WIZARA YA UTALII PEMBA YAONGEZA KASI KATIKA USHAJIHISHAJI WA UTALII KWA WOTE YAAHIDI KUONGEZA MASHIRIKIANO KWA WATU WA RIKA ZOTE
- Get link
- X
- Other Apps
Na Amina Ahmed Moh’d Pemba
VIJANA Kisiwani Pemba Wameaswa kuzichangamkia Fursa zinazopatikana kupitia Sekta ya Utali iwa aina mbali mbali ili kiweza kujipatia kipato wao binafsi na kuleta Maendeleo kwa Taifa sambamba na kutembelea Pamoja kutunza maeneo ya kihistoria yaliyopo.
Ametoa Ushauri huo Mkuu wa Wilaya Wete Hamad Omar Bakari Alipokuwa Akizungumza nao Katika Warsha Maalum ya Uhamasishaji wa Utalii kwa Wote iliandaliwa na Wizara ya Utalii na mambo ya kale Huko Katika Makumbusho ya kihistoria Chwaka Tumbe Mkoa Wa Kaskazini Pemba.
HAMAD OMAR BAKARI - MKUU WA WILAYA YA WETE
Amesema Utalii umekuwa Na Fursa nyingi zitakazosaidia kuwapatia kipato binafsi na Taifa Endapo wataamua kuzitumia kwa kufanya shughuli mbali mbali ikiwemo kuutangaza Utalii Wa kihistoria uliopo kisiwani Pemba.
Akizungumza katika Warsha hiyo Ofisa Mdhamini wizara ya Utalii na mambo ya kale Pemba Zuhura Mgeni Othman amesema Wizara hiyo
itaendelea kushirikiana na vijana, Wajasiriamali pamoja na wananchi mbali mbali katika kuimarisha na kutangaza utalii Wa aina mbali mbali.
ZUHURA MGENI OTHMAN - AFISA MDHAMINI WIZARA YA UTALII NA MAMBO YA KALE PEMBA.
wakizungumza baadhi ya vijana wajasiriamali na wanafunzi ambao wamehudhuria katika warsha hiyo ya kuhamasisha utalii kwa wote wameipongeza wizara ya utalii Pemba kwa kuendelea kuhamasisha jamii juu ya utalii wa ndani ambapo wamesema kupitia hamasa hiyo wameweza kujifunza mambo mbali mbali ya kihistoria.
Warsha hiyo imehudhuriwa na wadau mbali mbali wa Utalii wakiwemo wadau wa hoteli, waongoza wageni, watu maarufu katika kijiji cha chwaka, Wajasiriamali, wanafunzi pamoja na mtalii wa kigeni kutoka Nchi ya Holanzi ambapo Warsha hiyo iliambatana na kutembelea makumbusho hayo yenye historia mbali mbali ya chwaka Tumbe.
Mwisho
- Get link
- X
- Other Apps
Comments
Post a Comment