Dimwa Aja na Mikakati Kuimarisha chama cha Mapinduzi.
- Get link
- X
- Other Apps
Na AMINA AHMED MOH’D PEMBA.
CHAMA cha Mapinduzi CCM Zanzibar Kimesema kitaendeleza Mazuri yanayofanywa na viongozi Chama Cha Mapinduzi ikiwemo kudumisha Amani, Umoja Mshikamano , kutetea Maslahi ya Chama, kuongeza idadi ya Wanachama Sambamba na kulinda Muungano kwa Maslahi ya Wananchi .
Ahadi hiyo imetolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Muhammed Said Dimwa Alipokuwa akizungumza na Wananchi, Pamoja na Wanachama wa Chama hicho kisiwani Pemba huko katika ukumbi wa Fidel Castro Wawi Chake Chake Mara baada ya Kumalizika kwa Mapokezi ya aina yake kwa Naibu huyo ikiwa ni Mara ya Kwanza kufika Kisiwani Humo Tangia kuteuliwa kushika Nafasi hiyo.
Alisema Dhamira Njema ya Chama hicho ni kuendelea kuwa Karibu na Wananchi kwa kuanzisha Darasa la itikadi kwa Ngazi za Matawi ambalo litasaidia kuongeza Uelewa na Wanachama Wengi zaidi katika Chama hicho ambao watasaidia kuongeza Mashirikiano, kudumisha Amani,na Mshikamano na kupelekea kuongeza Ushindi Mkubwa Katika Uchaguzi 2025.
Aidha Naibu huyo Amewataka wananchama hao kuacha Makundi na badala yake kuweza kuungana Pamoja katika kukiimarisha zaidi Chama Cha Mapinduzi, ambacho ni chachu Ya Maendeleo kwa Wazanzibari.
Naibu huyo Amewaahidi Wanachama hao kuwa ataendeleza Mashirikiano na viongozi wa Ngazi zote ikiwa ni Pamoja na kufuata Ushauri na kupokea maoni ambayo yatasaidia kujenga Uimara wa Chama.
Hata Hivyo Dimwa Alisema Chama Cha Mapinduzi kimedhamiria kuimarisha na kutoa kipaumbele katika Mambo Mbali mbali ya Maendeleo kwa Akina Mama na Vijana,ikiwemo kuwawezesha Kiuchumi.
Awali Akizungumza Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kusini Pemba Yussuf Ali Juma Alimpongeza Naibu katibu huyo kwa kuteuliwa kushika nafasi hiyo Zanzibar ambapo alisema kuwa Wanachama wa Chama hicho Kusini Pemba kitaendelea kutoa Mashirikiano katika kuona anakamilisha vyema utekelezaji wa Majukumu yake.
Kwa Upande wake Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mattar Zahor Massoud Amesema kuwa Ujio wa Naibu Huyo kutasaidia kuimarisha Mipango ya Maendeleo ambayo itasaidia kuimarisha Maendeleo kwa Wananchi wa Mkoa huo.
Wanachama kutoka Matawi Mbali Mbali Wameshiriki katika Mapokezi Ya Kumpokea Naibu katibu Mkuu Muhammed Said Dimwa Pamoja na Wajumbe wa Idara za Kamati Maalum ya Nec ambapo shamra shamra hizo zilianza Mapema Leo Asubuhi huko katika Ofisi kuu za Chama Chachani Mkoa Kusini Pemba zikifuatiwa Na Burudani mbali mbali za Ngoma, Nyimbo, na Michezo ya kiumbizi kutoka kwa Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi.
- Get link
- X
- Other Apps
Comments
Post a Comment