Taasisi Ya kusafirisha mahujaji Arafat Haji na umrat Services Yawatoa hofu.
NA- AMINA AHMED MOH’D
TAASISI YA KIDINI ya Arafat Haji na Umrat Services imewatoa hofu waumini wa dini ya kiislam Nchini wanaotarajia kwenda katika miji mitukufu Makka Na Madina kutekeleza ibada ya hijja Mwaka 2023 sawa na mwaka 1442 Juu suala la uzoefu wa kufanya harakati za kusafirisha mahujaji.
Alitoa Kauli hiyo Mwenyekiti Wa Taasisi Ya Arafat haji na umrat Services Sheikh Khalifa Abdalla Said Mapema leo asubuhi Alipokuwa akizungumza na na kujibu maswali yalioulizwa na baadhi ya waumini wa dini ya kiislam kutoka maeneo mbali mbali ya kisiwa cha pemba waliofika katika kongamano Maalum la uzinduzi wa taasisi hiyo huko Samail Gombani Chake Chake.
Alisema uzoefu na uaminifu walionao viongozi na wasimamizi wa taasisi hiyo katika kusimamia safari za za mahujaji ni wa muda mrefu licha ya kuwa mpya kwa taasisi hiyo .
"Wasimamizi wa taasisi hii tuna uzoefu mkubwa tumesimamia suala hili katika taasisi nyengine takriban sote mnaotuona hapa mbele yenu katika kusimamia na kuongoza jambo hili.
Awali akizindua taasisi hiyo Sheikh Khamis Salum Ali Aliwataka Wasimamizi wa hao kubeba jukumu hilo kwa kutumia hekima na busara ili kufanikisha malengo yaliokusidiwa na mahujaji kwa kutekeleza majukumu ya uongozi kikamikifu.
" Mtekeleze Dhima hii kubwa kusimamia kutekeleza ibada ya hijja kwa waumini bila kujali maslahi ya kidunia .
Kwa upande wake Sheik Khamis Kassim Haji kutoka taasisi hiyo Aliwataka waumini hao waliofika katika kongamano hilo kuweka nia ya kufanya ibada ya hija na kuwa mabalozi kwa wengine juu ya Taasisi hiyo.
"Hija sio fedha bali ni taufik ya Allah hivyo ni vyema kila mmija wetu kuweka nia il kuliafikisha jambo hilo kwa pamoja"
Nae katibu wa Jumuia Ya Arafat haji na umrat Services Sheikh Sleiman Ahmed Moh’d Alieleza kuwa
Lengo la kuanzishwa taasisi hiyo ya kusafirisha mahujaji nchini ni kusaidia Waumini wa dini ya kiislam kutekeleza ibada ya hija bila usumbufu wowote .
Taasisi Ya Arafat haji na umrat Services ni Taasisi ya kidini ambayo imezinduliwa ramsi leo yenye lengo la kusafirisha mahujaji wa Kisiwani Pemba Unguja na Dar essalam , pamoja na kufanya harakati mbali mbali za dini ikiwemo kusaidia mayatima wajane na watu wasijiweza.
Mwisho
Comments
Post a Comment