Katika miaka ya mwanzo ya maisha ya mtoto ndipo msingi mkubwa wa ukuaji wake hujengwa. Mtoto mdogo anahitaji mazingira yatakayomsaidia kukuza akili, afya, hisia na uwezo wa kuwasiliana na watu wanaomzunguka. Vituo vya TUTU vimekuwa sehemu muhimu katika kuhakikisha watoto wa umri wa awali wanapata malezi na elimu inayowaandaa kwa maisha yao ya baadaye. Najua bado unajiuliza Tutu ni nini lakini kamwe katika masikio lako sio neon geni TUTU ni kifupi kinachotumika kumaanisha Taaluma ya Uangalizi na Ujifunzaji wa Watoto Wadogo. Vituo vya TUTU ni sehemu maalumu zinazotoa malezi, uangalizi na elimu ya awali kwa watoto wadogo kabla ya kuanza elimu rasmi ya msingi. Vituo hivi vinalenga kumsaidia mtoto kukua vizuri katika maeneo mbalimbali ikiwemo ukuaji wa akili, lugha, afya, hisia, tabia na mahusiano na watoto wengine. Katika vituo vya TUTU watoto hujifunza kupitia michezo, nyimbo, hadithi, mazoezi ya ubunifu na shughuli zinazolingana na umri wao. Lengo kubwa la TUTU ni kuhakikisha ...
NA AMINA AHMED MOH’D - PEMBA CHAKE Chake ni moja kati ya wilaya mbilizi zinazopatikana katika Mkoa wa Kusini Pemba Zanzibar Tanzania. Ambayo kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2012 ina idadi ya wakaazi 97,249 na anuani za makazi zikiwa ni 74200 Idadi Mpya ya wakaazi wa Chake Chake kwa takwimu za Sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 iliyotolewa hivi karibuni bado hazijapokelewa katika ngazi za wilaya ni kutokana na takwimu hizo kuikiishia katika ngazi za Mikoa pekee jambo ambalo limewia ugumu kupatikana idadi mpya ya wakazi wake wa sasa. Chake Chake ina jumla ya shehia 32 ambazo wakaazi wake hulazimika kutumia kituo kimoja pekee cha polisi katika kuripoti matukio mbali mbali. Matukio hayo ni pamoja uhalifu, udhalilishaji wa kijinsia wazee wanawake na watoto, wizi wa mazao , mifu...
MTANDAO wa Asasi za kiraia wa Pemba (PACSO) umeandaa mkutano maalumu kwa wananchi wa Kisiwa kidogo cha Kojani wenye lengo la kuiwezesha jamii kupata uwelewa mpana juu ya masuala ya kisheria na haki za binaadamu. Mkutano huo uliowashirikisha wananchi wa Kisiwa cha Kojani umeandaliwa na jumuiya PACSO kwa ufadhili wa shirika la UNDP na kufanyika huko ukumbi wa skuli ya msingi Kisiwani humo. Akizungumza na wananchi Mkurugenzi Mkuu wa PACSO Pemba Mohamed Najim Omar katika mkutano huo alisema, mpango huo una lengo la kuiwezesha jamii kupata ufahamu wa kisheria na haki za binaadamu. "Jamii zetu bado zina changamoto nyingi na baada ya kuliona hili tumeamua kuandaa mpango wa kupita kwenye jamii kutoa taaluma ya kuwawezesha watu ufahamu juu mambo haya, elimu zinatolewa nyingi lakini na sisi pia tumeona kuja haja ya kuwafikia", alisema. Aidha alisema, kutokana na kujitokeza masuala mbali mbali ya unyanyasaji wa kijinsia, watoto kudhalilishwa, wanawake, watu wenye ulemavu na hata wazee ...
Comments
Post a Comment