WIZARA AFYA ZANZIBAR TAYARI IMEANZA KUJIPANGA KUDHIBITI UGONJWA EBOLA KUTOINGIA NCHINI

Na AMINA AHMED 

Waziri wa Afya Zanzibar Nassor Ahmed Mazrui  Amewatoa hofu wananchi kuhusu ugonjwa wa ebola  ambao umeanza kusambaa virusi vyake katika nchi za jirani  za Africa ikiemo  Uganda ambapo amesema  kuwa wizara imeanza kuweka  ulinzi katika maeneo  ya mipaka yake katika kudhibiti kuingia ugonjwa huo visiwani Zanzibar. 
 
WAZIRI WA AFYA ZANZIBAR  NASSOR AHMED MAZRUI 
 Akizungumza na Habari hizi  waziri huyo amesema kuwa  tayari wizara inaendelea kujipanga kuhakikisha  ugonjwa   huo hauingii nchini . 

"Tayari Tumeanza kuchukua tahadhari kudhibiti ugonjwa huo endapo utaingia nchini  ikiwa ni pamoja na  kimarisha  ulinzi na kuweka vifaa vya afya ambvyo vitasaidia kupima afya za wanaoingia kutoka nchi nyengine.

Alisema kuwa   licha ya kudhibiti katika maeneo hayo  lakini pia serikali kupitia wizara hiyo imeeendaa vifaa vya kutosha  vya kujikinga  madakatari wa kutoa matibabu wa ugonjwa huo endapo utaingia  nchini   ikiwa ni pamoja na kutenga maeneo maalum ya kuwaweka wagonjwa endapo watabainika. 
 "Hatuombi uingie  nchini kwetu lakini endapo utaingia  Tayari tumeweka vifaa vya kutosha  madakatari watakaosaidia kudhibiti kuenea kwa ugonjwa" 

Mwisho




Comments

Popular posts from this blog

BAJAJI WAMLILIA RAIS DK MWINYI PEMBA ,WAOMBA MSAADA KWAKWE WASEMA WAMECHOSHWA NA HILI KUTOKA MAWASILIANO

Masheha wanawake wa Wilaya ya Magharib B walivyoleta mabadiliko na maendeleo kwenye shehia zao.

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.