WaWAZAZI SIMAMIENI MAADILI KUPUNGUZA UDHALILISHAJI KWA WATOTO MIAKA 15 NA KUENDELEA.

wazazi na walezi  Nchini wameaswa kusimamia maadili  na kuwalinda  watoto  dhidi y vitendo vya udhalilishaji  vinavyojitokeza kutokana na sababu mbali mbali katika jamii zao . 

Ameyasema  hayo Kamishna wa polisi Zanzibar Hamad Khamis Hamad  alipokuwa akizungumza na wananchi huko katika uwanja wa Mpira Kendwa  wilaya ya mkoani mkoa wa kusini Pemba katika mkutano maalum wa kushajihisha ulinzi sirikishi katika  shehia  za  kendwa na kiwani. 
KAMISHNA POLISI ZANZIBAR   HAMAD KHAMIS HAMAD

Amesema  moja ya sababu zinzazopelekea  watoto  kufanyiwa vitendo vya udhalilishaji ni  pamoja na kukosa maadili    na malezi bora hususan kwa watoto ambao tayari wamefikia umri wa miaka 15 na kuendelea jambo ambalo hupelekea kujiingiza   katika tabia hatarishi. 

 "Wazazi mnajukumu kubwa la kusimamia   maadili ya watoto wenu wakike na wakiume   haswa wale ambao umri wao  ni hatarishi   wanajiingiza katika tabia mbaya  kutokana na kutokuwafuatilia nyenendo zao  ". 

Aliwataka wazazi  hao pia  kuendelea kufuatilia nyendo za watoto  wao  na kuwachukulia hatua  stahiki ikiwa ni pamoja na kuwakanya  endapo watabaini kujihusisha na tabia mbaya. 

" Tusione wamekuwa watoto  na kuwaachia mamlaka ya kujiongoza wenyewe watafanya wanavyotaka bila kujali kuwa wanapotea  kila mzazi wajibu wake ni kumchunga mtoto wake dhidi ya vitendo viovu wanavyofanya wao  kwa wao lakini pia wanavyifanyiwa na watu ambao hawana  aibu kufanya   udhalilishaji kwa watoto". 

Aidha Amewataka wananchi haobkusimmka  suala la  mporomoko wa maadili   pamoja kuwashirikisha viongozi wa dini katika kulifanikisha suala hilo. 

"Viongozi wa dini maimu katik misikiti yetu licha ya kulikumbusha suala hili lkini pia tunayo nafasi kubwa  kuanzisha kamati maalum za kusimamia maadili  katika kusaidia  vizazi vyetu visivunje maadili". 

 Katika hatua nyengine Kamishna Hamad amewataka wananchi wa kendwa na kiwani kutoa mashirikino kwa ulinzi shirikishi katika kudhibiti vitendo vya kihalifu ikiwemo wizi wa mazao na mifugo katika shehia zao. 

 "Endapo wananchi tutatoa mashirikiano kwa wenzetu hawa walioamua kusaidia kuimarisha ulinzi katika shehia na vijiji vyetu  wizi wa mazao pamoja na mifugo  hata wizi ule wa kudokoa  majumbani hautokuwepo". 
Lakini tukiona ni jambo la kawaida  kesho kakamatwa mtoto wa fulani  Kachukuliwa hatua mzazi wake kaja juu hatutofika popote na uhalifu utaendelea". Aliendelea Kamishna.

 Akizungumza kwa niaba ya wananchi
 Mkutano huo wa kuhamasisha  mashirikiano   kwa wanajamii katika ulinzi shirikishi Yalikutanisha wananchi wa vijiji mbali mbali vilivyomo katika shehia za kendwa na kiwani.
 
kwa upande wa wananchi wamemshukuru Kamishna  ambapo wamesema kuwa   kunzishwa kwa vikundi hivyo kutasaidia kupunguza  vitendo vya kihalifu  katika vijiji vyao. 


Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

BAJAJI WAMLILIA RAIS DK MWINYI PEMBA ,WAOMBA MSAADA KWAKWE WASEMA WAMECHOSHWA NA HILI KUTOKA MAWASILIANO

Masheha wanawake wa Wilaya ya Magharib B walivyoleta mabadiliko na maendeleo kwenye shehia zao.

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.