VIONGOZI WA JIMBO LA OLE WAPEWA KONGOLE UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO JIMBONI MWAO.

NA, AMINA AHMED MOH’D- PEMBA.    0776859184 


KAMATI ya Siasa Jimbo la Ole Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa kusini Pemba Imesema Imeridhishwa na kasi ya Maendeleo iliyofanywa na inayoendelea kufanywa na Viongozi wa Jimbo  Hilo katika Kuleta Maendeleo  ya Huduma bora Kwa Wananchi  ndani ya Jimbo hilo.


Akizungumza na Habari hizi  Mara baada ya kumalizika Ziara Maalum ya kutembelea na kukagua Miradi mbali mbali iliyotekelezwa na  Mwakilishi Massoud Ali Muhammed  pamoja  Mbunge wa jimbo hilo Juma Hamad Omar Mwenyekiti  wa kamati hiyo ambae pia ni Kiongozi wa Madiwani   Wilaya ya Chake Chake Hamad Abdalla Hamad  amesema  utekelezaji  wa miradi hiyo imeleta Tija na  Maendeleo  kwa Wananchi katika kurahisisha  huduma mbali mbali .
 HAMAD ABDALLA HAMAD  -  M/KITI MADIWANI CHAKE CHAKE. 

Kwa Upande Wake Mbunge Wa Jimbo la Ole Juma Hamad Omar  amesema  lengo la kuzipatia ufumbuzi changamoto  sugu  zilizokuwa zinawakabili wananchi   katika Jimbo hilo ni kuboresha na kutatua Changamoto za Wananchi  kama Ambavyo ilani ya Chama cha Mapinduzi Imeelekeza.

Aidha Akizungumza  kwa Niaba ya Mwakilishi wa Jimbo hilo   Massoud Ali Muhammed   Diwani wa Wadi ya  Vitongoji  Chake Chake Hamad Abdalla Hamad amesema lengo la kutekeleza Miradi mbali mbali ni kusaidia kuwaondoshea usumbufu  Wananchi  wa jimbo hilo   na kupata huduma bora. 

Aidha kwa upande wake   katibu wa Jimbo La Ole Kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Yakoub Halfan Shaha Amesema  kuwa  Ziara hiyo ya kukagua miradi mbali mbali iliyofanywa na Mwakilishi pamoja na Mbunge wa jimbo ni kuangalia namna ya utekelezaji wa Ahadi zilizotolewa na Viongozi hao  katika Kipindi cha Miaka 5   juu ya Utekekelezaji wa Ilani ya Chama.
 
Kamati hiyo Imetembelea na kujionea   Miradi  ambayo Tayari Wananchi ndani ya jimbo hilo wameanza kunufaika nayo ikiwa ni pamoja na   Barabara za ndani ,  Ukarabati na ujenzi Skuli Za sekondari, Ujenzi wa Holi la Mitihani  Sekondari, Upaatikanaji wa  Maji katika maeno mbali mbali yaliopelekwa mabomba  na Viongoz hao  Huduma ya Umeme na kumalizia katika Soko la mboga mboga pamoja  na Matunda la  Ubaya Sikitu Lililopo Ole Kianga ambalo tayari Wafanya Biashara  wameanza kutumia kwa Harakati Zao. 

 Mwisho. 

 

Comments

Popular posts from this blog

BAJAJI WAMLILIA RAIS DK MWINYI PEMBA ,WAOMBA MSAADA KWAKWE WASEMA WAMECHOSHWA NA HILI KUTOKA MAWASILIANO

Masheha wanawake wa Wilaya ya Magharib B walivyoleta mabadiliko na maendeleo kwenye shehia zao.

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.