ZOYINA USHIRIKA ULIOFANIKWA KUANZISHA KIWANDA CHA UTENGENEZAJI WA SABUNI. MADUNGU CHAKE CHAKE CHACHU YA MAENDELEO NA AJIRA KWA VIJANA . WAJASIRIAMALI WALIOWENGI HUCHOTA UJUZI WA KUTENGENEZA BIDHAA KUPITIA MWANZILISHI WAKE WAMEANZISHA VIWANDA KATIKA MAENEO WANAYOISHI.
Na Amina Ahmed Moh’d - Pemba.
"MDOGO mdogo ndio mwendo " ni usemi maarufu unaohamasisha watu kutimiza malengo waliojiwekea hatua kwa hatua.
Naufananisha msemo huu baada ya ushirika wa ZOYINA kumiliki kiwanda kinachozalisha Sabuni kwa kutumia miti ya asili ikiwemo mti wa mronge, manjano karafuu pamoja na liwa ambazo hutumiwa kwa ajili ya dawa na urembo .
Kiwanda hicho huzalisha sabuni za maji, sabuni za vipande, Jiki, Scrub Pamoja na Udi ambacho kilianza harakati zake kidogo kidogo kikiwa na mtu mmoja pekee hadi leo hii imekuwa ni tegemeo la kujipatia kipato kwa vijana zaidi ya 20.
ZOYINA pia imekuwa ni moja kati ya vituo vya kujipatia Taaluma na ujuzi kwa akina mama kutoka maeneo mbali ambao hutumia ujuzi huo katika kujiajiri na kujipatia kipato cha kujikimu na familia zao.
ushirika wa ZOYINA ulianza kuzalisha bidhaa ya sabuni Ya vipande pekee lakini kwa sasa bidhaa mbali mbali zimekuwa zikizalishwa na ushirika huo.
Asili ya Jina la ushika wa Zoyina limetokana na Herufi za mwanzo za Mwanzilishi ambae mpka sasa ni mwenyekiti wa ushirika huo pamoja na herufi za mwanzo za majina za wasaidizi wa ushirika akiwemo makamo mwenyekiti, katibu pamoja na msaidizi katibu .
Baadhi ya vijana ambao kupitia ushirika huo uliofanikiwa kuanzisha kiwanda wanasema ukombozi waliopata imekuwa chachu ya kujikomboa kiuchumi.
Omar Issa Omar (29)Mkaazi wa Fueni Chake Chake Anasema kiwanda hicho kimekuwa mkombozi mkubwa katika maisha yake kwa vile sasa amepata sehemu rasmi ya kujipatia kipato cha kuendesha familia yake.
"Nilikuwa sina sehemu rasmi muda wote nashinda maskani, nilishauriwa nijiunge na kikundi cha Zoyina nashukuru nafanya kazi najipatia riziki yangu kupitia kiwanda hichi leo, kisingekuwepo sijui ningekuwa mgeni wa nani" .
" Ujuzi wa Kutengeneza Jiki ambao leo hii imekuwa ni moja kati ya biashara zangu zinazonipatia kipato na kuendesha shughuli za maisha yangu na familia yangu nimeupata kwa Zena Othman Yahya alinifundisha mwaka 2013 na mimi nafundisha na wengine ujuzi ule ule niliopata kwake".
Ni maneno ya Fatma Doto Shauri (47) Mkaazi wa Madungu Chake Chake
"Kazi yangu kubwa katika kiwanda hichi ni kupeki sabuni katika vifungashio baada ya kumaliza kutengenezwa inanipatia kipato, hakitoshelezi lakini kinasaidia kupunguza mahitaji yangu binafsi mimi pamoja na wanaonitegemea ".
Amini Juma Muhammed ni mfanya biashara za urembo umri (34) Anasema hufuata Bidhaa katika kiwanda hicho na kuuza mitaani kwa bei ya reja reja na kujipatia kipato cha kuendesha familia yake.
