WAZANZIBARI WAASWA KUUNGANA NA TAMWA-ZANZIBAR KUHUSU UONGOZI KWA WANAWAKE.


NA   AMINA AHMED MOH’D - PEMBA. 

BAADHI ya Viongozi wa Dini ambao ni Miongoni mwa Wanaharakati wa kutetea haki za Wanawake Kisiwani Pemba wamewataka wazanzibari  Kuungana na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Zanzibar TAMWA katika kuhakikisha Usawa wa kijinsia katika Ngazi za maamuzi Unafikiwa ifikapo  2025. 

Akizungumza na Habari hizi Mwanaharakati  wa Maendeleo ya Wanawake Pemba Pascal Nkuba Ambae pia ni Mchungaji wa kanisa Redeemed  Gospel Church   (RGC)    lililopo Minazini Chake Chake  Amesema  kutokana na Nia  na Dhamira Njema inayoendelea kuoneshwa na Taasisi hiyo   Wazanzibari wote wanaowajibu kuunga Mkono Juhudi hizo ambazo lengo lake ni kuongeza kasi ya Maendeleo kwa Wanawake. 

       MCHUNGAJI,   PASCAL NKUBA  - RGC  MINAZINI CHAKE CHAKE. 

"Tamwa   imekuwa Ikitoa Elimu kwa watu wote maeneo mbali  mbali na Makundi yote kuhusu Uongozi kwa wanawake   kwa Ishara hiyo tunao Wajibu wa kuiunga Mkono kufikia Malengo  hao abayo ni mema kwa wanawake. 

Aidha alisema kuwa ipo haja kwa  wadau na Makundi yote ambayo yamefikiwa  na Taasisi hiyo kuendelea kuhamasisha Jamii juu ya ushiriki wa  wanawake katika Uongozi na kuendelea kudai haki hiyo katika nyanja mbali mbali.

 "Binafsi nikiwa kama kiongozi wa Dini wa RGC  naendelea kutoa elimu kwa waumini wangu pamoja na kukemea vikali  kumkandamiza Mwanamke kwa  dhamira ya kubaki nyuma kimaendeleo, labda kwa kufanyiwa vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia, Au kunyimwa fursa ya kushiriki kutoa maamuzi na kumekuwa na mabadiliko kidogo kidogo wadau wa makundi ambayo yamefikiwa na Tamwa  Iendeelee kutoa elimu ambayo wamepatiwa "

Kwa Upande wake Fatma Hamad ambae  Mwanaharakati na Mwandishi wa habarikisiwani  alisema kuwa licha ya jamii kupata Uelewa ipo haja kwa Taasisi hiyo kuweka mpango mkakati ambao utasaidia kuikumbusha jamii juu ya suala la uongozi kwa wanawake   kila siku. 

"Tamwa na Taasisi nyengine Waendelee kutumia vyombo vya Habari vya aina mbali mbali, ikiwa ni radio, magazeti, mitandao, vipeperushi kufikisha ujumbe ambao Makundi yote yatakuwa na kauli moja kuelekea 2025 hii itasaidia kuongeza hamasa kwa jamii Alisema

" Mfano kuweke Kauli mbiu ambayo itakuwa ni endelevu Lakini itafikiwa na makundi yote  na itasikika kwa wote   mabadiliko yatafikiwa tu". 

Akizungumzia Suala hili  Sheikh Suleiman Said kutoka Mkanjuni ChakeChake Amewaasa waumini wanawake Kuitumia fursa hizi  za uongozi  kwa kufuata mafundisho ya Dini  bila kuenda kinyume. 

" Awali Waliowengi walikuwa wanaielewa vibaya hii Dhana ya Uongozi wapo ambao walikuwa wanashindwa kutofautisha ni upi uongozi unaopigiwa kelele na Asasi hii ya Tamwa  na Asasi nyengine lakini niseme tu  Kila mtu anaowajibu wa kuwa kiongozi akina uongozi ulioharamishwa kwenu sio huu ambao Tamwa wanaupigia kelele uwena usawa tumieni fursa". 

Kwa Upande wake Fat hiya Mussa Said Ambae ni Mratibu wa Chama  Cha Waandishi wa Habari Wanawake TAMWA Zanzibar Ofisi ya Pemba amesema Muamko kwa Jamii umeongezeka kufuatia elimu inayoendelea kutolewa juu ya masuala hayo ya uongozi na haki sawa kwa wanawake na wanaume ukilinganisha na Awali. 

 "Hali imebadilika awalo tulipoanza kutoa elimu juu ya sala hili wadau wakiwemo viongozi wadini walikuwa wakali sana hawakuwa wanataka kutoa hata mashirikiano yakutosha waliona kama tunapotosha Jamii lakini baaa ya kujengewa uelewa Tunashukuru wamekuwa wakituunga mkono na kusaidia kuondoa zile fikra Potofu a mawazo Mgando ambayo yamekuwa yamo katika akili za watu  "

 Aidha Mratibu huyo amewataka wananchi kisiwani Pemba Kuendelea kuunga mkono juhudi hizo zinazofanywa na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake  Zanzibar  kwa kushirikiana ma Wadau na Taasisi mbali mbali yenye lengo la  kuleta Mageuzi ya fikra na kukuza  Uchumi wa Wanake. 


Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake TAMWA Zanzibar ni Chama ambacho kimekuwa kikiendelea kupigania upatikanaji wa haki mbalo mbali za wanawake ikiwa ni pamoja na haki ya kushiriki katika ngazi za maamyzi, haki za uongozi, siasa Uchumi na Democrasia. 

Mwisho. 





Comments

Popular posts from this blog

BAJAJI WAMLILIA RAIS DK MWINYI PEMBA ,WAOMBA MSAADA KWAKWE WASEMA WAMECHOSHWA NA HILI KUTOKA MAWASILIANO

Masheha wanawake wa Wilaya ya Magharib B walivyoleta mabadiliko na maendeleo kwenye shehia zao.

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.