ANGOZA YATOA MAFUNZO MABADILIKO TABIA YA NCHI.

NA,  ARAFA MAKAME,RAIHAT NASSOR -PEMBA.
AFISA mdhamini wizara ya nchi ofisi ya makamu wa kwanza wa rais Pemba Ahmed Abubakar Mohammed amewataka amesema  ipo haja ya kulindwa na kuendelezwa  misitu  na mapori   ili kuhakikisha Kisiwa cha Pemba kinaendelea kubaki na haiba yake ya Kijani .

Ameyasema hayo wakati akifungua mafunzo ya siku moja kwa wawakilishi  wa  asasi tofauti za kiraia,Wananchi,watoto watu wenye ulemavu,wanawake  pamoja  na  watendaji wa serikali Pemba   uliyoaandaliwa na  ANGOZA  kwa ufadhili wa mfuko wa jumuiya ya madola  COMMON WEALTH FOUNDATION  katika kuleta mabadiliko ya tabia  ya nchi  (CLIMATE JUSTICE) yaliyifanyika  huko  katkka ukumbi wa  Madungu sekondari  .

Amesema katika kutekeleza suala  hilo  jamii inalazimika  kuacha   ukataji wa miti kiholela na kutumia nishati ambayo nisalama jambo ambalo  itapelekea kuharibu mazingira na kupelekea   kuwa na vihatarishi  vitakavyoleta athari  ikiwemo  kujaa maji ,katika maeneo ya makazi ya  wananchi   sambamba na kuzidi kwa kina cha maji  ya chumvi katika bahari.



Kwa upande wake Mkurugenzi  Kutoka taasisi ya ANGOZA  Zanzibar Hassan khamis Juma amewataka wawakilishi wa jumuia na makundi hayo kuwa mstari wa mbele katika kutoa elimu kwa jamii   katika  kulinda mazingira ili kupunguza athari zinazoweza kujitokeza wakati wa mabadiliko ya  tabia ya nchi wakiwemo wakina mama, vijana na watu wanaoishi  pembezoni mwa bahari sambamba na wakulima wa mwani..


Nae kwa  Upande wake  katibu mkuu  wa  Angoza  Zanzibar  khamis Ngwali Makame amesema lengo la kuanzishwa kwa mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo watu wa makundi mbali mbali juu ya kutambua  athari za uchafuzi wa mazingira  na haki ya mabadiliko ya tabia ya ncji ambayo yamekuwa yakiwagusa watu waote.

  
Amesema Pemba ni miongoni mwa nchi ambayo imeathirika zaidi kutokana na mabadiliko ya tabia ya nchi ambapo jumla ya  maeneo 123 yameshathirika kutokana na mabadiliko hayo kutokana na athari za kimazingira.

Ameongeza kuwa mradi huo  pia umegusa  mazingira  kwa wanawake wanaojishughulisha na kilimo wakiwemo wakulima wa mwani ,ambao pia ni   waathirika wakubwa 
Katika shughuli zao ,ambapo pia hutumia   
miti  katika  maeneo mbali mbali ya bahari na kupelekea kuharibu mazingira .

Akitoa elimu juu ya athari za kimazingira  kwa washiriki hao  mkufunzi wa mafunzo hayo Afisa kutoka ofisi ya makamu wa pili wa rais Pemba Salum Hamad Bakar  amesema taaluma ya mabadiliko ya tabia ya nchi  inayoendelea  kutolewa kwa washiriki hao imelenga kuwakumbusha wajibu wao kwa jamii katika kupambana na  kuweza kutatua  changamoto za mabadiliko ya tabia ya nchi yanapoweza kutokea katika jamii .

Mafunzo hayo yalijumuisha watu mbali mbali  wakiwemo wanawake, vijana, Watoto, watu wenye mahitaji maalumu pamoja na watu wanaoishi  pembezoni mwa bahari,asasi za kiraia,pamoja na asasi za serikali.

Mwisho



Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI