WAZAZI WAASWA MASHIRIKIANO KUTIMIZA NDOTO ZA WATOTO.




NA   AMINA AHMED MOH’D     

Mahafali ya kwanza  Ya wanafunzi wa   wahitimu wa Darasa la awali ( Maandalizi ) Pamoja Madarasa ya Msingi nSuper  kutoka   Skuli ya The Bright  Academy  Yaliojulikana kama  Super Heroes  days amefanyika leo  katika ukumbi wa Makonyo Wawi Chake Chake  Mkoa wa kusini Pemba . 

Akizungumza katika maghafali hayo  Ofisa mdhamini   Ofisi ya Rais Ikulu Pemba Shuweha Abdalla Omar  amesema kuwa serikali itaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na  Taasisi binafsi za kukuza elimu nchini kwa kutatua changamoto mbali mbali zinazokabili taasisi hizo ambazo hupelekea kurudiaha nyuma  harakati zao. 
     SHUWEHA ABDALLA OMAR 
 OFISA MDHAMINI OFISI YA RAIS IKULU    PEMBA 
 Amesema   mchango unaofanywa na taasisi za elimu ikiwemo kituo hicho cha the bright academy ni mkubwa   katika  sekta ya elimu  hivyo serikali haitosita kuwaunga Mkono  katika kuleta mendeleo na mageuzi ya elimu.
 
Amesema kuwa serikali ya awamu ya nane inaendelea kuchukua jitihada mbali mbali  kuboresha mendeleo ya elimu  ikiwa ni pamoja na kujenga skuli za kisasa  zitakazosaidia kuboresha elimu kwa wanafunzi sambamba na kuruhisiwa wanafunzi kutumia skul hub kujiendeleza. 

 Bi Shuweha Aliwapongeza waalimu wa skuli hiyo kwa jitihada zao katika kusimamia vyema wanafunzi  ambapo pia amewataka wazazi   kujitahidi kulipa ada kwa wakati sambamba kuwahimiza watoto kusoma   kwa bidii pamoja na kufika kwa wakati. 

Aidha Mdhamini huyo amewapongeza wahitimu   hao kwa jitihada zao   walizozionesha katika masomo  ambapo amewaasa  kuendeleza bidii katika kujifunza  mambo mbali mbali wanayofundishwa.

Akizungumza na wanafunzi wazazi pamoja na wahitimu wa mahafali hayo  Mweyekiti wa baraza la vijana  taifa  Rushda Khamis Kassim  amewaasa  wazazi na wanajamii  kusimamia  ndoto za watoto  walizonazo na kuwalinda dhidi ya vitendo vya udhalilishaji  ambao unaendelea kuathiri watoto na  kupelekea kukatisha malengo yao.

 RUSHDA  KHAMIS KASSIM. 
 M/KITI BARAZA LA VIJANA ZANZIBAR. 
 Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa Skuli hiyo Abdul karim Yunus Yahya ambae pia ni mwenyekiti wa vituo vya elimu   za kujtegemea Zanzibar  amesema kuwa licha ya kupiga hatua kwa kituo hicho ikiwa ni pmoja na kupata usajili rasmi sambamba na  kuwa kituo bora kinachoongoza kwa kutoa elimu  bora lakini  pia kinakabiliwa na ukosefu wa jengo  jambo ambalo linarudisha nyuma  kutokana na kulipia kodi ya jengo kila mwezi kuendeleza shughuli hizo. 

 Aidha Mkuu huyo amewaomba wadau na wahisani wa maendeleo ya elimu kusaidia ujenzi wa kituo cha  the bright  ambao tayari kwa hatua za awali   umeanza ili kuondokana na changamoto ya  kukosa eneo lao wenyewe. 
ABDUL- KARIIM  YUNUS YAHYA. 
 MWALIMU MKUU KITUO CHA THE BRIGHT ACADEMY
 Sherehe ya Mahafali hayo  imeambatana na burudani mbali mbali kutoka kwa wanafunzi wa kituo hicho   ikiwa ni pamoja na burudani ya musiki, kaswida, Mashindano ya kula,  masuali ya papo kwa papo kwa lugha ya kiengereza,  kuongea lugha ya kiengereza kwa ufasaha kwa watoto , utenzi, elimu y vitendo ambapo ktika mahafali hayo ya super heroes  kids  day   uliimba wimbo wa taifa  ikiwa ni katika kumuenzi baba wa taifa hayat Julius Nyerere katika kukumbuka na kuthamini mchango aliouacha kwa taifa  la Tanzania. 
WANAFUNZI   THE BRIGHT  KIDS 
MATUKIO YA WANAFUNZI KATIKA MAHAFALI YA THE BRIGHT ACADEMY SUPER HEROES KIDS.



PICHA BAADHI YA WANAFUNZI 



PICHA MWAAFUNZI


Mwisho. 







 
 

Comments

Popular posts from this blog

BAJAJI WAMLILIA RAIS DK MWINYI PEMBA ,WAOMBA MSAADA KWAKWE WASEMA WAMECHOSHWA NA HILI KUTOKA MAWASILIANO

Masheha wanawake wa Wilaya ya Magharib B walivyoleta mabadiliko na maendeleo kwenye shehia zao.

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.