JITIHADA ZAIDI ZINAHITAJIKA KUDHIBITI ONGEZEKO LA WAGONJWA WA KIFUA KIKUU ZANZIBAR
Na AMINA AHMED MOH’D.
Kifua Kikuu sio Jina la ugonjwa Mgeni ndani ya masikio ya waliowengi ambapo wapo wanaochukulia kuwa ni ugonjwa wa kawaida lakini pia wapo wasiojua kabisa ni ugonjwa gani, unasababishwa na nini lakini pia tiba yake pamoja na athari zake ni zipi.
Kwa faida ya wasomaji wa gazeti hili Kifua Kikuu ni Aina ya ugonjwa wa kuambukiza unasababishwa na bacteria Aina ya turbeclosis kwa kifupi (TB) ulio ambapo Ugonjwa huu husababishwa na aina mbalimbali za bakteria ambazo hujulikana kama Mycobacterium tuberculosis.
Mfano wa Mapafu yalioathrika kutokana na ugonjwa wa Kifua Kikuu. Picha hii ni Kwa Hisani ya mitndao ya kijamii.
Uambukizwaji wa ugonjwa huu huambukizwa kwa Njia ya hewa Ambapo magonjwa mwenye (TB) uambukiza wengine waliokiwa hawana pindi anapokohoa, anapozungumza, kucheka au kuimba.
TB ni miongoni mwa magonjwa 10 sugu ya kuambukiza Duniani ambayo yanaongoza kupoteza maisha ya watu siku hadi siku.
Kwa mujibu wa shirika la Afya Duniani Tanzania Takwimu zilionesha kuwa Takriban watu 133000 wanaishi na ugonjwa wa kifua kikuu.
Makala hii inajikita zaidi kungalia ugonjwa wa Kifua Kikuu TB unavyoongezeka siku hadi siku Visiwani Zanzibar Licha ya tahadhari kuchukuliwa na Wizara husika jambo ambalo linahitaji nguvu ya ziada katika kuendelea mapambno ili kuepusha vifo vitokanavyo na ugonjwa huu.
TAKWIMU KWA KIPINDI CHA MIAKA MITANO ZANZIBAR
Katika Kipindi Cha Miaka Mitano idadi yawagonjwa wa Kifua Kifuu (TB) ilikuwa ni yakupanda na kushuka Ambapo Mwaka 2017 ilikuwa na wagonjwa 948.
Mwaka 2018 Wagonjwa 944
2019 wagonjwa Wa kifua kikuu kufikia idadi ya 967
Wagonjwa katika mwaka 2020 ilikuwa na wagonjwa 1074
Mwaka 2021 ikawa na jumla ya wagonjwa 1090.
na hii ni kwa mujibu wa Wizara ya Afya Zanzibar.
Kwa hapa Visiwani Zanzibar Licha ya Juhudi mbali mbali zinazoendelea kuchukuliwa na Wizara ya Afya kupitia kitengo shirikishi cha maradhi ya kuambukiza Homa ya ini Kifua Kikuu na ukimwi lakini bado idadi ya wagonjwa wa Kifua Kikuu inaendelea kuongezeka siku hadi siku Visiwani Zanzibar.
Ambapo kwa mujibu wa ugunduzi Wa Kubaini Idadi ya wagonjwa wa kifua kikuu Zanzibar uliofnywa na kitengo hicho Kwa kushirikina na vituo mbali mbali vya Afya unguja na Pemba vimebainisha kuongezeka kwa idadi ya wagonjwa wa Kifua Kikuu ukilinganisha na miaka iliyopita huku baadhi ya wilaya zikiongoza kuwa na idadi kubwa ya wagonjwa wa Kifua kikuu.
Utafiti huo umebaini na kukisia kuwa Zanzibar Kuna wagonjwa 124 Kati ya kila laki moja 100000 ambapo ni Sawa na wagonjwa 1, 612 kwa mwaka.
Huku wagonjwa 1, 090 wakigunduliwa katika mwaka 2021 Sawa na asilimia 68.
MIKOA INAYOONGOZA KWA IDADI YAWAGONJWA WA KIFUA KIKUU
KISWANI UNGUJA
Ipo mikoa ambayo inaongoza kwa idadi kubwa ya wagonjwa wa maradhi ya Kifua Kikuu hapa Visiwani Zanzibar ambapo kwa upande wa kisiwa cha Unguja wilaya ya Mjini ilikuwa na idadi kubwa ya wagonjwa 281 kwa mwaka 2020 huku Mwaka 2021 ikiwa na idadi ya wagonjwa 186 wa Kifua Kikuu Ambapo Utafiti huo unaonesha kuwa mwaka 2020 idadi ya wagonjwa kwa upande wa wilaya ya maghrib A ilikuwa wagonjwa 76 Na 2021 idadi ya wagonjwa iliongezeka na kufikia 122.
Kwa upande wa wilaya ya maghrib b mwaka 2020 idadi ya wagonjwa ilikuwa ni 124 huku takwimu hizo zikionesha kuwa mwaka 2021 zimeongezeka kwa kuwa na idadi ya wagonjwa 164.
Hiyo ni kwa upande wa mkoa wa mjini maghrib ambapo Mka wa kaskazini wilaya ya kaskazini A mwaka 2020 ilikuwa na jumla ya wagonjwa 96 huku mwaka 2021 ikabainika kuwa na wagonjwa 79 Ambapo wilaya ya kaskazini b ugunduzi huo ulibainisha kuwa mwaka 2020 ulikuwa na idadi ya ya wagonjwa wa Kifua Kikuu 57 huku idadi ya wagonjwa ikiongezeka na kuwa na wagonjwa 73 kwa mwaka 2021.
Jee upande wa mkoa wa kusini unguja hali ya ugonjwa wa Kifua Kikuu ikoje ! Ugunduzi ulionesha kuwa katika kipindicha mwaka 2020 wagonjwa 86 walibainika katika hospitali na vituo vya Afya mbali mbali vya wilaya ya Kati ambapo mwaka 2021 idadi ya wagonjwa Hao ikipungua na kufikia 62 huku wilaya ya kusini ikibainika kuwa na wagonjwa 15 katika kipindi cha mwaka na 2020 kuwa na wagonjwa 22 mwaka 2021.
Upande wa kisiwani cha unguja ugonjwa huu umeonekana kwa kiasi kikubwa katika wilaya ya mjini .
HALI IPOJE KISIWA CHA PEMBA
Tuangalie Hali ya ugonjwa huu kwa upande wa ksiwa cha Pemba ambacho kina jumla ya wilaya nne katika mikoa miwili ambapo wilaya ya wete ikiongoza kwa idadi kubwa ya wagonjwa wa Kifua Kikuu ambapo ugunduzi ulibaibisha kuwa wagonjwa 105 kwa mwaka waliofanyiwa uchunguzi mwaka 2020 huku idadi ikiongezeka na kufikia 140 mwaka 2021.
Kwa upande wa wilaya ya Micheweni ambayo Ilikiwa na wagonjwa 54 na 7 mwaka 2020.
Tuiangalie wilaya ya Chake Chake na mwenendo wa ugonjwa Huu wa Kifua Kikuu (TB) ili Anika na kugunduliwa jumla ya wagonjwa 120 kwa mwaka 2020 huku mwaka uliofuata ikawa na idadi ya wagonjwa 111.
Wilaya ya Mkoani nako Hali ikoje 2020 ilikuwa na wagonjwa 60 na mwaka 2021 ikagundulika kuwa na wagonjwa 54.
WAHUSIKA WANASEMAJE KATIKA KUDHIBITI UGONJWA HUU
Mratibu kitengo shirikishi ukimwi, Homa ya ini Kifua Kikuu na Ukoma Pemba Dk Khamis Hamad Ali Alisema kuwa idadi ya wagonjwa Hao inaongezeka kila mwaka kutokana na wananchi kuhamasika kupima Afya zao ."Ni kweli Baadhi ya wilaya Zina idadi kubwa ya wagonjwa lakini hii ni kutokana na wananchi kupima Afya zao, na huo ni mkakati wa makusudi uliowekwa na Wizara ya Afya kupitia kitengo hicho ili kuweza kuwabaini wagonjwa wa TB.
Alieleza kuwa "tunaendelea kuchukua hatua za kuwapatia matibabu wagonjwa wa Kifua kikuu ambao wanabainika na dalili za awali lakini pia wale Ambao ni wagonjwa wenye Kifua Kikuu sugu tunaendelea pia kuwafuatilia majumban kuwapatia matibabu lakini elimu ya kujikinga ili wasiambukize ugonjwa kwa wengine lengo ni kuona tunadhibiti vifo vitonavyo na ugonjwa huu alisema.
Jee kwanini idadi inaongezeka na kupungua mkakati wa Wizara ni upi! Juu ya kudhibiti ugonjwa huo usiendelee.
"Mikakati mikubwa moja Wizara inaendelea kutoa huduma za upimaji wa Kifua kikuu Bure ambapo gharama za uchunguzi zote hulipwa na serikali wananchi niwaase kupima makohozi kugundua Hali za Afya zao Mara waonapo dalili za ugonjwa huu Hakuna gharama yeyote ni Bure kabisa alisema.
Jengine ni kufuatilia wagonjwa lakini pia kuwaanzishia matibabu pindi wanapobainika kuambukiza ugonjwa, Jengine tunaendelea kutoa elimu kuhusu ugonjwa huu kupitia vyombo vya Habari mbali mbali.
alisema.
NAO WANANCHI WANAMAONI GANI
Wakitoa Maoni Yao baadhi ya wananchi akiwemo mchanga Haroub shehe wameiomba serikali kupitia Wizara ya Afya kuweka ulazima wa kupima Afya zao na watakapougundilikana kwa haraka waanzishiwe matibabu.
"Rai yangu Mimi isewekwe ni hiari ya mtu kipima ugonjwa wa Kifua Kikuu ni Heri iwekwe ni lazima mtu yeyote anapokwenda hospital apimwe huu ugonjwa itasaidia kwanza wagonjwa kujulikana. Lakini pia kuanzishwa matibabu alisema".
Kwa upande wake Time Khamis Mwinyi ambae ni Mkaazi wa micheweni amelalamikia kucheleweshwa kwa majibu endapo mtu atafanya vipimo vya ugonjwa huo ambapo ameiomba Wizara ya Afya kuliangalia vyema suala hili katika kuona kasi ya kudhibiti kuenea kwa ugonjwa inafikiwa katika wilaya hiyo.
Picha Kwa Hisani ya Mitandao ya kijamii.
Kifua Kikuu sio Jina la ugonjwa Mgeni ndani ya masikio ya waliowengi ambapo wapo wanaochukulia kuwa ni ugonjwa wa kawaida lakini pia wapo wasiojua kabisa ni ugonjwa gani, unasababishwa na nini lakini pia tiba yake pamoja na athari zake ni zipi.
Kwa faida ya wasomaji wa gazeti hili Kifua Kikuu ni Aina ya ugonjwa wa kuambukiza unasababishwa na bacteria Aina ya turbeclosis kwa kifupi (TB) ulio ambapo Ugonjwa huu husababishwa na aina mbalimbali za bakteria ambazo hujulikana kama Mycobacterium tuberculosis.
Uambukizwaji wa ugonjwa huu huambukizwa kwa Njia ya hewa Ambapo magonjwa mwenye (TB) uambukiza wengine waliokiwa hawana pindi anapokohoa, anapozungumza, kucheka au kuimba.
TB ni miongoni mwa magonjwa 10 sugu ya kuambukiza Duniani ambayo yanaongoza kupoteza maisha ya watu siku hadi siku.
Kwa mujibu wa shirika la Afya Duniani Tanzania Takwimu zilionesha kuwa Takriban watu 133000 wanaishi na ugonjwa wa kifua kikuu.
Makala hii inajikita zaidi kungalia ugonjwa wa Kifua Kikuu TB unavyoongezeka siku hadi siku Visiwani Zanzibar Licha ya tahadhari kuchukuliwa na Wizara husika jambo ambalo linahitaji nguvu ya ziada katika kuendelea mapambno ili kuepusha vifo vitokanavyo na ugonjwa huu.
TAKWIMU KWA KIPINDI CHA MIAKA MITANO ZANZIBAR
Katika Kipindi Cha Miaka Mitano idadi yawagonjwa wa Kifua Kifuu (TB) ilikuwa ni yakupanda na kushuka Ambapo Mwaka 2017 ilikuwa na wagonjwa 948.
Mwaka 2018 Wagonjwa 944
2019 wagonjwa Wa kifua kikuu kufikia idadi ya 967
Wagonjwa katika mwaka 2020 ilikuwa na wagonjwa 1074
Mwaka 2021 ikawa na jumla ya wagonjwa 1090.
na hii ni kwa mujibu wa Wizara ya Afya Zanzibar.
Kwa hapa Visiwani Zanzibar Licha ya Juhudi mbali mbali zinazoendelea kuchukuliwa na Wizara ya Afya kupitia kitengo shirikishi cha maradhi ya kuambukiza Homa ya ini Kifua Kikuu na ukimwi lakini bado idadi ya wagonjwa wa Kifua Kikuu inaendelea kuongezeka siku hadi siku Visiwani Zanzibar.
Ambapo kwa mujibu wa ugunduzi Wa Kubaini Idadi ya wagonjwa wa kifua kikuu Zanzibar uliofnywa na kitengo hicho Kwa kushirikina na vituo mbali mbali vya Afya unguja na Pemba vimebainisha kuongezeka kwa idadi ya wagonjwa wa Kifua Kikuu ukilinganisha na miaka iliyopita huku baadhi ya wilaya zikiongoza kuwa na idadi kubwa ya wagonjwa wa Kifua kikuu.
Utafiti huo umebaini na kukisia kuwa Zanzibar Kuna wagonjwa 124 Kati ya kila laki moja 100000 ambapo ni Sawa na wagonjwa 1, 612 kwa mwaka.
Huku wagonjwa 1, 090 wakigunduliwa katika mwaka 2021 Sawa na asilimia 68.
MIKOA INAYOONGOZA KWA IDADI YAWAGONJWA WA KIFUA KIKUU
KISWANI UNGUJA
Ipo mikoa ambayo inaongoza kwa idadi kubwa ya wagonjwa wa maradhi ya Kifua Kikuu hapa Visiwani Zanzibar ambapo kwa upande wa kisiwa cha Unguja wilaya ya Mjini ilikuwa na idadi kubwa ya wagonjwa 281 kwa mwaka 2020 huku Mwaka 2021 ikiwa na idadi ya wagonjwa 186 wa Kifua Kikuu Ambapo Utafiti huo unaonesha kuwa mwaka 2020 idadi ya wagonjwa kwa upande wa wilaya ya maghrib A ilikuwa wagonjwa 76 Na 2021 idadi ya wagonjwa iliongezeka na kufikia 122.
Kwa upande wa wilaya ya maghrib b mwaka 2020 idadi ya wagonjwa ilikuwa ni 124 huku takwimu hizo zikionesha kuwa mwaka 2021 zimeongezeka kwa kuwa na idadi ya wagonjwa 164.
Hiyo ni kwa upande wa mkoa wa mjini maghrib ambapo Mka wa kaskazini wilaya ya kaskazini A mwaka 2020 ilikuwa na jumla ya wagonjwa 96 huku mwaka 2021 ikabainika kuwa na wagonjwa 79 Ambapo wilaya ya kaskazini b ugunduzi huo ulibainisha kuwa mwaka 2020 ulikuwa na idadi ya ya wagonjwa wa Kifua Kikuu 57 huku idadi ya wagonjwa ikiongezeka na kuwa na wagonjwa 73 kwa mwaka 2021.
Jee upande wa mkoa wa kusini unguja hali ya ugonjwa wa Kifua Kikuu ikoje ! Ugunduzi ulionesha kuwa katika kipindicha mwaka 2020 wagonjwa 86 walibainika katika hospitali na vituo vya Afya mbali mbali vya wilaya ya Kati ambapo mwaka 2021 idadi ya wagonjwa Hao ikipungua na kufikia 62 huku wilaya ya kusini ikibainika kuwa na wagonjwa 15 katika kipindi cha mwaka na 2020 kuwa na wagonjwa 22 mwaka 2021.
