ZFDA PEMBA YATOA ELIMU VISIWA VIDOGO VIDOGO JUU USALAMA WA CHAKULA, YATOA NA ANGALIZO KWA WAMILIKI WA MADUKA.
Na- AMINA AHMED MOH’D, PEMBA.
WAKAAZI wa Visiwa Vinne Kusini na Kaskazini mwa Kisiwa Cha Pemba wamefikiwa na Maafisa wa Vitengo mbali mbali Kutoka Taasisi ya Wakala wa Chakula Dawa na Vipodozi Na Kupatiwa Elimu Juu ya Usalama wa Chakula Ikiwa ni Maadhimisho Ya Siku Ya Usalama wa Chakula Duniani Inayoadhimishwa kila ifikapo Tarehe 7/6.
Akizungumza na Wanafunzi, Wananchi, Pamoja na Vijana Wa Kisiwa Cha Fundo Wilaya ya Wete katika Mkutano Maalum wa kutoa Elimu Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Wakala wa Chakula Dawa na Vipodozi ZFDA Ofisi ya Pemba Makka Khamis Ali Amesema kuwa Taasisi hiyo Kwa Upande wa kisiwani Pemba imeamua kutoa Elimu kwa Wananchi wanaoishi Maeneo ya Visiwa ili kuweka usawa wa Upatikanaji wa Elimu hiyo kwa wananchi wote Waliomo ndani ya Visiwa vidogo vidogo.
"Tunapita na kutoa Maeneo yote lakini Kuna utofauti kwa wananchi wanaoishi Katika Visiwa vidogo vidogo na Wananchi wanaoshi maeneo mengine Kutokana na sababu mbali mbali ni mara chache Wananchi wa Maeneo ya visiwa kufikiwa kupata Elimu hii ukilinganisha na wananchi ambao hawaishi visiwani hivyo Dhamira yetu ni kuona kuna kuwa na usawa wa Elimu hii ya Usalama wa chakula kwa Watu wote". Alisema Makka Kaimu Mkurugenzi ( ZFDA)
Alieleza kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imetoa Jukumu kwa Mamlaka hiyo kusimamia na kuhakikisha Usalama Wa Vyakula kwa wananchi wote, Hivyo Mamlaka h Itaendelea kutoa Elimu ya Usalama wa Chakula kwa ili kuweza kuhakikisha Wananchi wanaondokana na Madhara ambayo kwa kutumia Vyakula Visivyosalama yataweza Kuathiri Afya zao.
"Lengo la Maadhimisho haya ya Siku ya Usalama wa Chakula Duniani na tumeamua maalum kuifanya hapa, katika kisiwa cha Fundo ni kutoa Elimu na Uelewa kwenu nyinyi wananchi juu ya Kuweza kutambua vyakula Salama, na kuweza kuvitambua ili kuondokana na madhara yale yote yanayoweza kujitokeza kwa kutumia ama kula vyakula ambavyo sio salama. "
Aidha Kaimu Mkurugenzi huyo Alisema kuwa Taasisi hiyo katika kuhakikisha usalama wa Wananchi unapatikana Inaendelea kufanya ukaguzi katika Maduka ya vyakula Maghala, Wajasiriamali wa bidhaa, Vyombo ambavyo vinasafirisha Chakula, ili kuzidisha Uelewa kwa Wamiliki juu ya Kutunza na kuhifadhi Vyema Kwa Maslahi ya afya njema za wananchi wake.
Kwa Upande wake Mkuu wa kitengo cha Udhibiti na Usalama wa Chakula Aweza Hassan Haji amewataka wananchi hao Kuzidisha uangalifu katika kuhifadhi vyakula ili viepukane kuchafuliwa na vimelea vya Maradhi mbali mbali kemikali zisizo salama Takataka pamoja na Sumu kwa kuweka na kuandaa kwa mpangilio Sahihi.
Awali Akiwakilisha Mada kwa wananchi hao Kassim Fadhil Kassim aliwataka kutambua vyema majukumu ya Taasisi ya wakala wa Chakula Dawa na Vipodozi ZFDA kuwa ni pamoja na ukaguzi, usajili, Uchunguzi wa kimaabara sambamba na kuwataka kutambua Ubora wa chakula kwa kutumia njia hizo za kitaalamu.
Katika Hatua nyengine Taasisi hiyo Imewataka Wamiliki wa Maduka ya Vyakula kujiepusha Kuuza Dawa za kutibu Magonjwa ya Binaadamu ndani ya maduka hayo ambapo imesema kufanya hivyo ni kinyume na sheria na taratibu zilizowekwa.
"Tunaendelea kuwakumbusha Wamiliki wa Maduka kuwa Kuuza Dawa Tiba yayote katika Maduka ya Vyakula ni kosa kisheria endapo mmiliki hatokuwa na uthibitisho maalum utakaomruhusu kuuza, Dawa zote zinahitajika kuuzwa kwa utaratibu maalum na Maduka maalum, ZFDA haitisita kuchujua hatua Stahiki kwa atakaekwenda kinyume na suala hili " Alisema Mussa Muhammed Abdalla Afisa kutoka ZFDA Pemba.
Akitoa neno la Shukurani Kwa niaba ya Wananchi wa kisiwa cha Fundo Naibu Sheha Wa Shehia Hiyo Hadia Ali Juma ameishukuru Taasisi hiyo kwa Elimu hiyo ambapo amesema itasaidia kuongeza uelewa wa Wananchi kuweza kutambua Ubira wa vyakula kabla ya kutumia ili kuepusha madhara ya Afya Zao na kuahidi kuwa mabalozi kwa wengine juu ya Elimu hiyo.
Siku ya Usalama wa Chakula Duniani kisiwani Pemba imeadhimishwa kwa utolewaji wa Elimu katika Visiwa vya Kojani, Makongwe, Panza pamoja na Fundo ambapo Elimu juu ya Chakula Salama, Chakula Kisicho salama, Madhara ya Chakula kisicho salama Pamoja na Majukumu ya Taasisi hiyo ya ZFDA Ilitolewa kwa wananchi wa visiwa Hivyo.
Mwisho
Comments
Post a Comment