WAZEE WAGONJWA WAPATA FARAJA HII KUTOKA KWA MWAKILISHI NA MBUNGE WA JIMBO LA OLE.
Na, Amina Ahmed Moh’d - Pemba - 0719859184.
JUMLA ya Wagonjwa 15 Wamepatiwa Fedha kwajili ya Kusaidia Kupunguza Gharama za Matibabu ikiwemo kununua Dawa ikiwa ni Msaada Maalum uliofanywa na Mwakilishi wa Jimbo La Ole Massoud Ali Muhammed Pamoja na Mbunge wa Jimbo hilo Juma Hamad Omar.
Wagonjwa hao ambao wanaendelea kupatiwa huduma za matibabu Majumbani kutokana na Uzee wamepatiwa Msaada huo kufiatia ziara maalum ya kuwatembelea na kuwajulia hali iliyofanywa na viongozi hao wakiambatana na kamati ya Siasa ya Jimbo hilo Mapema Leo Asubuhi.
Akikabidhi Fedha hizo Mbunge Wa Jimbo hilo Amesema Uongozi wa Jimbo kwa Pamoja umeamua kufanya ziara hiyo na kutoa Masada ili kusaidia kuimarisha Afya zao na kurudi katika utekelezaji wa Majukumu yao kama ilivyokuwa Awali.
Aidha Akizungumza kwa niaba ya Mwakilishi wa jimbo la Ole Massoud Ali Diwani wa Wadi ya Vitongoji Hamad Abdalla Hamad Amesema kuwa Uongozi wa Jimbo utaendelea kufanya hivyo katika kutunza Na kuthamini Mchango Uliotolewa na wazee hao walipokuwa na Afya Imara Ikiwa ni pamoja na Mawazo mazuri ya kuchochea na kuhamasisha Maendeleo ndani ya Jimbo hilo.
Hata hivyo Uongozi huo umesema utaendelea kusaidia Zaidi Huduma za Matibabu kwa wagonjwa hao Pindi zitakapohitajika ambapo umewataka wauguzi wa wazee hao kuendelea Kutoa mashirikiano juu ya Hali ya upatikanaji wa huduma za matibabu yao ili kuendelea kuchangia Zaidi.
Wakizungumza Baadhi ya Wazee hao Akiwemo Mbwana Ali Omar mkaazi wa Vikunguni, Haji Abdalla Ali Pamoja na Mchanga Hamad Bakari Mkaazi Vitongoji wameushukuru uongozi huo kwa kuwasaidia fedha hizo ambapo wamewataka Viongozi wengine kuiga Mfano huo wa kuwatembelea na kuwafariji wazee Wanaoendelea kujiuguza Majumbani maeneo mbali mbali.
Jumla Ya Shilingi Laki 7 na 50 Zimetolewa kwa Wagonjwa hao ambapo pamoja na kuwatembelea lakini pia uongozi huo Uliwaombea Dua kuwafariji Pamoja na kupoke Ushauri juu ya mambo mbali mbali waliopewa na Wazee hao ambapo kila mmoja Alikabidhiwa Jumla ya shilingi elfu 50.
Mwisho.
Comments
Post a Comment