Upande wa kisiwani cha unguja ugonjwa huu umeonekana kwa kiasi kikubwa katika wilaya ya mjini .
HALI IPOJE KISIWA CHA PEMBA
Tuangalie Hali ya ugonjwa huu kwa upande wa ksiwa cha Pemba ambacho kina jumla ya wilaya nne katika mikoa miwili ambapo wilaya ya wete ikiongoza kwa idadi kubwa ya wagonjwa wa Kifua Kikuu ambapo ugunduzi ulibaibisha kuwa wagonjwa 105 kwa mwaka waliofanyiwa uchunguzi mwaka 2020 huku idadi ikiongezeka na kufikia 140 mwaka 2021.
Kwa upande wa wilaya ya Micheweni ambayo Ilikiwa na wagonjwa 54 na 7 mwaka 2020.
Tuiangalie wilaya ya Chake Chake na mwenendo wa ugonjwa Huu wa Kifua Kikuu (TB) ili Anika na kugunduliwa jumla ya wagonjwa 120 kwa mwaka 2020 huku mwaka uliofuata ikawa na idadi ya wagonjwa 111.
Wilaya ya Mkoani nako Hali ikoje 2020 ilikuwa na wagonjwa 60 na mwaka 2021 ikagundulika kuwa na wagonjwa 54.
WAHUSIKA WANASEMAJE KATIKA KUDHIBITI UGONJWA HUU
Mratibu kitengo shirikishi ukimwi, Homa ya ini Kifua Kikuu na Ukoma Pemba Dk Khamis Hamad Ali Alisema kuwa idadi ya wagonjwa Hao inaongezeka kila mwaka kutokana na wananchi kuhamasika kupima Afya zao ."Ni kweli Baadhi ya wilaya Zina idadi kubwa ya wagonjwa lakini hii ni kutokana na wananchi kupima Afya zao, na huo ni mkakati wa makusudi uliowekwa na Wizara ya Afya kupitia kitengo hicho ili kuweza kuwabaini wagonjwa wa TB.
Alieleza kuwa "tunaendelea kuchukua hatua za kuwapatia matibabu wagonjwa wa Kifua kikuu ambao wanabainika na dalili za awali lakini pia wale Ambao ni wagonjwa wenye Kifua Kikuu sugu tunaendelea pia kuwafuatilia majumban kuwapatia matibabu lakini elimu ya kujikinga ili wasiambukize ugonjwa kwa wengine lengo ni kuona tunadhibiti vifo vitonavyo na ugonjwa huu alisema.
Jee kwanini idadi inaongezeka na kupungua mkakati wa Wizara ni upi! Juu ya kudhibiti ugonjwa huo usiendelee.
"Mikakati mikubwa moja Wizara inaendelea kutoa huduma za upimaji wa Kifua kikuu Bure ambapo gharama za uchunguzi zote hulipwa na serikali wananchi niwaase kupima makohozi kugundua Hali za Afya zao Mara waonapo dalili za ugonjwa huu Hakuna gharama yeyote ni Bure kabisa alisema.
Jengine ni kufuatilia wagonjwa lakini pia kuwaanzishia matibabu pindi wanapobainika kuambukiza ugonjwa, Jengine tunaendelea kutoa elimu kuhusu ugonjwa huu kupitia vyombo vya Habari mbali mbali.
alisema.
MAONI YA WANANCHI
Wakitoa Maoni Yao baadhi ya wananchi akiwemo mchanga Haroub shehe wameiomba serikali kupitia Wizara ya Afya kuweka ulazima wa kupima Afya zao na watakapougundilikana kwa haraka waanzishiwe matibabu.
"Rai yangu Mimi isewekwe ni hiari ya mtu kipima ugonjwa wa Kifua Kikuu ni Heri iwekwe ni lazima mtu yeyote anapokwenda hospital apimwe huu ugonjwa itasaidia kwanza wagonjwa kujulikana. Lakini pia kuanzishwa matibabu alisema".
