WATUMISHI WA UMMA PEMBA WAPEWA USHAURI KUBORESHA UTENDAJI KAZI.
Na Amina Ahmed
Waziri wa Nchi ofisi ya raisi tawala za mikoa serikali za mitaa na idara maalum za smz Massoud Ali Muhammed Ameagiza Maafisa Watumishi wa taasisi mbali mbali zilizo chini ya wizara hiyo kisiwan pemba kufanya uhakiki na kujua ongezeko la watumishi ambao majukumu yao yanaendana sawa katika taasisi zao na kuwahamishia taasisi ambazo zina upungufu wa watumishi hao si zaidi wiki moja kutoka sasa.
Ametoa agizo hilo Huko katika ukumbi za wizara hiyo Wawi Chake Chake Pemba alipokuwa akizungumza na wakuu wa taasisi mpoja na maofisa watumishi katika kikao kazi cha wizara hiyo mapema Leo Asubuhi.
Massoud Ali Muhammed
Waziri Tamisemi Zanzibar.
Amesema kumekuwa na mrundikano wa watumishi ambao wana majukumu sawa katika baadhi ya taasisi zilizopo chini ya wizara hiyo huku baadhi ya taasisi nyengine zikikosa Watumishi kutokana na kukosa watendaji wenye sifa kutokana na waliowengi kukaa sehemu moja na kurudisha nyuma shughuli zautendaji kazi.
"Natoa wiki moja kwa maafisa utumishi mtathmini wengi na kulifanyia kazi suala hili sio kazi ya mtu mmoja wanafanya watu wanne watano ndio wanafanya nataka lishughulikiwe mara moja waondolewe wengine wapelekwe ambako hakuna wakafanye kazi wasikae tu huko wakaishia kutowajibika Alisema Waziri Massoud kila sehemu nataka nikute wafanya kazi wanawaibika sio nifike baadhi ya maeneo watumishi hakuna. "
Aidha waziri huyo ameagiza wakuu wa taasisi na watendaji hao Kuandaa mafunzo maalum kwa wafanya kazi wa wizara hiyo kila baada ya muda ili kuwasaidia kuzidisha ufanisi na kutambua majukumu miiko na maadili ya ya kazi zao.
" Ni jambo La kusikitisha Mtumishi wa wizara kutojuwa wajibu wake kutojua vipi anatakiwa avae, kutokujua haki zake kama mtumishi ni zipi naagiza kuliangalia suala hili kwa kuandaa mafunzo kila baada ya muda kwa watumishi tunataka watumishi bora sio bora watumishi".
Aidha amewataka watendaji na maofisa hao kutosita kuchukua hatua za kinidhamu kwa watumishi ambao wanakwenda kinyume na sheria za kazi kwa kukiuka sheria pamoja na kutoa taarifa endapo watakuwa nahofu ya kuwawajibisha.
" Mkiona mtendaji awe baraza la mji halmashauri wete mkoni chake na kwengineko anakiuka maadili mnamuwajibisha hawajibiki msisite kushirikisha viongozi wa juu kma ni naibu katibu hata mimi ambae nina dhaman nitamuwajibisha kwa makosa yakekama ni uhamisho kumsimamisha au hata kumfukuza lakini muwawajibishe endapo watakuwa wanatenda mambo ya ovyo alisema. ".
Aidha Massoud amewaasa maafisa utumishi kutoa mashirikiano mazuri kwa wafanya kazi na kuacha kutumia lugha chafu zisizo stahiki .
" Nataka muwe na ukaribu katika kesi ndogo ndogo muwe mnazitatua ni jambo la aibu mfanya kazi kukosa mashirikiano kunitafuta mimi kunilalamikia hata kesi ndogo tu mfani ya stahiki yake ya likizo na mambo mengine wakati watendaji dhamana wapo huku, nataka iwe mfano bora katika mashirikiano sio maafisa mjione nyniy ndio bora kuliko wengine waliooo chini yenu kila mmoja ajuwe ni mtumishi wa umma ".
Alindelea kusema kuwa endapo ofisi haitokuwa na mashirikiano uwajibikaji na utendaji kazi hautoimarika kwani kila mtu hatokuwa na nifhamu ya utendaji kazi.
Akizungumza katika kikao hicho Ofisa mdhamini wizara ya nchi ofisi ya raisi tawala za mikoa serikali za mitaa na idara maalum za smz Thabit Othman Ali amemshukuru Waziri huyo kwa kuwakumbusha zaidi wajibu na utendaji kazi wao ambpoa amesema kuwa wizara hiyo kisiwani pemba itazidisha mashirikiano katika kusimamia utendaji kazi kwa watumishi wake sambamba na kuyafanyia kazi maagizo aliyoyatoa .
Kishoto Ofisa Mdhamini wizara ya nchi ofisi ya raisi tawala za mikoa serikali za mitaa na idara maalum za smz
Thabit Othman Ali.
Mwisho
Comments
Post a Comment