UKOSEFU WA USAFIRI WA MELI YA TANGA PEMBA WANANCHI WAMLILIA RAIS KUTOLIFUMBIA MACHO.
NA AMINA AHMED MOH’D - PEMBA
WANANCHI Wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba Wamemuomba Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Hussein Ali Mwinyi Kuwasaidia Usafiri wa uhakika ambao utawarahisishia huduma za usafiri kutoka Pemba kwenda Mkoani Tanga kwa shughuli zao mbali mbali ikiwemo Kufuatilia ununuaji wa bidhaa za Biashara.
Wametoa Ombi hilo Huko katika Bandari ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba walipokuwa wakizungumza na Kamati ya Ulinzi na usalama ya Wilaya hiyo iliyifika Bandarini hapo kwajili ya kutoa Elimu kwa wananchi Waliokamatwa kutoka maeneo mbali mbali ya Wilaya hiyo wakisafiri kuelekea Mkoa wa Tanga kupitia Bandari zisizo Rasmi kwa kutumia Majahazi ya Mizigo.
Walisema kutokana na kukosa usafiri wa Uhakika wa kutumia Hulazimika kupanda Majahazi ya Mizigo Na kulazimika kushuka Bandari zisizo Rasmi ambapo hupelekea kuhatarisha Maisha yao na kupelekea hasara kwa Serikali.
Pamoja na Haya Mliosema Viongozi Wetu sisi kama Wananchi Tunakiri Tumekosea kutumia Bandari zisizo rasmi, Tatizo halitokwisha tunamuomb Mh Rais aone hii changamoto na Atupatie Ufumbuzi wa haraka haraka, Sio kama Tunapenda kupanda Majahazi, kwa kweli tunateseka, hakuna Mtu anapemda kuhatarisha Maisha yake lakini kuna dharura zinatubidi tufanye ivyo haziepukiki .
"Changamoto zinatupata sisi kama Wananchi usafiri wa Kutoka Pemba kwenda Tanga hamna , Tunaiomba Serikali Itutafutie Mbadala ili kusijitokeze mambo ambayo sisi hulazimika kuyafanya kutokana na kukosa Mbadala wa usafiri, ambao ni kusaidiwa kuletewa Meli maalum ambayo itasaidia kuchua Abiria wanaotoka Pemba kuelekea Tanga ili Wananchi wasiendelee kutumia Bandari zisizo Rasmi na kuingia hatiani Alisema. "Alisema Hamisa Apolinali Mwaliandi .
Kai Khatib kai ambae pia ni Mshirika wa usafiri wa Majahazi Kutoka Pemba kwenda Mkoani Tanga Alisema kuwa Kipindi hiki ambacho Usafiri wa Meli kutoka Tanga kwenda Pemba umekuwa Na usumbufu na baadhi ya Manahodha ambao hawajulikani kisheria na Ushirika huo ndio ambao hutumia Mwanya huo kuchukua wananchi na wafanya Biashara kwa kutumia Bandari zisizo rasmi.
"Tunatumia bandari Rasmi inayotambulikana kisheria Mambo yanayofanywa na Baadhi ya manahodha ambao hawatambulikani na ushirika Ndio hayo ambayo yanajitikeza wanatumia bandari bubu bila sisi kujua".
Akizungumza na Wasafiri hao waliokamatwa katika Bandari zisizo rasmi ikiwemo Mtambwe, Fundo, hiyo Kaimu wa Kamati ya Ulinzi na usalama ya Wilaya ya wete Mgeni Khatib Yahya Ambae Pia ni Mkuu wa wilaya ya Micheweni aliwataka wasafiri hao kuacha Mara moja kutumia Usafiri huo ambao sio rasmi kwa shughuli za kuchukulia Abiria pamoja na kutumia bandari bubu badala yake kutumia bandari Rasmi iliyowekwa na Serikali.
"Sisi kama Serikali Tunatambua kuwa siku Rasmi ya Haya Majahazi hapa katika Bandari ya wete Kaskazini Pemba ni Siku ya Jumanne, na Jumapili kuondoma Pemba kuelekea Tanga.
" Wananchi Napenda Mjue kwamba Usafiri wa Msahua, Majahazi Kutoka Tanga kuja Pemba, na kutoka Tanga kuja Pemba, kubeba Abiria Ni Makosa, Nyinyi abiria ambao Tayari mshafanya hivyo na wananchi mtambue hili, Kuanzia leo yeyote ambae atakamatwa ni lazima Sheria ichukue Mkondo wake, kwa Abiria na mnahidha Pia.
Aidha Mgeni Alisema kuwa Serikali ya Wilaya kwa kushirikiana na ...... Haitosita kusitisha safari kwa chombo chochote cha Majahazi ambacho kitachukua Abiria badala ya Mizigo na kutumia Bandari Bubu.
" Vyombo hivi havijasajiliwa kwajili ya kuchukulia Abiria Manahodha mlitambue hili, mnachukua Abiria Mkikamatwa Mjue Tutazuia vyombo visifanye kazi, tutaviweka pale juu bila Muhali kwa jambo hilo Tunafanya hivyo kwa kuzingatia Usalama wako Wewe Mwananchi .
Akizungumzia Malalamiko hayo yaliotolewa na Wananchi ambao ni abiria hao waliokamatwa katika Bandari zisizo rasmi Mwenywkiti huyo aliwataka wananchi kuwa waumilivu kutokana na kukosekana kwa Mwli inayifanya safari za Tanga Pemba kwa vile ipo Katika Matengenzo.
"Sote tunajua kama meli ambayo ilikuwa inafanya safari za pemba Tanga imeenda Servise ni kwa maslhi yenu wenyenu ingeendelea kutumiwa inheleta matatizo Mzigo wa lawama woote ungekuja kwa Serikali muendelee kiwa wastahamilivu alisema.
Wananchi hao waliokamatwa katika bandari mbalimbali zisizo Rasmi imekuja kufiatia ziara maalum iliyifanywa na kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Wete kwa kushirikiana na Mamlka ya Bandari wilaya ya wete ZRM wilaya ya wete pamoja na TRA.
Comments
Post a Comment