Kwa upande wake Time Khamis Mwinyi ambae ni Mkaazi wa micheweni amelalamikia kucheleweshwa kwa majibu endapo mtu atafanya vipimo vya ugonjwa huo ambapo ameiomba Wizara ya Afya kuliangalia vyema suala hili katika kuona kasi ya kudhibiti kuenea kwa ugonjwa inafikiwa katika wilaya hiyo.
WAHUSIKA WANASEMAJE BAADA YA MAONI HAYO YA WANANCHI.
Akizungumza suala la ucheleweshwaji wa majibu kwa wagonjwa hao Mratibu wa Kifua Kikuu Pemba Ali Amrani Amesema Ucheleweshwaji huo ni kutoka a na sababu mbali mbali ikiwa ni pamoja na kukosekana kwa vifaa vya kuchunguzia ugonjwa huo katika baadhi ya hospital ambapo kwa Sasa suala hilo limeshafanyiwa maboresho.
"Nikiri Zamani kulikuwa na hilo tatizo lakini Sasa labda walalamikaji hao walikwenda Zamani katika hiyo hospital lakini tayari limeshachukuliwa hatua baada ya kuonekana ni usumbufu kwa hiyo mgonjwa yeyote atakaefanya vipimo vya Kifua Kikuu Ataweza kupatiwa majibu yake kwa muda mfupi hosptali yeyote, wito wangu wajitokeze kupima tu usumbufu huo umeshatatuliwa".
MADAKTARI WANAELEZA KIUNDANI UGONJWA WA KIFUA KIKUU
Akizungumzia ugonjwa huu moja Kati ya Daktari wa Kifua Kikuu kisiwani Pemba Hamad Omar Hamad Alieleza kuwa dalili za ugonjwa wa Kifua Kikuu ambapo aliwataka wananchi ku chukua hatua za kufika hospitali kufanya uchunguzi endapo watakuwa na dalili kama hizi.
,"Dalili ni nyingi lakini moja ni mtu kuwa na kikohozi kwa muda mrefu ambapo atakohoa kwa zaidi ya wiki mbili, na makohozi hayo wakati mwengine huchanganyika na damu.
Alindelea kuwa kutoka na jasho jingi wakati wa usiku hata kama ni kipindi cha baridi, kukonda na kupungua uzito bila ya sababu maalum, pamoja na Homa za mfululizo kwa wiki mbili au Zaid hasa wakati wa jioni.
Katika hatua nyengine daktari huyo Alieleza Aina za Kifua Kikuu zilizopo ambapo alisema kuwa Kifua Kikuu cha ndani ya mapafu ambapo Alieleza kuwa Kifua hicho huambukiza kwa kasi zaidi.
"Aina nyengine ya Kifua Kikuu ni Kifua Kikuu cha nje ya mapafu ambacho huathiri sehemu yeyote Ile ya nje katika miwili kama vile viungo, ngozi, mifupa, kibofu cha mkojo, tezi, ngozi inayozunguka Moyo na mapafu, Uti wa mgongo na ubongo ambapo Aina hii ya Kifua Kikuu haiambukizi".
Hata hivyo daktari huyo alitowa Rai za kuweza kumaliza maradhi ya Kifua Kikuu Ambapo amewataka wagonjwa wa Kifua Kikuu kuacha usugu wa ku tumia xawa zakifua kikuu (TB) lakini pia kuepuka mikusanyiko isiyoyalazima katika makundi mbali mbali ya watu ili Kusaidia kuzuia vifo vitokanavyo na ugonjwa huo.
Kifua Kikuu ni ugonjwa hatarii na sugu lakini unaweza kutibika na kuzuilika katika kuona vifo vitokanavyo na ugonjwa huo haviongezeki Zanzibar endapo wananchi watajitokeza kufanya uchunguzi wa Afya zao juu ya ugonjwa huu lakini serikali kuchukua hatua za makusudi za kuweka ulazima wa kupima ugonjwa huu ili idadi ya vifo visiongezeke.
Miongoni mwa mambo makuu yanayirudisha nyum maendeleo kwa wananchi ni maradhi nafsi hujaahofu hivyo ushirikiano kati ya serikali na mashirika mbali mbali yanayosaidia afya kwa wananchi ni vyema kuzidisha bidii juu ya kupunguza idadi ya wagonjwa pamoja na kudhibiti kuongezeka kwa kesi mpya za ugonjwa huu.
