WANANCHI WAOMBA SERIKALI KUWASAIDIA KUPATA MELI TANGA PEMBA

Na AMINA AHMED MOH’D-  PEMBA. 

WANANCHI na Wafanya Biashara  wilaya ya Wete  Mkoa wa Kaskazini Pemba wanaochukua bidhaa mbali mbali kutoka Mkoa wa Tanga na kuleta Wilayani Humo Wamemuomba Rais  Wa Zanzibar Na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi DkHussein Ali Mwinyi Kuwasaidia  Usafiri wa uhakika  ambao utawarahisishia kusafiri wao na bidhaa zao.

 Wametoa Ombi hilo  Huko katika Bandari ya Wete  Mkoa wa Kaskazini Pemba walipokuwa wakizungumza na Kamati ya Ulinzi na usalama ya Wilaya hiyo iliyifika bandarini hapo kwajili yawafanya wanaosafirisha bidhaa kwa kutumia usafiri wa Baharini unaotambulika kwa jina la Majahazi na kutumia Bandari zisizo rasmi kushusha Mizigo yao ya biashara .

Walisema kutokana na kukosa usafiri  wa Uhakika wa kutumia kusafirisha bidhaa zao za Biashara  Hulazimika kupanda Majahazi wao  Pamoja na Mizigo yao Na kulazimika kushuka Bandari yeyote  ambapo hupelekea kuhatarisha Maisha yao wao na Mizigo yao ambayo ndio  Tegemeo lao la kuendesha harakati zao Kiuchumi. 

Kuna Changamoto zinatupata  sisi kama wafanya biashara ambao tunasafiri kufuata bidhaa nje ya kisiwa hichi  Tunazifata  Tanga, Tunalazimika kutumia Mbadala huu wasafiri na wafanya biashara kwutoka Pemba   Tunaiomba Serikali Itutafutie Mbadala ili kusijitokeze mambo  ambayo sisi hulazimika kuyafanya kutokana na kukosa mbadala Hamisa Apolinali  



Comments

Popular posts from this blog

BAJAJI WAMLILIA RAIS DK MWINYI PEMBA ,WAOMBA MSAADA KWAKWE WASEMA WAMECHOSHWA NA HILI KUTOKA MAWASILIANO

Masheha wanawake wa Wilaya ya Magharib B walivyoleta mabadiliko na maendeleo kwenye shehia zao.

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.