Wadau na Serikali Tuungeni Mkono Kujikomboa na umasikini

Na UWEISIYA KHAMIS - UNGUJA. 
UMOJA wa Kikundi  Cha Akina MamaJambo Nia   kinachojishughulisha na Ushonaji wa Mazulia, Vipochi, Kamba za Usumba, Mikoba ya Ukili, Pamoja na  Mashuka, Kilichopo Shehia ya Kiungoni Makunduchi Mkoa wa Kusini Unguja  Wameiomba Serikali Pamoja na wadau wa Maendeleo Kuwasaidia Kupata Soko la Uhakika la kuuzia Bidhaa zao pamja na Elimu itakayowasaidia kuongeza ujuzi katik Kazi zao wanazozizalisha.

Wakizungumza na Mwandishi  wa Habari  aliefika katika Ofisi zao zilizopo Mtaa wa  Sheba Makunduchi baadhi ya akina Mama  wa Umoja wa Kikundi  hicho  Akiwemo Fatma Ali Makame  Amesema  kukosa Soko la uhakika  pamoja na Elimu ya Uzalishaji  kunapelekea kurudisha nyuma harakati zao za Maendeleo kutokana na Kutegemea  kuendesha  maisha na familia zao kila siku kupitia Kazi wanazozizalisha. 
  AKINA MAMA KIKUNDI CHA JAMBO NIA -  MAKUNDUCHI 
Amesema Kupitia Shughuli wanazozizalisha  katika kikundi hicho   wameacha utegemezi na huendesha shughuli zao   ikiwemo kuwasomesha watoto, pamoja na kukidhi mahitaji yao mbali mbali.

Aidha Fatma Ambae pia Ni Mwenyekiti wa kikundi hicho  Amesema kuwa licha ya Changamoto hizo  kikundi cha  Jambo Nia  kimekuwa kimbilio kwa akina mama wengi na kusaidia majukumu Mengi ya familia katika Majumba yao ikiwa ni pamoja na ulipaji  wa ada  na ukataji wa Sare za watoto Skuli, na Madrsa.
       BAADHI YA BIDHAA ZINAZOZALISHWA
Akizungumza juu ya changamoto hiyo  Afisa Ushirika Wilaya ya Kusini Unguja Salum Abdalla Salum Amesema  Changamoto za Soko   Mtaji na Elimu  zinaendelwa kupatiwa ufumbuzi na Serikali ikiwemo Kujemgewa Masoko maakum ya kuuzia biashara zao. 

 Aidha Afisa huyo amewataka wanakikundi hicho kufuata utaratibu  ikiwa ni pamoja na kuomba Mikopo kuoitia wizara ya uwezeshaji wananchi kiuchumi Zanzibar il kuweza kuondokana na tatizo la Mtaji. 

Ushirika wa akina Mama hao Jambo Nia  ulioanzishwa Mwaka 2007 umekuwa ukipata fursa mbali mbali za kutangaza Biashara zao katika Sehemu za Maonesho  huku  jumla ya akina mama 42 wakiendelea kunufaika na kikundi hicho kinachozalisha bidhaa  mbali mbali za Mikono. 
Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

BAJAJI WAMLILIA RAIS DK MWINYI PEMBA ,WAOMBA MSAADA KWAKWE WASEMA WAMECHOSHWA NA HILI KUTOKA MAWASILIANO

Masheha wanawake wa Wilaya ya Magharib B walivyoleta mabadiliko na maendeleo kwenye shehia zao.

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.