Wananchi wapewa wito Kuhusu VVU

Fatma Abrhman 


JAMII nchini imetakiwa kutokupuuzia kuhusu gonjwa la 
 Ukimwi, kwani bado upo na unaendelea kuwa tishio kwa maisha ya watu katika makundi na rika zote Ulimwenguni .

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar  Othman Masoud Othman, ametoa kauli hiyo huko Viwanja vya  Skuli ya Msingi Jadida Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba  katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani .

Amesema ni vyema kila mmoja kuwa ni askari wa kupinga vita tatizo la Ukimwi   na kwa pamoja kukemea vitendo vinavyosababisha maambukizi ya makusudi au hata ya bahati mbaya  sambamba na kulaani udhalilishaji wa aina zote na kuepuka kuwanyanyapaa wagonjwa wa maradhi ya Ukimwi.

Akizungumzia hali halisi ya Ugonjwa huo hapa Zanzibar Makamu  Othman amesema jitihada zinafanyika katika kuyafikia  malengo  kupambana  na maradhi ya Ukimwi na hadi kufikia Disemba 2021 idadi ya maambukizo mapya  imepungua  kwa asilimia 32 ingawa lengo ilikuwa ni kuzuia maambukizi hayo kwa asilimia 83.

Aidha amesema kiwango cha maambukizo mapya kwa  vijana wa kike kimeongezeka kwa mara tano zaidi ya malengo yam waka 2025, huku utumiaji wa kinga kwa makundi maaulum nao ukipungua na  kufikia baina ya asilimia 27 hadi 53 ikiwa ni asilimia ndogo ya kuweza kuyafikia malengo yaliyowekwa ya kuondosha tatizo hilo nchini ifikapo 2030.

Kutokana na hali hiyo Mhe. Othman amezitaka Tume za Ukimwi , Wizara ya Afya  pamoja na wadau wengine kushirikiana na kuzifanyia tathmini takwimu za tatizo hilo zilizopo ili kubaini vyema makundi ya jamii ambayo hayafikiwi na huduma hizo pamoja na kuongeza ufanisi katika kuzifikia shabaha na maelengo ya kuondoa Ukimwi kabisa Zanzibar ifikapo 2030.

 Kwa upande wake waziri  wa nchi Afisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar  Mhe. Harous Said Suleiman, amesema serikali kupitia Tume ya Ukimwi na kwa mashirikiano na wadau mbali mbali wamekuwa wakifanya jitihada kubwa za kutoa elimu ikiwa ni jitihada za kupambana vyema na maradhi hayo sambamba na kuzuia maambukizi mapya ya Ukimwi.

Nae  Mwenyekiti wa Tume ya Ukimwi Zanzibar Dk. Ali Salim amesema  ukosefu wa usawa katika upatikanaji wa huduma za maradhi ya ukimwi ni changamoto hasa katika kuyafikia makundi maalum ambayo yanaathirika zaidi na maradhi hayo. 

Naye Mwakilishi kutoka Mahirika ya Umoja wa Mataifa George Loy amesema  katika kupambana na maradhi hayo ni vyema kwenda na mpango wa vipaumbele zaidi ikiwemo kongeza jitihada ya kutafutwa fedha ambayo ni changamoto kubwa katika kukuza ufanisi wa kuyakabili maradhi hayo sehemu mbali mbali duniani.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Kaskaszini Pemba Salama Mbarok Khatib amewataka wanaume na wanawake kubadili mtazamo  ili kuhakikisha  wanaepukana na ushawishi wa kuwepo maambukizi mapya ya maradhi ya ukimwi Zanzibar.

Amesema  mkoa wake utaendelea na jitihada mbali mbali zitakazoasaidia kuongeza uelewa kwa jamii na hasa vijana kuachana na ,masuala yote yanayoweza kusababisha maradhi ya ukimwi ikiwemo kuachana na tabia ya kuwa na wapenzi wengi jambo ambalo ni hatari zaidi kwa maambukizi mapya ya maradhi hayo.

Comments

Popular posts from this blog

BAJAJI WAMLILIA RAIS DK MWINYI PEMBA ,WAOMBA MSAADA KWAKWE WASEMA WAMECHOSHWA NA HILI KUTOKA MAWASILIANO

Masheha wanawake wa Wilaya ya Magharib B walivyoleta mabadiliko na maendeleo kwenye shehia zao.

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.