" Nachukuwa Sabuni za karafuu, Sabuni za Mronge, Scrub pamoja na Udi Pale kiwandani kwa bei ya jumla na mimi narandisha mitaani kwa bei ya reja nanunua na bidhaa nyengine za urembo madukani narandisha na inanipatia tija siku Zoyina inanisaidia kwa njia hiyo kiupande wangu.
Baadhi ya Vijana ambao wanaendelea kunufaika kupitia kiwanda hicho ni wale ambao wamepata ajira za muda kufanya shughuli mbali mbali wanasema wanatamani fursa hiyo ingekuwepo kila siku katika maisha yao.
"Mimi binafsi natamani hichi kiwanda kiwe na uwezo wakutuajiri moja kwa moja isiwe kama hivi kazi za siku tu , kwanza mashirikiano ya bosi wetu hayakufanyi uchoke unafanya roho radhi Alidai Hafidh Said
"Kwa sasa hii ni ajira yangu ya muda lakini matumaini yagu ya baadae ni kufanya kazi hapa hapa kwa sababu najipatia ujuzi kadri ninavyokuja kufanya kazi huenda nisipopata hapa bhasi nikaanzisha kiwanda changu kwa ujuzi ambao ninazidi kuona hapa" Idrissa Ali Zahor.
Mafunda Hamad Rubea Ni sheha wa Shehia ya Madungu anasema kuwa kiwanda hicho kimekuwa mfano katika shehia yake kwa kuonesha wigo kwa vikundi vyengine lakini pia kutoa msaada kwa vijana kujipatia kipato.
" Uongozi wa shehia tunatambua na kuthamini juhudi zilizofikiwa na kikundi cha Zoyina na sisi tunaendelea kutoa mashirikiano katika kuona kinafikia malengo iliyoyakusudia.
Aliendeleza kuwa" Vipo vikundi ambavyo kutokana na kukosa umakini vimekosa mkopo vikiendelea kjiimarisha zaidi kufikia fursa hiyo lakini utayari na moyo wa kujitolea kufikia maendeleo kwa kiongozi wa kiwanda cha Zoyina Zena Yahya Othman leo hii ni kikundi pekee katika shehia yangu kilichopata mkopo wa pesa nyingi za kuendeleza shuguli za ujasiriamali ni jambo la kujivunia".
Moja kati ya vipaumbele vya Serikali ya Awamu yanane ya Dokta Hussein Ali Mwinyi ni kuwatambua rasmi wajasiriamali kwa kuwapatia vitambulisho maalum, Kuwawezesha kiuchumi kuwapatia elimu ya ujasiriamali, Lakini pia Kuwapatia Mikopo itayaosaidia kuendeleza shughuli zao wanazizifanya.
Tarehe 24/9/2021 katika ukumbi wa Sheikh Idrissa Abdul wakil Kikajuni Mjini Unguja Dk Hussein Ali Mwinyi Rais wa Zanzibar Alipokuwa akizindua mfumo wa utolewaji wa vitambulisho vya wajasiriamali Alitangaza na kusema kuwa Serikali ya awamu ya nane imekwisha tenga Jumla ya shilingi Bilioni 50 pamoja na kufanya mazungumzo na mabenki mbali mbali nakuwa tayari kuongeza Bilioni 50 kwa ajili ya kupatiwa mikopo kwa wajasiriamali wadogo wadogo Unguja na Pemba.
"Nimeanza kufanya mazungumzo na taasisi za fedha kwa lengo la kutafuta njia bora za kushirikiana na kutafuta namna bora ya kutoa mikopo hiyo kwa wananchi na bahati Nzuri benki ya CRDB imeonesha hamu kubwa ya kutaka kushirikiana na serikali katika kufanikisha utoaji wa mikopo hiyo".
Waswahili wanasema " Kuvuja kwa pakacha Ni Neema kwa Mchukuzi Ndivyo ninavyofananisha msemo huu Ushirika wa Zoyina kupata Neema iliyotangazwa na Rais wa Zanzibar Dk Hussein Siku ya tarehe 24 huko Kikwajuni lakini pia Maeneo mbali mbali alimokuwa akigusia suala hili.
