MKURUGENZI WA MASHTAKA ZANZIBAR AFANYA ZIARA KISIWANI PEMBA.

Na   AMINA AHMED MOH’D. 

Mkurugenzi wa mashtaka Zanzibar  Mgeni Jeilani Jecha Amewataka  watendaji wa Ofisi hiyo kisiwani pemba kufanya kazi na   Kusimamia  majukumu yao kwa  kutenda haki  na kufuata   sheria ikiwa ni pamoja na kutojihusisha Katika vitendo vya rushwa .

 Ametoa ombi hilo  Alipokuwa akizungumza na wafanya kazi wa Ofisi hiyo Madungu Chake Chake  pemba katika Ghafla  maalum  ya  kuzungumza na kujitambulisha kwa   ikiwa ni siku chache mara baada ya kuapishwa kuongoza nafasi hiyo. 
 Amesema   Ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka ndio iliyobeba dhamana  ya nchi katika kuchunga  kusimamia na kutoa haki  bila upendeleo   hivyo ni vyema kuiendeleza sifa hiyo kwa kutokujihusisha na vitendo    visivyofuata maadili ambavyo vitapelekea  kuondoa uaminifu   huo kwa   wananchi.
 Akizungumza katika ghafla hiyo Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar   Mwanamkaa  Abdul Rahman Muhammed  amewataka watendaji na wafanya kazi wa ofisi hiyo kuendelea kutoa mashirikiano kwa kiongozi huyo ili kuongeza ufanisi katika kusimamia na kuongoza vyema majukumu aliyopewa na serikali.

Awali wakitoa neno la shukurani   kwa niaba ya wafanya kazi wa ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka pemba Mwanasheria dhamana   kisiwani humo Ali Haidar  Muhammed   pamoja na  wakili wa serikali kutoka ofisi hiyo wamesema  wataendelea kutekeleza na kusimamia majukumu ya uendeshaji  kupitia, kutoa ushauri   kupokea malalamiko   kwa vyombo husika, sambamba  na kuendeleza mashirikiano kwa kufany kazi kwa bidii.
 Ziara ya mkurugenzi huyo kisiwani pemba  imekuja   ikiwa ni siku chache  Rais wa zanzibar  kumteuwa  ndugu Mgeni jeilan jecha kuwa mkurugenzi  mkuu ofisi ya Mkurugenzi mashtaka zanzibar sambamba na kumuapisha mnamo  tano mwezi huu.
Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

BAJAJI WAMLILIA RAIS DK MWINYI PEMBA ,WAOMBA MSAADA KWAKWE WASEMA WAMECHOSHWA NA HILI KUTOKA MAWASILIANO

Masheha wanawake wa Wilaya ya Magharib B walivyoleta mabadiliko na maendeleo kwenye shehia zao.

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.