SALMA KHMIS - UNGUJA KATIKA Uongozi wa taifa hili viongozi ambao wako karibu na wananchi na wanapaswa kuhakikisha maendeleo yanafikiwa na yanafanyika ni Masheha. Masheha wa Wilaya ya Magharib B wamejipanga kuhakikisha maendeleo na mabadiliko yanapatikana ndani ya shehia zao. Wilaya ya Magharibi B ni miongoni mwa Wilaya tatu zilizomo katika mkoa wa mjini magharib Unguja ambapo Mkoa huo una jumla ya masheha 121 kati ya hao 19 ni wanawake na 101 ni wanaume. Wilaya ya Magharibi B ni Wilaya iliyotoa shehia 34 kati ya hizo shehia 6 zinaongozwa na masheha wanawake na shehia 28 zinaongwa na masheha wanaume. Shehia ya kijitoupele na michungwani ni Shehia maarufu zilizomo katika Wilaya ya Magharib B ambazo zinaongozwa na Masheha wanawake. Shehia hizo kwa kiasi kikubwa zimepiga hatua za kimaendeleo ikiwemo kueka mazingira safi na kupambana na vitendo vya uchimbaji wa ...
NA AMINA AHMED MOH’D - PEMBA CHAKE Chake ni moja kati ya wilaya mbilizi zinazopatikana katika Mkoa wa Kusini Pemba Zanzibar Tanzania. Ambayo kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2012 ina idadi ya wakaazi 97,249 na anuani za makazi zikiwa ni 74200 Idadi Mpya ya wakaazi wa Chake Chake kwa takwimu za Sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 iliyotolewa hivi karibuni bado hazijapokelewa katika ngazi za wilaya ni kutokana na takwimu hizo kuikiishia katika ngazi za Mikoa pekee jambo ambalo limewia ugumu kupatikana idadi mpya ya wakazi wake wa sasa. Chake Chake ina jumla ya shehia 32 ambazo wakaazi wake hulazimika kutumia kituo kimoja pekee cha polisi katika kuripoti matukio mbali mbali. Matukio hayo ni pamoja uhalifu, udhalilishaji wa kijinsia wazee wanawake na watoto, wizi wa mazao , mifu...
NA ASIA MWALIM MARA nyingi tumeshuhudia uzinduzi wa mipango mikakati kwenye masuala mbali mbali ikizinduliwa, lakini ukifatilia kwa karibu utabaini utekelezaji wake haufikii lengo husika. Kwa kuwa utekelezaji wake hauzingatiwi, huo huwa wakati kwa baadhi ya watu kutokujali kutekeleza yalioelezwa kutokana kutochukuliwa hatua yoyote. “Huwezi kumwambia mgeni apite wakati mlango wa nyumba yako umeufunga” huu ni wakati sasa serikali, wadau mbali mbali wa michezo na jamii kushirikiana katika utekelezaji wa mpango mkatati jumuishi wa michezo ili kufikia dhana ya kuanzishwa kwake na kila mmoja kunufaika na fursa za michezo. Kwa muda mrefu kundi kubwa la wanawake na wasichana walishindwa kushiriki michezo ipasavyo kutokana na changamoto kadhaa ambazo hazina usalama kwao kushiriki michezo. Hali hiyo ni miongoni mwa vikwazo vinavyowakabili baadhi ya wanawake wanaojitokeza kushiriki michezo, hatimae kuvunja ndoto zao ya kuibua vipaji kwa kut...
Comments
Post a Comment