MWENGE WA UHURU WAFIKA WILAYA YA MICHEWENI PEMBA
Na Amina Ahmed Moh’d Pemba
JUMLA ya Miradi 5 ya Maendeleo katika Sekta ya Kilimo, Biashara, Elimu, Afya, umeme na Maji Yenye Thamani ya Shilingi Bilion 13 Milioni 349 Laki Moja 67 imetembelewa kukaguliwa na kuwekewa Mawe ya Msingi Katika Wilaya ya Wete Ikiwa ni Muendelezo wa Ziara Ya Matembezi ya Mwenge Wa Uhuru Nchini Ambao Uliwasili Katika Mkoa wa Kaskazini Pemba Mapema Jana Asubuhi huku kukimbizwa Umbali wa Kilo mita 80 katika Maeneo mbali mbali wilayani Humo.
Ameyasema hayo Katibu Tawala Wilaya ya Wete Mkufu Faki Ali Alipokuwa Akitoa Taarifa kwa Niaba ya Uongozi wa Wilaya hiyo katika Ghafla ya Makabidhiano ya Mwenge Wa Uhuru pamoja na Wakimbiza Mwenge huo kutoka Wilaya ya Wete kwenda Wilaya Micheweni kwajili ya kuendeleza Shughuli za Ufunguzi wa Miradi mbali mbali ya Maendeleo Mapemba Leo Asubuhi Katika Viwanja vya Skuli ya Msingi Finya.
Amesema kuwa Miradi hiyo Ambayo imekuwa Tija Fursa na Maendeleo ya Wananchi wa wilaya ya Wete zaidi ya shilingi Bilioni 7 Milion 491 Miatatu 34, ni Mchango Wa Serikali kwa wananchi wake Huku zilizosalia zikiwa ni Fedha kutoka kwa Wahisani mbali mbali Pamoja na Wananchi.
"Miradi iliyokaguliwa na Mwenge wa Uhuru Mwaka huu 2023 katika Wilaya ya Wete Imegusa moja kwa moja Maendeleo ya Wananchi katika sekta mbali mbali ambapo Serikali yetu ndio ambayo Imewekeza Fedha nyingi katika Miradi hiyo".
Aidha Alieleza kuwa Kupitia Mkesha wa Mwenge Wa uhuru katika Wikaya hiyo wananchi mbali mbali Waliweza Kutumia fursa Ya Kupima Afya zao ju ya Maradhi mbali mbali, ikiwemo Virusi vya ukimwi, Sambamba na wajasiriamali Kuuza bidhaa na kuweza kujipatia kipato.
"Neema hii ya Mwenge wa Uhuru imeleta tija kwa wananchi mbali mbali katika Wilaya ya Wete ikiwemo wajasiriamali Kutumia Shamra shamra hizo kuuza bidhaa zaona kujipatia Kipato, Pamoja na kupima Afya zao bure."
Aidha Kwa upande wake Kiongozi Mkuu wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2023 Ndugu Abdalla Shaibu ameutaka Uongozi wa Wilaya ya Micheweni Kutoa Mashirikiano Kwa Wakimbiza Mwenge hao ili kuweza Kutimiza Malengo Yao waliyakusudia
" Tumepata Mashirikiano na Tumeridhishwa na Miradi mbali mbali Tuliyoitembelea Katika Wilaya ya Wete Tuntarajia Mashirikiano Haoa katika Wilaya ya Micheweni ambapo Mwenge wetu wa uhuru Umepiga Hodi leo hii ili kuona Lengo kutembelea Na kukagua Miradi ya Maendeleo Linafikiwa Ipasavyo .
Kwa Upande wake Mkuu wa Wilaya Ya Micheweni Mgeni Khatib Yahya Amesema kuwa Uongozi Wa Wilaya hiyo Umeandaa na kuratibu vyema Shughuli za Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo katika Wilaya ya Micheweni.
Ukiwa Katika Wilaya hiyo Ya Micheweni Kiongozi huyo wa Mwenge wa Uhuru Ameshiriki Zoezi, la Upandaji wa Miti Katika Eneo la Kishindeni, Wingwi Mapofu, Kuweka Jiwe la Msingi katika Maabara ya Skuli ya Sekondari Shumba Viamboni, Ulazaji wa Mabomba ya Maji safi na salama Katika kijiji cha Kironjo Wingwi huku Ukitarajiwa Kuendelea na Ukaguzi wa miradi mbali mbali ndani ya wilaya hiyo Ambapo kauli mbiu ya Mwenge wa uhuru Mwaka huu ni Tunza Mazingira Okoa Vyanzo Vya Maji, kwa Ustawi wa viumbe Hai kwa Ustawi wa Taifa.
Mwisho.
Comments
Post a Comment