ZNCC Yawafikia wafanya biashara Pemba

Jumuiya ya kitaifa ya wafanyabiashara Zanzibar ZNCC imewafikia   wafanyabiashara waliopo kisiwani Pemba na kushirikiana nao katika kuwajengea miundombinu imara Ili kufikia maendeleo endelevu.

Akiwa katika ziara ya kutembelea wafanyabiashara mbali mbali huko wilaya ya mkoani mratibu kutoka jumuiya ya wafanyabiashara ya kitaifa Zanzibar ZNCC  Khalfan Amour Muhammed  amesema wajasiriamali wengi amesema  Bado wajasiriamali hawajitangazi na  kuonesha uwezo wao wa kazi katika kufikia  viwango ubora vinavyohitajika .

Aidha amesema ZNCC imeandaa mradi ulio kwa lengo la kuwasaidia wafanyabiashara katika Kuwapatia fursa mbali mbali Ili waweze kufikia malengo yao sambamba na kuwakuza kiuchumi.

Wakitoa changmoto zao wajasiriamali hao wamesema kuwa ukosefu wa vitendea kazi umekua ukiwapelea kushindwa kufanya kazi zao Kwa ufanisi.

Aidha wamewaomba wafanyabiashara walioko kisiwani Pemba kuwasogezea karibu malighafi Ili Wendell  sambamba na wajasiriamali wengine.

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI