WIZARA YA AFYA ZANZIBAR IMEWATAKA WANACHI KUTOPUUZA KUSAJILI KADI ZA MATIBABU............ NI MUHIMU

Na Amina Ahmed . 

wizara ya afya Zanzibar   imetoa wiki mbili kwa    wananchi   wote ambao hawasajili kadi i za  afya ya mtibabu zinazotolewa  na wahudumu wa afya jamii katika shehia  zao kuharakisha kusajili    kadi hizo  na kuanza kuzitumia   wanapokwenda katika  kufata matibabu  katika vituo vya afya  pamoja na hospitali . 

 Ametoa Agizo Hilo Waziri wa Afya Zanzibar   Dk Nassor Ahmed Mazrui Alipkiwa akizungumza na masheha Wa mkoa wa kaskazini Pemba Katika Warsha maalum ya utoaji taarifa juu ya umuhimu wa kusajili kafi za matibabu kwa wananchi huko katika ukumbi wa Skuli ya Miti ulaya Wete. 

Amesema Kadi hizo  zinatolewa kwa wananchi kupitia wahudumu wa  afya  jamii wanaopita katika shehia   kusajili vitambulisho vya afya    zina lengo  la  kusaidia  serikali kupanga mpango wa utowaji wa huduma za matibabu na urahisi wa kupata huduma  za afya  zilizo bora kwa wananchi .

Amesema  Serikali hairidhishwi n mfumo wa matibabu uliopo kwa sasa  hivyo mfumo huo wa ktumia  kitambulisho cha matibabu utasaidia wananchi  kuweza kupata mtibabu sahihi  na  kwa wakati

Aidha Waziri Mazrui amefahamisha kuwa  mfumo huo utasaidia   kujua taarifa muhimu  za mwananchi  ikiwa ni pamoja na kujua  taarifa muhimu    za maradhi mbali mbali ya mwananchi. 

Kwa upande wake mkurugezi mkaazi kutoka shirika la Pharm Acess Faundation  Akses Dr .HERI Marwa amesema MFUMO huo utaweza kusadia kuweka kbmbu za wagonjwa na mahali walipotibiwa hivyo ametaka Wanachi kuzitumia kadi hizo Ili kuweza kapata matbabu bila usumbufu .

Nae mkuu wa wilaya ya wete  Dr ,Hamad Omar Bakar  amesema mkoa Kwa kushirikiama na Masheha ili kuendelea kwalimisha wananchi Umuhimu wa kutumia kadi za matibabu na  watahakikisha wananchi wote wanapata kadi hio bila usumbufu.
mwisho. 

Comments

Popular posts from this blog

BAJAJI WAMLILIA RAIS DK MWINYI PEMBA ,WAOMBA MSAADA KWAKWE WASEMA WAMECHOSHWA NA HILI KUTOKA MAWASILIANO

Masheha wanawake wa Wilaya ya Magharib B walivyoleta mabadiliko na maendeleo kwenye shehia zao.

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.