Masheha wanawake wa Wilaya ya Magharib B walivyoleta mabadiliko na maendeleo kwenye shehia zao.
SALMA KHMIS - UNGUJA KATIKA Uongozi wa taifa hili viongozi ambao wako karibu na wananchi na wanapaswa kuhakikisha maendeleo yanafikiwa na yanafanyika ni Masheha. Masheha wa Wilaya ya Magharib B wamejipanga kuhakikisha maendeleo na mabadiliko yanapatikana ndani ya shehia zao. Wilaya ya Magharibi B ni miongoni mwa Wilaya tatu zilizomo katika mkoa wa mjini magharib Unguja ambapo Mkoa huo una jumla ya masheha 121 kati ya hao 19 ni wanawake na 101 ni wanaume. Wilaya ya Magharibi B ni Wilaya iliyotoa shehia 34 kati ya hizo shehia 6 zinaongozwa na masheha wanawake na shehia 28 zinaongwa na masheha wanaume. Shehia ya kijitoupele na michungwani ni Shehia maarufu zilizomo katika Wilaya ya Magharib B ambazo zinaongozwa na Masheha wanawake. Shehia hizo kwa kiasi kikubwa zimepiga hatua za kimaendeleo ikiwemo kueka mazingira safi na kupambana na vitendo vya uchimbaji wa ...
Comments
Post a Comment