TUTAWEKA KIPAUMBELE SEKTA YA ELIMU ZANZIBAR NA KUIMARISHA MASLAHI YA WAALIMU

Na AMINA AHMED MOH’D PEMBA. 

RAIS  wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Hussein Ali Mwinyi Alisema Serikali yake  ina Dhamira Njema ya kuendelea  Kuzipatia Ufumbuzi Changamoto Zinazokabili Walimu Unguja na Pemba ikiwemo kuzipatia Ufumbuzi Stahiki zao   ili  kuongeza ufanisi wa utendaji  kazi zao, katika Kuleta  Mageuzi ya   Elimu Na kuwa katika Mfumo   Bora  wa Ufundishaji  utakaoendana na mabadiliko ya Sayansi na Teknologia . 


Aliyasema Hayo Katika Maadhimisho ya Siku ya Waalimu Duniani yalioambatana n Mkutano Mkuu wa Ufunguzi wa Uchaguzi wa Chama cha Waalimu  Zanzibar ZATU  uliofanyika Katika Ukumbi Wa ZSSF Tibirinzi Chake Chake Pemba Mapema Leo Asubuhi. 

Alisema Chanagamoto mbali mbali ambazo zimewasilishwa na wizara hiyo  ikiwemo  nyongeza ya Mshahara, Uhaba wa Madarasa , Posho la waalimu, Mafunzo  na Ajira  Waalimu,pamoja  na  marekebisho ya Mitaala  Serikali imezipatia ufumbuzi kwa Asilimia kubwa  hivyo Changamoto zinazoendelea kujitokeza  siku hadi siku katika kuimarisha Seketa ya Elimu  Zitaendelea kupatiwa ufumbuzi Kwa kushirikiana na Waalimu Serikali na Wadau mbali mbali. 

Alisema Dhamira ya Kwanza ni Kuendelea kutafuta vyanzo vya Fedha ambazo zitasaidia kuimarisha Zaidi uchumi wa Nchi ambao utapelekea kuimarisha Maslahi ya waalimu Nchini na kuimarisha Sekta Ya Elimu .
 
"Serikali Itaweka Kipaumbele katika Bajeti ya Sekta hii ya Elimu  kutokana na Mchango wao kwa Taifa ,Pamoja na kutafuta vyanzo vyengine vya Fedha  vitakavyosaidia kuimarisha   Elimu kwa ununuzi wa Thamani, Vitabu, Ajira kwa waalimu , Pamoja na vitu vyote ambavyo  vitasaidia kufundishia, Ni Dhahiri kuwa haja ya kufanya hivyo ni kubwa kwa sekta hii kutokana na ongezeko la Watoto Wetu  wanaohitaji kupata Elimu Ambayo ni Haki yao" . 

 Aidha   Aliwataka Waalimu kuona Umuhimu wa kuzitumia Fursa mbali mbali zilizopo za  Kujiendeleza kielimu  ili kuweza kupata Maarifa Mapya ya kufundishia  Wanafunzi kwa Uweledi Zaidi na kuweza kujijengea Heshima Kwa Jamii.

"Fursa za kujiendeleza kielimu hivi sasa zimezidi kuongezeka Nchini Vipo vyuo Vikuu, ambavyo mnaweza Kuvitumia katika  Kujiendeleza na Kuongeza Maarifa na kuongeza viwango vyenu vya Elimu." 

 Hata Hivyo Dk Mwinyi aliwataka Waalimu Kuimarisha Uhusiano  Kati yao na Wazazi wa Wanafunzi kwa kuwahimiza kuimarisha Malezi ya Pamoja , kwa watoto  ili kuwajengea Maendeleo na Mustakbali Mwema Wa Maisha ya Sasa na  ya Baadae. 

" Ili watoto waweze kuwa Na Madili Mema  Waalimu niwatake kuwa na Mashirikiano na wazazi katika Malezi ili kupata watoto ambao watajiepusha na Tabia hatarishi, na kuwa Raia wema  ambao watakuwa Tegemezi katika Maisha ya Baadae" . 

Akizungumzia Suala la Uchaguzi wa  Viongozi wa Chama Cha Waalimu  Zanzibar ZATU Dk Hussein Aliwataka Wanachama wa Chama hicho amabao ni waalimu  kuwa  Makini katika Kuchagua Viongozi bora  watakaofanikisha kusogeza mbele Maendeleo  Chama cha Waalimu. 

 Aidha Alisema kuwa Serikali itaendelea kulifanyia  kazi ombi  lilitolewa na Waalimu   juu ya kupata Tume  Maalum ya  Utumishi  Serikalini kwa  Waalimu   ambayo itasaidia  kuimarisha Maslahi ya Waalimu Nchini. 


Awali Akitoa salam za Wizara katika  Kilele cha Siku hiyo ya Waalimu   Waziri Wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Leila Muhammed Mussa  Aliwataka Waalimu Wakuu  nchini  kusimamia Mitaala Mipya iliyofanyiwa marekebisho  kwa Wanafunzi wa Skuli za Msingi.

Aidha aliwaomba waalimu kuendelea kujiunga na Chama hicho ili kukizidishia uhai  ambao utasaidia katika kutatua changamoto mbali mbali zinazowakabili waalimu kwa urahisi. 


Awali akisoma Risala kwa niaba ya Chama cha Waalimu Zanzibar ZATU Katibu Mkuu wa Chama hicho Haji Juma Omar Alisema kuwa Chama kimeweka Mikakati Endelevu ya Miaka 5 ikiwemo kujadili Maendeleo ya Chama hicho, Kuchagua Viongozi wapya, ambao watahimiza uwajibikaji kwa Waalimu, pamoja na kuunga Mkono juhudi zinazoendelea kufanywa na Serikali  ya Awamu ya Nane katika Kukuza  maendeleo ya Elimu. 

 Siku ya Waalimu Duniani huadhimishwa kila ifikapo February 12  Ambapo  Vyama vya waalimu kutoka nchi mbali mbali vikishiriki katika Maadhimisho hayo huku Chama cha Walimu Zanzibar ZATU kikiadhimisha siku hiyo kwa kufanya Mkutano Mkuu wa nane ambapo wananchama wa chama hicho Kesho  watafanya  uchaguzi wa  kuwachagua Viongozi wakuu wapya Watakaongoza chama hicho. 

Ambapo pamoja  Mkutano huo pia  Rais wa Zanzibar Alifanya ziara ya Kushtukiza katika Maduka ya vyakula  Katika Mji wa Chake Chake Na Machomanne kuulizia Bei ya Bidhaa ya Mchele   jumla na reja reja pamoja na kutaka kujua Hali ya upatikanaji wa bidhaa hiyo kutoka kwa wafanya Biashara. 

Mwisho. 






 





  


Comments

Popular posts from this blog

BAJAJI WAMLILIA RAIS DK MWINYI PEMBA ,WAOMBA MSAADA KWAKWE WASEMA WAMECHOSHWA NA HILI KUTOKA MAWASILIANO

Masheha wanawake wa Wilaya ya Magharib B walivyoleta mabadiliko na maendeleo kwenye shehia zao.

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.