UWT TAIFA WAIPONGEZA SERIKALI UTEKELEZAJI ILANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI.

NA AMINA AHMED MOH'D PEMBA. 

MWENYEKITI wa umoja wa wanawake  UWT  Taifa   Mery Pius Chatanda amepongeza juhudi kubwa zinazofanywa na Rais Dr. Hussein Ali Mwinyi  ya kujenga miradi mikubwa ya Maendeleo  kwa wananchi wa visiwa vya Unguja na Pemba na kueleza Ilani ya CCM anaekeleza kwa kasi kubwa mno ambayo   haikuwahi kutokea. 

Akizungumza kwa nyakati tofauti Mwenyekiti huyo wa UWT  amempongeza Rais  Dkt Mwinyi  pamoja na rais wa Tanzania kwa juhudi   za kutekeleza ilani ya chama cha Mapinduzi  na kusimamia miradi mbali mbali ya maendeleo kwa wananchi ndani ya mkoa huo. 

Amesema kasi ya  ujenzi wa maendeleo katika miradi  iliyomo ndani ya mkoa huo itasaidia kuongeza zaidi uhai wa chama na jumuia zake  sambamba na kuendelea kuwatumikia wananchi  kwa kuitekeleza ilani ya chama cha Mapinduzi kwa Asilimia 100.

 Kwa upande wake akiwa katika kukagua mradi wa ujenzi wa Skuli ya ghorofa huko Kiwani Makamo Mwenyekiti wa UWT   Zainab Khamis Shomari  amesema haoni daliki za upinzani kufurukuta kufuatia miradi wenzeshi ya Maendeleo inavyoendelea kujengwa na serikali inayongozwa na Rais Dkt. Samia na Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi. 

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa kusini Pemba Mattar Zahor Massoud ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya siasa Mkoa huo amesema katika kujali hali  wananchi wa kisiwa cha Pemba serikali ya CCM inaendelea kuboreaha hali za wananchi kwa kuimarisha upatikanaji  huduma  bora. 

Nao baadhi ya Wakuu wa taasisi za serikali zilizopata kutembelewa na viongozi hao  wamesema suala la utatuzi wa jero  mbali mbali za wananchi wamekuwa wakizipa kipaumbele kufuatia maelekezo yanatolewa kwao na Rais Dkt Hussein Ali Mwinyi na kwa sasa kero nyingi zimeshapatiwa ufumbuzi huku jengine ziko endelea kwa kasi kubwa. 

Akielezea utekelezaji wa Ilani ya CCM ktk miundombinu ya Elimu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Leila Moh'd Mussa amesema Rais Dkt  Mwinyi tayari ashatekeleza kwa zaidi ya asilimia 150.

  Mwenyekiti huyo ametembelea  mradi wa nyumba za madaktari, Eneo la Maegesho ya Makontena nya mizigo banadari ya Mkoani, ujenzi wa  ZSTC Madungu, Ujenzi wa skuli Michakaini,  ukarabati wa uwanja wa  Gombani   ambapo pia  ziara hiyo imetembelea miradi mbali mbali ya maendeleo  ndani ya mkoa huo sambamba na kukabidhi kadi kwa wanachama 50  za wananchama wapya wa umoja huo. 

Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI