WADAU WAANZA KUMUITA HAMISA FURSA KATIKA MICHEZO

NA AMINA AHMED, PEMBA.
NISHAITWA  katika mafunzo ya michezo mara mbili siku na wadau tofauti wananipigia simu  nilisema nikutafute mwandishi lakini namba yako Ilinipotea na huku nina mambo mengine nikahaflika nashukuru leo tumeonana tena.
 Waalimu tunapokuwa katika mazoezi ya vitendo wananikubali sana wananiambia kweli niko fiti na ninauwezo wa michezo Alisema .
Ni maneno ya Hamisa Omar  Hamad  mwanamichezo kutoka  Club ya mazoezo ya viungo Gombani fitness kuanza kufikiwa na fursa za kushirikishwa katika michezo alipokutana na mwandishi wa habari hizi  katika uwanja wa Gombani akiwa katika harakati za kuoatiwa mafunzo ya vitendo juu ya  kutumia mbinu za michezo  kupamabana na vitendo vya udhalilishaji yalioandaliwa na  Chama cha wanasheria wanawake Zanzibar Zafela.
Hamisa ambae awali alitamani kupata fursa ya kushirikishwa katika michezo mbali mbali ambayo  anaamini kwa utayari wake na uthubutu alionao anaweza kushiriki kuicheza na kuifundisha ambapo kupitia makala iliyochapishwa  na mwandishi wa habari hizi aliomba wadau kumshirikisha kuweza kuonesha uwezo wake.

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI