SHIJUWAZA Yatoa msaada kwa watu wenye ulemavu Pemba.



NA AMINA AHMED MOH’D 

Jumla ya Familia saba  za watu wenye ulemavu  pamoja na  mazingira magumu    zimepatiwa  Msaada wa Chakula  ikiwemo Unga Sukari na  Mchele  kutoka Shirikisho  la jumuia za  watu wenye ulemavu Zanzibar Shujiwaza.

 Akizungumza katika ziara maalum ya kuzitembelea familia hizo katika familia maeneo mbali mbali kisiwani Pemba ikiwa ni shamra shamra za kuelekea  siku ya watu ulemavu  duniani   Mwenyekiti wa Shirikisho  la  Jumuia ya watu wenye ulemavu   Mwadawa Khamis Muhamed  Aliwataka wasimamizi  wa familia  hizo  kujiunga na jumuia za watu wenye ulemavu ili kuweza kupata haki zao mbali mbali. 

Amesema  watu wengi wenye mahitaji maalum wamekuwa wakipata haki zao muhimu baada ya  kujiunga katika vyama  na jumuia mbali mbali na kubadisha maisha  yao kiuchumi.  

 Tumeamua kufanya ziara hii ambayo ni maalum kuwatembela watu wenye ulemavu kuwafariji lakini pia  kuwatia moyo kuona kama hawako eke yao  tinawajali na kuwathamini  niwaombe wasimamizi kuona umuhimu wa kuwasajili katika jumuia   mbali mbali ili kupata fursa  watakapokaa ndani tu hazitowafikia. 


   Ali  Hassan Ali  Afisa  kutoka baraza la watu wenye ulemavu  Zanzibar kutoka   wilaya ya Micheweni Amesema Baraza hilo  litaendelea kutoa mashirikiano kwa jumuia zinazoendelea kusaidia watu   wenye ulemavu  kwa katika kushirikiana kutatua changamoto mbali mbali zinazowakabili  watu hao. 
Baraza kama serikali tutaendelea kutoa mashirikiano ikiwa ni pamoja na kusaidiana na jumuia mbali mbali kutatua changamoto zinazowakabili watu wenye ukemavu tutaendelea kushirikiana kuwapatia mahitaji yao muhimu ikiwemo visaidizi mwendo. 


 Nae Kwa upande wake  Afisa Mtendaji Kutoka Shirikisho la  jumuia za watu wenye ulemavu  Pemba  Aisha  Abdalla Juma  Aliwataka wazazi na walezi Kisiwani  humo kutoa mashirikiano katika kutetea haki za watu wenye ulemavu sambamba na kuacha ubaguzi katika malezi na uahirikishwaji  katika mambo ya maendeleo.

  Kila mtu Anapaswa kutoa mashirikiano kwa watu wenye ulemavu  kusimamia kupata haki zao ikiwemo haki hii ya kutambulika hivyo tunawajibu wakuwashirikisha katika mambo ya maendeleo ambayo wanayafanya. 


Wakizungumza baadhi ya Wanafamilia hao  waliopatiwa msaada huo na  shirikisho la jumuia za watu wenye ulemavu  wameshukuru  kitendo hicho walichofanyiwa ambapo wameziomba taasisi na jumuia nyengine kuiga mfano huo  wa shirikisho kuwasaidia na kuwatatulia changamoto zao zinazowakabili. 

 Tumepokea msaada huu kwa furaha sana kwani ni wachache wenye mioyo ya  kusaidia tunawaomba na wengine waige mfano huu kutusaidia changamoto nyengine ikiwemo sehwmu za kukaa na kufanya shughuli zetu.  
Alisema   Time Ramadhan juma mtu mwenye ulemavu Micheweni majenzi amabae pia ni mjasiramali wa ushoni. 

    Msaada huo umetolewa katika Eneo la   Inga ndugu Mvumoni , Mbuzini, Chake Chake, Sizini,  Mibrani  konde, Pamoja na  Micheweni   kwa haji shehia ya   Majenzi.

 Mwisho 


  


Comments

Popular posts from this blog

BAJAJI WAMLILIA RAIS DK MWINYI PEMBA ,WAOMBA MSAADA KWAKWE WASEMA WAMECHOSHWA NA HILI KUTOKA MAWASILIANO

Masheha wanawake wa Wilaya ya Magharib B walivyoleta mabadiliko na maendeleo kwenye shehia zao.

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.