ZAWA WAKUMBUSHWA AHADI WALIOIWEKA KWA WANANCHI GOMBANI NI KUHUSU KUMALIZA TATIZO LA MAJI SAFI NA SALAMA.

NA AMINA AHMED MOH’D - PEMBA. 
UONGOZI wa Shehia ya Gombani wilaya ya Chake Chake Umeikumbusha Mamlaka ya Maji Zanzibar Zawa Ofisi ya Pemba kuhusu Kukosekana kwa huduma ya Maji Safi na salama katika baadhi ya vijiji jambo ambalo limekuwa likiendelea kuwaathiri siku hadi siku walioahidi kulioatia ufumbuzi Mwanzoni mwa Mwezi wa January 2023.


 Akizungumza na  Mwandishi wa Habari hizi Sheha wa Shehia ya Gombani wilaya Ya Chake Chake Mkoa wa kusini Pemba Subira Khamis Kombo  Alisema kuwa  Licha ya Ahadi walioekewa  kutoka kwa Mamlaka hiyo Kuwa Suala la kukosekana kwa huduma hiyo ya Maji Safi katika baadhi ya vijiji vya Gombani kupatiwa ufumbuzi Mwanzoni mwa Mwezi huu  lakini bado   hakuna Taarifa zozote juu ya suala hilo.

 Alisema Wananchi wake bado Wanaendelea kusumbuka kutokana na kufuata Huduma hiyo Maeneo ya mbali huku waathirika wakubwa wakiwa ni wanawake  na watoto. 

"Tuliambiwa Tuvute Subra Mpka Mwanzoni Mwa Mwezi huu wa Januari 2023 Lakini Naona  kimya tu Ndicho  Kilichotawala  Sijui  hata Wananchi wangu niwajibu nini juu Ya Maji ya Zawa Alisema. 
  
 Akizungumza Asha Sleiman Mkaazi wa Gombani Alisema kuwa usumbufu huowanaokumbana nao Wakubwa na wadogo Katika baadhi ya Vijiji Shehiani humo unarudisha Nyuma Harakati zao. 

  Akizungumzia Suala hilo Kwa Niaba ya Mkurugenzi wa Mamlka ya Maji Zanzibar Zawa Ofisi ya Pemba , Afisa Mahusiano wa Mamlaka Hiyo  kisiwani Humo Sleiman Anass Massoud  Aliwataka Wananchi  Hao kuendelea kuwa Wastahamilivu  kwani Mradi  utakaonufaisha Upatikanaji wa Huduma ya Maji vijiji   Vya Gombani Umefikia Hatua Nzuri. 
 
"Matarajio Yetu  tulikusudia  Mwanzoni Mwa Mwezi huu Tatizo la Maji baadhi ya Vijiji Gombani libaki Historia tu Lakini Kutokana na Sababu zilizokuwa Nje ya Uwezo Wetu  Mradi huo Utamaliza Mwisho wa Mwezi wa March Mwaka huu 2023.

Anass Alitaja  Sababu hizo  na Kusema kuwa " Baadhi  ya  vifaa vyao Vya Ujenzi na ulazaji Mabomba Vilizuiwa Bandarini Unguja  Kwa hiyo Mafundi wakachelewa  Vilikuwa havitoshi kukamilisha kwa wakati Mradi, Mabomba, Viungo, Pampu, Saruji, Kokoto, Nondo, na Magari ya Kukorogea Zege" Alisema. 

Akizungumzia Suala la Utolewaji Taarifa kwa Wananchi juu ya Hatua za Ujenzi wa Mradi  huo   Sleiman alisema kuwa Mamlaka ilitumia vyombo vya Habari mbali mbali kuwajulisha wananchi. 

" Hatukumfata kila Mtu kwake lakini katika Media ZBC Redio Tv, na Radio Jamii na baadhi na Vikao vya Masheha Wilaya zote Tumewambia nini kinaendwlwa kwa sababu Mradi wa Maji Gombani ni moja kati ya miradi  inayotekelezwa kwa fedha za ahuweni ya Uviko 19.

Aidha alisema kuwa Mamlaka imelenga kuimarisha Huduma ya Maji kwa kuongeza idadi ya Visima vya Maji vitakavyo Hudumia Chake Chake ikiwemo Gombani. 
 
Shehia ya Gombani yenye wakaazi 4835 ambao wao ni Wanawake na Watoto wamekuwa wakishindwa kufanya shughuli zao kwa wakati kutokana na usumbufu  wa kukosa Maji  baadhi ya Maeneo  kwa Zaidi ya Miezi Saba Sasa na hulazimika kuyafata Masafa ya mbali   huku baadhi ya Maeneo kupata kwa Mgao usiku usiku ambapo Mnamo siku ya Tarehe 16/12  2022 Uongozi wa Mamlaka  ya Maji Zanzibar zawa ofisi ya Pemba walidai kuwa Suluhu ya Usumbufu huo itakamlika Mwanzoni mwa Mwezi huu kutokana na kuendelea kwa ujenzi wa mradi  visima pamoja na Ukazaji wa Mabomba yakusambazia Maji. 

Comments

Popular posts from this blog

BAJAJI WAMLILIA RAIS DK MWINYI PEMBA ,WAOMBA MSAADA KWAKWE WASEMA WAMECHOSHWA NA HILI KUTOKA MAWASILIANO

Masheha wanawake wa Wilaya ya Magharib B walivyoleta mabadiliko na maendeleo kwenye shehia zao.

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.