MAHAFALI YA PILI WAANDISHI CHIPUKIZI (YMF) YAMEFANYIKA LEO WAASWA KUENDELEZA HAYA

AMINA AHMED MOH'D.

  SHEREHE ya mahafali  ya  pili   kwa waandishi wa habari chipukizi   Young media fellowship  (YMF) imefanyika leo katika ukumbi wa Bima Kisiwani Unguja ambapo jumla ya wahitimu 24 waliopatiwa mafunzo  kwa muda wa mwaka mmoja kupitia mradi wa  kuandika habari  zenye  kuimarisha  uongozi kwa wanawake kupitia vyombo vya habari  wamepatiwa vyeti maalum  .

Akizungumza na wahitimu hao kupitia Sherehe  hiyo   iliyoandaliwa  na  chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania  Tamwa Zanzibar kwa ufadhili wa shirika la  National endowment for democracy ( NED)   mkurugenzi wa chama hicho Dk Mzuri  Issa Ali amewataka waandishi hao  kuendelea    kushirikiana na chama hicho   katika kutetea haki za wanawake   ili kuweza kupata haki wanazostahiki ikiwemo masuala ya uongozi

Awali akizungumza  Mjumbe wa bodi kutoka Tamwa Hawra Shamte kwa niaba ya mwenyekiti wa Chama hicho  amewapongeza wahitimu hao kwa kufikia malengo  ya mradi huo ambapo amewataka wahitimu hao kuendelea kutumia vyema kalamu    zao katika kuwasaidia wanawake kuondokana na changamoto mbali na kuwaonesha wanawake kupitia vyombo mbali mbali vya habari .

Aidha amewataka wahitimu hao  kujiwekea malengo ya kuwa waandishi   wa habari  ambao watakuwa wawakilishi wa wananchi wasio na sauti katika kupata haki zao mbali mbali badala yake kuendeleza kupaza sauti  kwa uadilifu katika kutetea maslahi ya wanawake  na makundi ya pembezoni.

 Akizungumza kwa niaba ya wakufunzi wa  wahitimu  hao Shifaa Said  amewataka wahitimu hao kuendeleza uandishi wa habari wenye maslahi ya jamii na kuondokana na uandishi wa habari  wa  matukio ambao hauleti tija kwa jamii.

Aidha amewataka wahitimu hao kudhibiti kufanya uandishi wa habari kwa kufanya mahojiano marefu  kutoka kwa vyanzo vya habari ili kupatikana habari zenye kueleweka kwa uharaka zaidi.

Akisoma taarifa  ya  mradi huo wa kuimarisha  uongozi kwa wanawake kupitia vyombo vya habari kaimu Afisa mradi huo Hairat Haji amesema  kuwa  wahitimu hao wamefikia kwa asilimia 99.9  malengo ya mradi huo ambapo jumla ya habari  347 kati ya 348 zilizohitajika   zimeandikwa na  kutumwa katika vyombo mbali mbali  vya habari  tofauti ikiwemo mitandao ya kijamii radio na magazeti habari ambazo zimefanyiwa utafiti.

Akitoa neno la  shukurani  kwa niaba  wahitimu hao  24 ambao ni waandishi wa habari vijana  Khadija Rashid Nassor amesema kuwa mafunzo hayo ya mwaka mmoja  kupitia mradi huo yamekuwa chachu  ya mabadiliko katika kuandika habari za maendeleo   ambapo ameutaka uongozi wa tamwa kuendelea kuwatumia  wahitimu hao katika kazi zao mbali mbali za habari katika kuibua  na kuandika habari mbali mbali   kwa lengo la kuleta maendeleo kwa taifa.

 Nao baadhi ya  wahariri ambao ni wadau wa  habari   za maendeleo kwa wanawake akiwemo Said Omar Said  kutoka radio jamii mkoani ameushukuru uongozi wa Tamwa zanzibar katika kuwafundisha vyema waandishi wa habari vijana kuandika habari zenye tija  na mabadiliko katika jamii

Katika Sherehe hiyo Wahitimu watatu kati ya 24  waliofanya  vizuri katika kazi za habari hizo  wametunukiwa  zawadi maalum  ambazo ni  Laptop pamoja na vyeti maalum.

Mwisho.

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI