WAZIRI MASOUD AFANYA ZIARA UJENZI WA BUSTANI MWANAMASHUNGI CHAKE CHAKE.

NA   AMINA AHMED MOH’D  

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala Za Mikoa Serikali Za Mitaa Na Idara Maalum za SMZ  Massoud Ali Muhammed Amefanya ziara maalum ya kutembelea na kukagua ujenzi wa eneo la  Bustani   Mwanamshungi Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa kusini Pemba.

 Akiwa Katika eneo La ujenzi huo Waziri Massoud Amewataka  Wakanadarasi  kuongeza kasi   ili  wananchi waweze kulitumia jengo hilo kwa wakati    sahihi uliowekwa na serikali.
WAZIRI TAMISEMI ZANZIBAR. MASSOUD ALI MUHAMED. 

   Aidha  Amewataka wasimamizi  kufuatilia  na kutembelea ujenzi huo   ili kiongeza mashirikiano na kutatua changamoto ndogo ndogo zinazojitokeza katika utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Eneo hilo la bustani ya kupumzikia wananchi. 

  Akizungumza mkuu wa wilaya ya chake chake  Abdalla Rashid Ali amesema  wataendelea  kusimamia na kutembelea mara kwa mara kuona ujenzi huo unavyoendelea  ikiwa ni pamoja na kupokea changmoto zitakazojitokeza ili kuziptia ufumbuzi. 

 Ghafla ya kukagua ujenzi huo iliambatana viongozi mbali mbali ikiwa ni pamoja na mkurugenzi wa Baraza la  Chake chake, Ofisa mdhamini wizara ya nchi ofisi ya raisi tawala za mikoa serikali za mitaa na idara maalum za smz Pemba  pamoja na wasimamizi   wa mradi  huo. 
MKUU WA WILAYA YA CHAKE CHAKE ABDALLA RASHID ALI PAMOJA NA AFISA MDHAMINI TAMISEMI PEMBA THABIT OTHMAN ALI. 
Mwisho


Comments

Popular posts from this blog

BAJAJI WAMLILIA RAIS DK MWINYI PEMBA ,WAOMBA MSAADA KWAKWE WASEMA WAMECHOSHWA NA HILI KUTOKA MAWASILIANO

Masheha wanawake wa Wilaya ya Magharib B walivyoleta mabadiliko na maendeleo kwenye shehia zao.

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.