Zena Othman Yahya ni Mwenyekiti na Mwanzilishi wa ushirika wa Zoyina cooperative ambapo anasema Haikuwa kazi rahisi kufika hapo alipo sasa katika kukuza ushirika huo hadi kumiliki kiwanda ambacho ni fursa ya vijana kujipatia kipato, Kuwa ushirika darasa kwa wajasiriamali lakini pia Kupata mkopo wa Serikali.
Kitu pekee kilichonifikisha hapa ni moyo wa kutokata tamaa subra pia, vikwazo ni vingi lakini nilisimama sikuchokaniliamini ninaweza na kweli leo hii nimekuwa tegemeo na mkombozi kwa waliowengi ".
" Kiukweli nilianza mbali mwaka 2003 nikiwa peke yangu nilianza kwa mtaji wangu mwenyewe kutengenza scrub kupitia miti asili, niliona kuna haja kutafuta elimu zaidi kutengeneza izi bidhaa na nikamtafuta baba mmoja mkaazi wa wete ambae alikuwa anafanya kazi ushirika wa viwanda vidogo alikuwa anakuja nyumbani kwangu kunifundisha na mimi nilkuwa namlipa,nilibaini kuna fursa za kujikwamua naweza kutengeneza nikapata kipato nikafanya hivyo".
"Niliendelea kidogo kidogo mwaka 2008 nikaanza kuunda kikundi baada ya kuona shughuli zimekuwa nyingi nikiwa sina msaidizi kilianza watu 40 wanawake 34 wanaume 6 kukosa moyo wa kujitolea kulipelekea kuondoka mmoja mmoja siku hadi siku mpka kubakia watu saba wanaume 6 na mimi pekee tunaendelea vyema mafanikio yanaendelea kuoatikana mpka leo hii tunashukuru.
"Jambo la kushukuru waliondoka wote waliondoka wakiwa tayari wanaujuzi wakutosha katika utengenezaji wa vitu mbali mbali na waliowengi wanaendelea kutumia ujuzi huo".
Mwenyekiti wa Ushirika wa Zoyina - Zena Yahya Othman.
"Nimetoa elimu ya vitendo katika taasisi mbali mbali za elimu hapa pemba ikiwemo Skuli ya Msingi Madungu jinsi ya kutengeza sabuni, Chuo Cha ufundi Rans nimevifikia vikundi mbali mbali kutoa elimu hii na humo mote ilikiwa nakusanya wanawake zaidi ya 40 darasa moja kuwapatia ujuzi huu Wapo walikuwa wakinipigia simu kunishukuru baada ya kuanzisha shughuli zao".
Licha ya Mafanikio hayo lakini pia Mwenyekiti huyo alisema kuwa kwa sasa changamoto inayowakabili ni ukosefu wa soko la uhakika la kuuzia bidhaa zao wanazozizalisha ambapo kupitia makala hii akaiomba Serikali pamoja na wafadhili mbali mbali kusaidia kulioatia ufumbuzi suala hilo.
MATUMAINI YA BAADAE.
Hata Hivyo Zena alieleza mipango ya baadae ya ushirika wa Zoyina ni kutoa fursa za ajira za kudumu katika kiwanda hicho kwa watu 8, kuzalisha uzalishaji zaidi kutoka michi 5000 hadi kufikia 10000 pamoja na kutoa ajira zisizo rasmi 100 kwa vijana.
" kwa sasa ajira zisizo rasmi ni 25 vijana wanakuja wala wanapeki wale wanasambaza mitaani malipo ya siku lakini malengo ya baadae ni kupata vijana hawa 100 watakaofanya kazi hizi, ushirika una wafanya kazi 6 ambao wa najipatia mshahara kwa mwezi malengo ya baadae ni kuongeza tena Wafana kazi 8 amabao watapa ajira za kudumu haoa katika kiwanda hichi".
