MAABARA YA AFYA JAMII KISIWANI PEMBA YAFUNGLIWA RASMI USUMBUFU WA KUCHUNGUZA MAGONJWA NJE YA KISIWA HICHO SASA BHASI.
Na Amina Ahmed Moh’d Pemba.
WIZARA ya Afya Zanzibar leo hii imepokea na kuzindua Rasmi Maabara ya Afya jamii kisiwani Pemba ambayo itasaidia kuchunguza magonjwa mbali mbali kwa wakati na uhakika jambo ambalo lilikosekana awali kisiwani humo na kupelekea usumbufu katika kuchunguza magonjwa mbali mbali.
Maabara hiyo ya kisasa ambayo imegharimu Shilingi Bilioni 3. 5 Fedha za Tanzania hadi kukamilika kwakwe ikiwa ni Utekelezaji wa Mradi American Rescue plan Act of 2021 ARPA ambao unatekelezwa na shirika la Usimamizi na Maendeleo ya Afya Menegment and Development for Health (MDH) kwa kushirikiana na Unicef , Pamoja na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, ikiwa ni Ufadhili wa Shirika la (U. S. CDC)
Akizungumza katika Ghafa hiyo Waziri wa Afya Zanzibar Nassor Ahmed Mazrui Amewataka Watendaji wa wizara hiyo Pemba kuitunza Maabara hiyo na vifaa vyake ili viweze kusaidia na kufikia lengo lililokusudiwa la kufanyika shughuli za Uchunguzi na upimaji kwa wakati na ubora unaoendana na kasi ya Sayansi na Teknologia.
Aidha Mazrui amelishukuru na kulipongeza shirika la( MDH) kwa kuendelea kuwa na Mchango Mkubwa katika kuimarisha Na kusaidia sekta ya Afya hususan katika upatikanaji wa uhakika juuYa Huduma za afya inazohitaji Uchunguzi wa Magonjwa mbali mbali na li kuimarisha Uchumi wa Zanzibar na kuongeza Kipato kupitia Sekta ya Utalii.
Akizungumza kwa niaba ya wananchi wa kisiwani Pemba Mkuu wa Mkoa wa kusini Pemba Mattar Zahor Massoud Amesema Maabara hiyo itasaidia kupatikana huduma za uchunguzi kwa haraka kwa wananchi wa kisiwani humo na kuondolea usumbufu wa kufata huduma za uchunguzi wa Magonjwa nje ya kisiwa hicho.
Akizungumza kwa Niaba ya Shirika la Usimamizi na Maendeleo ya Afya ( MDH) Daktari David Sando amesema shirika hilo limedhamiria kuondosha Changamoto za Upatikanaji wa Huduma za Uchunguzi wa Magonjwa ya kijamii kisiwani Pemba .
Nae Kwa upande wake Said Muhammed Ali Amabae ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Maabara ya Afya jamii kisiwani Pemba Ameahidi kutumiwa vyema Maabara na vifaa katika kuboresha afya katika Jamii kisiwani Pemba.
Ghafla ya Makabidhiano na Ufunguzi wa Maabara hiyo imefanyika Mapema leo huko Wawi Chake Chake ambapo maabara hiyo inatarajiwa kutumika kwa shughuli za Upimaji wa uchunguzi wa Magojwa mbali mbali ya wananchi Kusini na Kaskazini Pemba .
Comments
Post a Comment