WANAOKUSANYA KODI WAMEOMBWA KUZIDISHA KASI
- Get link
- X
- Other Apps
Na Maryam Hamad
Naibu Waziri Ofisi ya rais Fedha na Mipango Zanzibar Ali Sleiman Ameir amewataka watendaji na wasimamizi wa ukusanyaji kodi Pemba kuongeza kasi katika sula hilo sambamba na kulifanya kuwa endelevu katika kufikia malengo ya upatikanaji wa mapato katika vianzio mbali mbali .
ALI SLEIMAN AMEIR
Naibu Waziri Ofisi Ya Rais Fedha Na Mipango Zanzibar
Ameyasema hayo Alipokuwa akizungumza na na watendaji wa wizara na tasisi za serikali ,makatibu tawala wilaya na mkoa ,watendaji wa mabaraza ya miji na halmashauri , Tra,ZRB ,wakala wa serikali mtandao pamoja na wakuu wa taasisi zinazojitegemea kisiwani humo katika kikao kazi kinachohusu mikakati ya kufikia makusanyo kwa mwaka 2022,23 huko katika ukumbi wa wizara hiyo Gombani chake chake.
Amesema endapo watendaji hao watashirikiana pamoja katika suala hilo mpango wa makusanyo na mapato utakuwa endelevu na wenye kuleta maendeleo kwa wananchi na serikali .
Awali akizungumza na watendaji pamoja na wasimamizi hao naibu katibu mkuu ofisi ya rais fedha na mipango Zanzibar Aboud Hassan Mwinyi amesema kila mmoja ana wajibu wa kushajihisha suala la ulipaji kodi pamoja kudai risiti kwa wafanya biashara.
Kwa upande wake ofisa mdhamini ofisi ya rais fedha na mipango Abdul wahab said abuubakar amesema wizara hiyo itaendelea kushirikiana na watendaji na taasisi zinazohusika na ukusanyaji wa mapato kisiwani pemba ili kufikia malengo yaliowekwa na serikali katika kupata makusanyo yaliokusudiwa kufikiwa kwa mwaka.
Kikao kazi hicho kiliwashirikisha watendaji waofisi ya rais fedha na mipango pemba, wasimamiz pamoja na taasisi zinazohusika na ukusanyaji wa kodi , makusanyo na mapato katika maeneo mbali mbali kusini na kaskazini pemba.
mwisho
- Get link
- X
- Other Apps
Comments
Post a Comment