Hivi karibuni Kiwanda hicho kimepata bahati ya Kupata Mkopo Wa Enuka kiuchumi wa Shilingi Milioni 25 Unaoendelea kutolewa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa wajasiramali ambao lengo lake ni kuwezesha wajasiriamali ambapo Zena anasema
" Mkopo wa benki nimepata bila usumbufu wowote kwa sababu nilikuwa na vielelezo vyote muhimu vya kuaminika , wengine wamekosa fursa hii kutokana na kukosa vile vitu muhimu benki wanavyovihitaji kama vithibitisho vya kupatiwa mkopo kama wajasiriamali unaodelea kutolewa na Rais kwa wajasiriamali "
" Mkopo umeniongezea kasi ya utendaji awali tulikuwa tunazaisha lakini kwa mikono na mashine ambayo ilikuwa inazalisha kwa wingi michi 100 lakini Mkopo umesababisha kupata mashine ambayo inazalisha michi 5000, tunaagiza malighafi kwa wingi ukilinganisha na awali, tumepata ofisi yetu wenyewe jambo ambalo awali tulikuwa tunalipia kodi kupitia mkopo.
Ni maneno ya Zena hayo Mweyekiti wa Zoyina Cooperative.
Issa Othman Muhammed ni mume wa Mwenyekiti wa Zoyina anasema Ushirika huo unaosimamiwa na mke wake umekuwa msaada mkubwa katika familia yao katika kukidhi mahitaji na matumizi ya familia.
Baadhi ya wananchi ambao wanatumia Bidhaa za sabuni ya Mronge, Karafuu, n Manjano pamoja Scrub zinazozalishwa na kiwanda hicho wamezungumza na mwandishi wa Makala hizi ambapo wamesema Sabuni hizo zimekuwa tiba na zinaendelea kutunza urembo wa ngozi na miili yao.
" Hivi karibuni mwanagu alifanya Pele za Tete nikawa na mpka mara kwa mara povu la sabuni ya Mronge wiki tu zilififia hzikurudi tena ". Fatma Salum Sefu maarufu Mama duli mkaazi wa karibu na kiwanda hicho cha Zoyina kilichopo Madungu Mwanamashungi Chake Chake.
" Sabuni Ya karafuu inanifaa sana uso wangu umekuwa hauna mafuta tangu nimeanza kutumia sabuni hii na natumia kila siku kusafishia uso Kauthar Hakim (21).
Mimi natumia kwa mda sasa inansaidia kuondoa mmba kwenye ngozi yangu umepungua kwa kaisi kikubwa ukilinganisha na awali nilivyokuwa
Alisema Baba Is-haka ambae jina lake kamili hakutaka liandikwe katika makala hii.
Jukumu la Uwakala wa uwezeshaji wananchi kiuchumi ni kutoa taaluma ya uzalishaji, Mtaji kwa wananchi, wajasiriamali wa vikundi, binafsi, pamoja na wawekezaji wazawa uzalishaji wa bidhaa zenye ubora masoko, ushawishi wa uwekaji miundo mbinu pamoja na kuboresha uzalishaji kwa mbinu za kisada.
Mratibu wa Wakala wa Mifuko ya Uwezeshaji wananchi kiuchumi Pemba Haji Khamis Haji anasema uwakala huo unaendelea na shughuli za uwezeshaji kwa wajasirimali wa aina mbali mbali ambapo wa wanawake pekee wametengewa asilimia 35 ya fedha zote zilizotolewa sawa na shilingi bilioni 280 kati fedha zilizotolewa kwa ajili ya kuwawezesha wajasiriamali wadogo wadogo kupata mkopo.
Sheria ya wakala wa uwezeshaji wananchi kiuchumi Zanzibar mwaka 2022 katika ukurasa wa 14 haikuwaacha nyuma wajasiriamali wanawake katika makundi mabli mbali ambapo imeweka na kutaja wazi makundi ya wajasirimali wanawake wanayo haki ya kupata fursa ya kuwezeshwa kiuchumi kwa kupatiwa taaluma, mitaji pamoja na kujengewa uwezo na mazingira rafiki ya kuendesha shughuli wanazofanya.
Mwisho.
Comments
Post a Comment