WANANCHI TOENI MASHIRIKIANO KUDHIBITI VITENDO VYA UHALIFU.

Na Amina Ahmed

Kamishna Wa Polisi Zanzibar Hamad Khamis Hamad  amesema Jeshi la Polisi litaendelea  Kutoa Mashirikiano  Katika  kutatua changamoto za kihalifu zinazojitokeza katika shehia  Mbali Mbali  kwa kushirikiana na ulinzi shirikishi katika shehia hizo ili kudhibiti na kumaliza vitendo hivyo. 
KAMISHNA WA POLISI ZANZIBAR   
HAMAD KHAMIS HAMAD 
 Ameyasema Hayo Alipokuwa Akizungumza  na Masheha wa shehia za  Mkoa wa kusini Pemba,  Viongozi wa dini Askari wakaguzi  pamoja na maafisa   Ustawi wa jamii   katika ukumbi wa Polisi Madungu Chake Chake   katika  mkutano maalum wa kujitambulisha   pamoja na kusikiliza  changamoto kwa  shehia ikiwa ni siku chache  baada ya kuteuliwa kushika nafasi hiyo Visiwani Zanzibar 

 Amesema  kuimarisha ulinzi na usalama ndio nyenzo pekee itakayosaidia wananchi kuweza kufanya shughuli zao za kuleta  maendeleo   wakiwa katika hali ya utulivu. 

"Mwalimu ataweza kusomesha  Daktari ataweza kutibu mfanya biashara atakuwa huru kufanya biashara  na kila kitu katika nchi kitakwenda  vyema endapo tutakuwa na mashirikiano katika kudhibiti vitendo hivi jeshi la polisi linahitaji mashirikiano  yenu  kulifanikisha hili Tutamia mbinu zetu kama watendaji wa jeshi kulifanikisha hilo".

Alisema kuwa masheha viongozi wa dini na maafisa ustawi pamoja na wananchi  wanafahamu 
Zaidi Changamoto zipi zinapelekea uhalifu katika maeneo yao hivyo ni vuema kushirikisha jeshi la polisi  katika kuzipatia ufumbuzi changamoto hizo. 

"  Msiogope kuwashirikisha askari polisi katika  kudhibiti uhalifu katika Shehia Zenu   toeni taarifa kwa maafisa wakaguzi  askari wa wilaya  mkoa hata ikiwezekana kwangu mimi  matukio au viashiria vyivyote vya uhalifu tutaafanyia kazi". 

Aidha   Kamishna Hamad Amewataka masheha kuwatambua  wageni wanaoingia katika shehia zao  n kutoa taarifa  endapo watakuwa na hofu juu ya  mgeni yeyote ili kudhibiti  vitendo vya uhalifu  kutokana na muingiliano huo   wa watu   wenye tabia mbali mbali. 

"Asilimia  Kubwa Wananchi katika vijiji wanajuana tabia zao  masheha utaratubu wa  wa kuwatambua  wageni   wanaoingia na kutoka katika shehia musiupuuze ni moja kati ya sababu zinazopelekea  kujitokeza matendo hayo  maovu".

Wakizungumza Baadhi  ya washiriki  wa mkutano huo kwa upande wa masheha, Sheha wa shehia  Madungu  Mafunda Hamad Rubea   Pamoja   Ali khamis Massoud Sheha wa shehi ya mvumoni   wamemuomba Kamishna huyo Kushirikisha  Vikosi vyengine vya Polisi  vilivyopo Zanzibar Katika kuendeleza maoambano ya kudhibiti uhalifu   . 

"Kuna kipindi tuliona  vikosi vyite vinafanya kazi kwa pamoja  sasa ule wingi wao  wahakifu unawatia hofu wanapunguza  matabia yao lakini lei shehi nzima askri mmoja ikifika jioni anarudi kwakwe hawatogopa tunomba mrudishe yale mambo  alisema  Ali khamis". 


 Kwa upande wao viongozi wa dini Akiwemo Robert Migue    kiongozi wa dini katika kamati ya dini wilya ya chake chake Pamoja na  Hamad Shaame Hamad   wameliomba jeshi hilo kuwapatia mafunzo    ya vitendo  askari  jamii walioamua kujitolea kusaidia ulinzi katika shehia na vijiji vyao. 

" Tunapata madhila  sana sisi ambao tumejitolea kudhibiti wahalifu lakini inafikia hatua moka mtu anapomkamata muhalifu anatafunwa anabaki na kovu atakwenda nazo kaburini hii ni kutokana na kukosa uelewa na mbinu za kupambana nao tunaomba uliangaie hilo moite katika shehia vikundi vya ulinzi shirikishi muvipatie mafunzo"Alisema sheh shaame. 

Katika mkutano huo mambo Mbali Mbali  Yalishauriwa katika kuimarisha ulinzi na kupunguza vitendo vya uhalifu Kusini Pemba ambapo awali Kamishna huyo  alizungumza na masheha mkoa wa kaskazini Pemba huku akitarajiwa kuzungumza na viongozi wa siasa   Mkoa huo Mapema Kesho. 

Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

BAJAJI WAMLILIA RAIS DK MWINYI PEMBA ,WAOMBA MSAADA KWAKWE WASEMA WAMECHOSHWA NA HILI KUTOKA MAWASILIANO

Masheha wanawake wa Wilaya ya Magharib B walivyoleta mabadiliko na maendeleo kwenye shehia zao.

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.