Akizungumza suala la ucheleweshwaji wa majibu kwa wagonjwa hao Mratibu wa Kifua Kikuu Pemba Ali Amrani Amesema Ucheleweshwaji huo ni kutoka a na sababu mbali mbali ikiwa ni pamoja na kukosekana kwa vifaa vya kuchunguzia ugonjwa huo katika baadhi ya hospital ambapo kwa Sasa suala hilo limeshafanyiwa maboresho.
"Nikiri Zamani kulikuwa na hilo tatizo lakini Sasa labda walalamikaji hao walikwenda Zamani katika hiyo hospital lakini tayari limeshachukuliwa hatua baada ya kuonekana ni usumbufu kwa hiyo mgonjwa yeyote atakaefanya vipimo vya Kifua Kikuu Ataweza kupatiwa majibu yake kwa muda mfupi hosptali yeyote, wito wangu wajitokeze kupima tu usumbufu huo umeshatatuliwa".
MADAKTARI WANAELEZA KIUNDANI UGONJWA WA KIFUA KIKUU
Akizungumzia ugonjwa huu moja Kati ya Daktari wa Kifua Kikuu kisiwani Pemba Hamad Omar Hamad Alieleza kuwa dalili za ugonjwa wa Kifua Kikuu ambapo aliwataka wananchi ku chukua hatua za kufika hospitali kufanya uchunguzi endapo watakuwa na dalili kama hizi.
,"Dalili ni nyingi lakini moja ni mtu kuwa na kikohozi kwa muda mrefu ambapo atakohoa kwa zaidi ya wiki mbili, na makohozi hayo wakati mwengine huchanganyika na damu.
Alindelea kuwa kutoka na jasho jingi wakati wa usiku hata kama ni kipindi cha baridi, kukonda na kupungua uzito bila ya sababu maalum, pamoja na Homa za mfululizo kwa wiki mbili au Zaid hasa wakati wa jioni.
Katika hatua nyengine daktari huyo Alieleza Aina za Kifua Kikuu zilizopo ambapo alisema kuwa Kifua Kikuu cha ndani ya mapafu ambapo Alieleza kuwa Kifua hicho huambukiza kwa kasi zaidi.
"Aina nyengine ya Kifua Kikuu ni Kifua Kikuu cha nje ya mapafu ambacho huathiri sehemu yeyote Ile ya nje katika miwili kama vile viungo, ngozi, mifupa, kibofu cha mkojo, tezi, ngozi inayozunguka Moyo na mapafu, Uti wa mgongo na ubongo ambapo Aina hii ya Kifua Kikuu haiambukizi".
Hata hivyo daktari huyo alitowa Rai za kuweza kumaliza maradhi ya Kifua Kikuu Ambapo amewataka wagonjwa wa Kifua Kikuu kuacha usugu wa ku tumia xawa zakifua kikuu (TB) lakini pia kuepuka mikusanyiko isiyoyalazima katika makundi mbali mbali ya watu ili Kusaidia kuzuia vifo vitokanavyo na ugonjwa huo. Picha kwa hisani ya mitandao ya kijamii.
Kifua Kikuu ni ugonjwa hatarii na sugu lakini unaweza kutibika na kuzuilika katika kuona vifo vitokanavyo na ugonjwa huo haviongezeki Zanzibar endapo wananchi watajitokeza kufanya uchunguzi wa Afya zao juu ya ugonjwa huu lakini serikali kuchukua hatua za makusudi za kuweka ulazima wa kupima ugonjwa huu ili idadi ya vifo visiongezeke.
Miongoni mwa mambo makuu yanayirudisha nyuma maendeleo kwa wananchi ni maradhi nafsi hujaahofu hivyo ushirikiano kati ya serikali na mashirika mbali mbali yanayosaidia afya kwa wananchi ni vyema kuzidisha bidii juu ya kupunguza idadi ya wagonjwa pamoja na kudhibiti kuongezeka kwa kesi mpya za ugonjwa huu.
Mwisho.
Comments
Post a Comment