NA AMINA AHMED PEMBA. WANANCHI katika Manispaa ya Mji wa chake chake na Vitongoji vyake walilazimika kuchelewa kakika harakati zao za kujitaftia riziki baada ya usafiri uliozoeleka kwa siku za hivi karibuni wa Bajajj kutoonekana au kuonekana chache kwenye viunga tofauti mapema leo Machi, 6, 2025. Baada ya hali hiyo kushika kasi huku wananchi wakipigwa na butwaa, mnamo Majira ya saa 3 Asubuhi Gari za Daladala ikiwemo za Ole Kianga kuanza kuchukua Abiria hao na kuanza kuwasafirisha. Hata hivyo wakizumzia kutoonekana katika vijiwe vyao kubeba abiria baadhi ya waendesha Balaji walisema kuwa walilazimika kushiriki katika kikao cha dharura kwa ajili ya kujadili unyanyasaji wanaopata katika mamlaka za serikali ikiwemo Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi kupitia mamlaka ya usafirishaji. Wamesema Mawasiliano na Baraza MawasilianoJuu kile walichodai kuwa Wamechoshwa na Udhalilishaji wanaofanyiwa na Mamlaka hizo mb...
SALMA KHMIS - UNGUJA KATIKA Uongozi wa taifa hili viongozi ambao wako karibu na wananchi na wanapaswa kuhakikisha maendeleo yanafikiwa na yanafanyika ni Masheha. Masheha wa Wilaya ya Magharib B wamejipanga kuhakikisha maendeleo na mabadiliko yanapatikana ndani ya shehia zao. Wilaya ya Magharibi B ni miongoni mwa Wilaya tatu zilizomo katika mkoa wa mjini magharib Unguja ambapo Mkoa huo una jumla ya masheha 121 kati ya hao 19 ni wanawake na 101 ni wanaume. Wilaya ya Magharibi B ni Wilaya iliyotoa shehia 34 kati ya hizo shehia 6 zinaongozwa na masheha wanawake na shehia 28 zinaongwa na masheha wanaume. Shehia ya kijitoupele na michungwani ni Shehia maarufu zilizomo katika Wilaya ya Magharib B ambazo zinaongozwa na Masheha wanawake. Shehia hizo kwa kiasi kikubwa zimepiga hatua za kimaendeleo ikiwemo kueka mazingira safi na kupambana na vitendo vya uchimbaji wa ...
NA ASIA MWALIM MARA nyingi tumeshuhudia uzinduzi wa mipango mikakati kwenye masuala mbali mbali ikizinduliwa, lakini ukifatilia kwa karibu utabaini utekelezaji wake haufikii lengo husika. Kwa kuwa utekelezaji wake hauzingatiwi, huo huwa wakati kwa baadhi ya watu kutokujali kutekeleza yalioelezwa kutokana kutochukuliwa hatua yoyote. “Huwezi kumwambia mgeni apite wakati mlango wa nyumba yako umeufunga” huu ni wakati sasa serikali, wadau mbali mbali wa michezo na jamii kushirikiana katika utekelezaji wa mpango mkatati jumuishi wa michezo ili kufikia dhana ya kuanzishwa kwake na kila mmoja kunufaika na fursa za michezo. Kwa muda mrefu kundi kubwa la wanawake na wasichana walishindwa kushiriki michezo ipasavyo kutokana na changamoto kadhaa ambazo hazina usalama kwao kushiriki michezo. Hali hiyo ni miongoni mwa vikwazo vinavyowakabili baadhi ya wanawake wanaojitokeza kushiriki michezo, hatimae kuvunja ndoto zao ya kuibua vipaji kwa kut...
Comments
Post a Comment