilo pamoja na kufanyika kwa shughuli mbali mbali za kijamii.

Hata hivyo Mratibu huyo amewataka waandishi  na wananchi maeneo mbali mbali kisiwani Pemba kujitokeza  kwa wingi katika  maeneo mbali mbali yatakayotumika kwajili ya michezo iliyoandaliwa katika bonanza hilo. 

 Kwa Upende wake Afisa Utalii Kutoka kamisheni ya Utalii Pemba Said Salum  Ali  amewataka wananchi kisiwani humo kuonfoa dhana ya utalii ni uhuni badala yake waendelee kuinga mkono serikali kupitia sekta hiyo kufanya utalii katika maeneo mbali mbali  kwajili ya kuongeza kipato kitakachotumika kuongeza maenedeleo nchini.
 
SAID SALUM ALI-AFISA UTALII  KASKAZINI, PEMBA. 
Aidha Amesema kuwa Bonanza hilo  limeandaa zawadi  nono kwa washindi   pamoja na washiriki wote ambao wanatarajiwa kushiriki katika michezo mbali mbali sambamba na kuendelea kusimamia maadili ikiwemo  utalii unaoendana na  uhifadhi wa mazingira ya kisiwa hicho. 

Michezo hiyo inayotarajiwa kushindaniwa katika bonanza hilo maalum la Kuhamasisha utalii  ni pamoja na Gwaride la Punda, ambalo litaanzia Tibirinzi  Chanjaani na kumalizia Pujini, Pamoja na Mchezo wa ng'ombe, Mbio za baiskeli, kukimbia , mashindano ya kuogelea,  Mpira wa fukwe,Taarabu asiliya, Mashindano ya dufu, mchezo wa bao, Ngoma, Mashindano ya ngalawa,  Mchezo wa Ngware,  Mashindano ya kula  vyakula vya Asili, matembezi ya utalii wa kiislam, Usafishaji wa fukwe,  sambamba na shughuli za  wajasiriamali kwa akina mama kwa utaratibu na siku maalumu .

Maeneo yatakayotumika kwajili ya mashindano ya michezo mbali mbali ni pamoja na Puniji, Vuma wimbi, Micheweni,  Msitu wa ngezi, Tibrinzi, Mkoani, pamoja na  Tumbe. 

 

Comments

Popular posts from this blog

BAJAJI WAMLILIA RAIS DK MWINYI PEMBA ,WAOMBA MSAADA KWAKWE WASEMA WAMECHOSHWA NA HILI KUTOKA MAWASILIANO

Masheha wanawake wa Wilaya ya Magharib B walivyoleta mabadiliko na maendeleo kwenye shehia zao.

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.