Wamiliki wa Vyombo vya habari vya Mtanadao fuateni sheria za habari.

Na AMINA AHMED MOH’D 

Wamiliki wa Tv radio na magazeti ya   mitandao Kisiwani pemba Wametakiwa kutokiuka sheria zilizowekwa  na tume  ya utangazji Zanzibar  katika kutumia mitandao hiyo kufanya kazi za kihabari.

Akizungumza na wamiliki wa vyombo hivyo  katika ukumbi wa Wizara ya Habari Gombani Chake Chake katika mkutano  maalum  wa kutoa elimu juu ya matumizi sahihi Ya  Matumizi na uwekeji wa maudhui za kihabari  mitandaoni Katibu Mtendaji Tume Ya utangazaji Zanzibar  Sleiman Abdalla Salum  Alisema  Baadhi Ya Wamiliki wamekuwa wakikiuka sheria  za habari  n kuweka maudhui ambazo hazina maadili. 

  Alisema kufanya hivyo Ni makosa hivyo ni vyema wamiliki hao kitumia vyema mitandao ya kijamii kwa kufuata sheria miko na maadili ya habari ili kuepuka kuingia katika matatizo. 

"  kumekuwa na baadhi ya vyombo vya mitandaoni vinafanya vile vinavyojiskia hakuna maadili katika uwekaji wa maudhui, hawazingatii sheria za uandishi wa habari wanafanya vile tu wanavyojiskia wao. 

" Hii tabia inaweza kupelekea  wamiliki wakaingia mtatizoni ni vyema mkatumia maadili kufuata sheria pia. 

Aidha  Sleiman aliwataka wamiliki ambao si waandishi wa habari kushirikiana na waandishi  wanapofanya kazi zao za habari ili kuepuka kuingia  katika matatizo
"Wapo wale ambao wanamiliki kamera microphone wanamiliki youtube acount wanaamua kuingia  mitaani kuhiji watu bila kujua ABC kuhusu habari wanatuma kwenye mitandao hii  sio sahihi Wenye tabi hiyo  wanatakiwa waiwache mara moja  au washirikiane na wanaojua endapo watahitaji taarifa   mfuate sheria hata kuwafuata wanaojua taaluma hiyo kuwaelekeza. 

 Kwa upande wake ofisa mdhamini wizara y habari Pemba  MFamau Lali Mfamau  Aliwataka wamiliki hao kuweka mipaka katika  uwekaji maudhui kwa kufuata sheria za habari   mitandaoni. 

"Hakuna Uhuru usio na mipaka   Mtumie mitandao kwa sheria zilizowekwa fuateni taratibu za kihabari habari zinataratibu zake msikiuke.

Kwa Upande wake  Mrajis Tume ya utangazaji  Zanzibar Sheikha Haji Dau aliwataka  wamiliki hao kusaijili     vyombo vyao ili kuweza kufanya kazi kwa kutambulikana kwa mujibu wa sheria ili kuepuka usumbufu wa kutokufungiwa  vyombo vyao. 
 
   Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

BAJAJI WAMLILIA RAIS DK MWINYI PEMBA ,WAOMBA MSAADA KWAKWE WASEMA WAMECHOSHWA NA HILI KUTOKA MAWASILIANO

Masheha wanawake wa Wilaya ya Magharib B walivyoleta mabadiliko na maendeleo kwenye shehia zao.

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.