Wajasiriamali kilimo ca mboga mboga Wamemshukuru Rais wa Zanzibar.
Amina Ahmed Moh’d
Mkuu wa wilaya ya Wete Mkoa wa kasakazini pemba amewataka wananchi na wajasiriamali kuzitumia fursa za kujikomboa kiuchumi zilizotolewa Na Rais wa Zanzibar Ikiwemo Mikopo Ya wajasiriamali na kuwekeza katika kilimo.
Aliyasema Hayo Alipokuwa Akizungumza na wananchi wa vijiji vya pujini Mara baada kumaliza ghafla ya kukagua na kushiriki zoezi la uvunaji wa Zao la tungule katika shamba la wajasiriamali wa mboga mboga wa kikundi cha Mshikamano Lililopo Kijili Pujini wilaya ya Chake Chake Mkoa wa kusini Pemba ikiwa ni shamra shamra za kutimiza Miaka miwili Ya uongozi Wa Rais wa Zanzibar Dk Hussein Ali Mwinyi .
Alisema Serikali imeweka mazingira ya kuimarisha uchumi na kuwa endelevu kwa wananchi ambao utawasaidia kujikomboa kiuchumi na kuweza kujiajiri kwa kuwawezesha na kuwapatia Mikopo hivyo ni vyema kuitumia fursa hiyo kwa shughuli mbali mbali ikiwemo kilimo.
Aidha Mkuu wa wilaya Huyo ameitaka wizara ya kilimo umwagiliaji maliasili na mifugo kushirikina na wizara ya Maji ili kusaidia upatikanaji wa maji katika mashamba ya wajasiriamali wa kilimo cha mboga mboga Kijili.
"Wizara ya kilimo Mzidishe jitihada kuwa karibu na wizara ya maji ili yasipopatikana maji ya bomba katika shamba bhasi waweze kuwasaidia mbinu za uongezaji wa visima krqhisisha upatikanaji wa hiduma za maji".
Katika Hatua nyengine Mkuu huyo Aliwataka wananchi wa Pujini kujiepusha na vitendo vya udhalilishaji sambamba na kudai risiti wanaponunua bidhaa mbali mbali ili kusaidia upatikanaji wa kodi katika biashara mbali mbali.
Akizungumza kwa niaba ya ofisa mdhamini wizara ya kilimo umwagiliaji maliasili na mifugo Mkuu wa idara ya kilimo Pemba Asha Omar Faki Alisema juhudi zilizofanywa na rais huyo kwa kutoa mikopo ya fedha za ahuweni ya uviko 19 kwa wajasiriamali wa kilimo cha mboga mboga na matunda zimeleta mafanikio katika shughuli za kilimo kwa wakulima hao.
"Kupitia fedha za covid 19 wajasiriamali hawa wameweza kupata mafanikio ikiwemo kuzalisha maji, pamoja na pembejeo jambo ambalo limekuwa, sote tunaelewa kuwa kilimo bila maji haiwezekani kupitia mkopo huu umewasaidia wao kuchimba kisima, kuweka miundo mbinu ya maji na kuweza kumwagilia kwa matone ambazo ni teknolgia bora za kisasa na pia wameweza kupata pembejeo za kilimo kupitia fedha hizo wameweza kufanikisha.
Aidha Alisema kuwa wizara itendelea kushirikianana wakulima mbali mbali ambao wameamua kujikomboa kupitia shughuli za kilimo.
Awali Akizungumza kwa niaba ya wajasiriamali wa kilimo cha mboga mboga kikundi cha Mshikamano Kijili Pujini Mwakilishi wa kikudi hicho Abassi Hassani Issa wamemshukuru Rais wa Zanzibar kwa kuwapatia fursa za mitaji wananchi wa pujini kupitia kikundi hicho na kuwa wanufaika wa fedha za ahuweni ya uviko mkopo ambao una masharti nafuu ambao tunanufaika nao .
" Kupitia shamra shamra hizi za kutimiza miaka miwili Tunakushukuru Dk Mwinyi sisi wajasiriamali wa mboga mboga pujini kwa kutupatia fursa za mitaji kupitia programu ya Enuka tunaona jitihada zako katika kupunguza tatizo la ajira na utegemezi na kupunguza umaskini kwetu sisi wananchi wako ".
Tunaimani na uongozi wako tunaamini ahadi zako ulizotuahidi katika kipindi cha kampeni kutupatia mikopo ambayo leo hii imeanza kutukomboa n kuttengenezea ajira sisi vijana.
Aidha Mwakilishi wa kikundi hicho Alisema Kupitia kilimo hicho kilichoanzishwa kupitia fedha za mkopo huo tayari kimezalisha ajira zaidi ya 100 ambazo wananchi hunufaika na kujipatia kipato kupitia kilimo hicho.
"Mshikamano Tumezalisha ajira Zisizo rasmi miamoja kupiti kilimo watu wananufaika kwa kilimo hichi kuna wakulima , wanaovuna, wanaopalia shamba, walinzi kupitia ahadi zako za kutengeneza ajira leo hii tumeweza kuzalisha ajira hizo.
Hata Hivyo Mwakilishi huyo ameiomba serikali kupitia wizara ya biashara kuwasadia kutatua changamoto ya soko la uhakika la kuuza bidhaa zao wanazozizalisha ili kufikia zaidi lengo liliowekwa na rais wa Zanzibar kujikwamua kiuchumi.
"Pamoja na yite hayo bado kilio chetu Wajasiriamali wa kilimo cha mboga mboga na matunda hatuna soko la uhakika ambalo litasaidia kuuza biashara zetu baada ya mavuno jambo ambalo linaturudisha nyuma zaidi kuona mazao yanakosa wateja tunaomba serikali itusaidie kupata ufumbuzi wa tatizo hili".
wajasiriamali wa kilimo cha mboga mboga Kijili Pujini ni miongoni mwa walionufaika na mkopo wa shilingi milioni Tano na kuanzisha shughuli ya kilimo cha mboga mboga kujikwamua na umaaskini ambapo Mkutano huo wa kumshukiru rais huyo ni katika kusherehekea kutimia miaka miwili ya uongozi umehudhuriwa naa viongozi mbali mbali kisiwani pemba ikiwa ni pamoja na Mkuu wa wilaya ya Chake Chake, Mkoani, Maofisa wadhamini wizara mbali mbali pemba viongozi wa Chama Cha Mapinduzi Pamoja na Maafisa kutoka wizara ya kilimo.
Mwisho
Comments
Post a Comment