CCM KUSINI PEMBA YATOA TANO KWA SERIKALI NA VIONGOZI WAKE YAAHIDI MAZURI HAYA 2025

Na,Amina Ahmed Moh'd  -Pemba.
KAMATI YA Halmashauri  kuu ya CCM  Mkoa wa Kusini Pemba imetoa Pongezi kwa Serikali zote Mbili  zinavyoendelea  kutekeleza kwa zaidi ya asilimia 100 ilani ya Uchaguzi ya mwaka   2020 / 2025   sambamba na  kutoa Huduma  zenye ubora kwa  jamii.


 Akitoa Pongezi hizo kwa waandishi wa  habari   Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi  CCM  Mkoa wa Kusini Pemba  Yussuf Juma Ali    Amesema utekelezaji wa ilani  ya Uchaguzi uliofanywa na Dk Samia Suluhu Hassan Pamoja na Dk Hussein Ali Mwinyi umekuwa chachu ya katika kuleta Maendeleo  ya wazi katika sekta zote  yanayowanufaisha  wananchi Unguja ,Pemba na Tanzania .

 Kamati hiyo kwa kushirikiana na wananchama wa chama cha Mapinduzi CCM imesema itaendelea kuunga mkono juhudi za viongozi hao kwa kuwalipa ushindi wa vishindo chama  na viongozi hao katika uchaguzi wa  mwaka 2025.

Kamati hiyo pia imeiomba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kusimamia suala la kupungua kwa  bei za vyakula ikiwemo Mchele    ili lengo  la  maboresho ya Bandari  ya Mkoani yaliyochukuliwa yaweze kufikiwa na kuweza kuwanufaisha wananchi  kwa vile tayari meli za makontena  zimeanza kufika  moja kwa moja kutoka Mombasa  Hadi kisiwani Humo  lakini bado hakuna utofauti katika bei za vyakula  zilizokuwepo awali na sasa  .

Mkutano huo maalum kwa waandishi wa habari  uliofanyika leo disemba 24 katika ukumbi wa Baraza la manispaa Chake chake umefuatiwa na mkutano mkuu wa kamati ya halmashauri kuu ya CCM mkoa huo .


Mwisho.

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI