E Goverment yasema haya kwa mawakala wa mtandao.
Amina Ahmed Moh’d.
Mkurugenzi Mtendaji Wakala wa Serikali Mtandao Zanzibar Said Seif Said Amewataka watoa huduma wanaotumia manunuzi kupitia mfumo wa mtandao (E - PROCUREMENT) ambao hawajajisajili rasmi kuitumia fursa ya kujisajili ili kupata fursa ya kushiriki katika ushindani wa kupata zabuni na ununuzi wa vitu vya serikali.
Ametoa wito huo Alipokuwa akizungumza na watoa huduma kutoka maeneo mbali mbali kisiwani pemba katika mkutano maalum wa kusikiliza maoni ya watumiaji wa mfumo huo uliofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Rais Fedha na Mipango Gombani Chake Chake pemba mapema Leo Asubuhi.
Amesema Lengo ni kuweka uwazi katika utumiaji wa mifumo na utowaji wa zabuni na ununuzi wa vitu vyote vya Serikali jambo ambalo awali halikuwepo kutokana na kukosekana kwa mfumo huo.
Aidha Mkurugenzi huyo Amesema kuwa mamlaka hiyo itaharakisha kuzipatia ufumbuzi changamoto zilizotolewa na Watoa huduma hao ili kuwaondoshea usumbufu na kasoro ndogo ndogo zinazowapa usumbufu katika utumiaji wa mfumo huo.
Mkutano huo wa siku moja kwa watoa huduma wanaotumia manunuzi ya vitu vya serikali kupitia mfumo mtandao umejadili mambo mbali mbali ambayo yatasaidia kuboresha mambo mbali mbali katika mfumo huo ambapo watoa huduma wa vitu mbali mbali ikiwemo vifaa vya magari, vifaa vya ofisini, pamoja na watoa huduma za vyakula washiriki na kutoa maoni yao katika mkutano huo ambaoo awali waliiomba mamlka hiyo kuwapunguza makato pamoja na kuweka uwazi katika vitu mbali mbali vinavyofanyiwa manunuzi.
Mwisho
Comments
Post a Comment