MATTAR ATOA NENO KWA WAJASIRIAMALI NA WAFANYA BIASHARA PEMBA AWATAKA PIA KUAGIZA BIDHAA KUTOKA NJE YA NCHI KUPITIA KAMPUNI YA MUNIMS CARGO KWA UHAKIKA ZAIDI KUEPUSHA USUMBUFU.

NA AMINA AHMED MOH’D, PEMBA. 
           

WAJASIRIMALI na wafanya biashara  kisiwani Pemba wametakiwa  kuitumia fursa ya kuanzisha  huduma  muhimu zinazohitajika katika jamii kwa  kushirikiana na kampuni zinazoaminika na serikali  katika kuagiza bidhaa mbali mbali nje ya nchi ili kujikomboa kiuchumi na kupata maendeleo waliokusudia .

 Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa mkoa wa Kusini Pemba Mattar Zahor Massoud alipokuwa akizungumza na wafanya biashara  na wajasiriamali  kutoka maeneo mbali mbali kisiwani Pemba  katika mkutano maalum  ulionadaliwa na kampuni ya kuagiza na kusafirisha bidhaa mbali mbali kutoka nchini China kuja Tanzania MUNIMS  CARGO  International Trading Company Limited   uliofanyika katika ukumbi wa Tibirinzi Chake Chake. 

Amesema  wafanya biashara na wajasiriamali wadogo wanazo fursa katika kukuza uchumi wao na taifa kwa kuanzisha biashara muhimu ambazo zinahitajika na jamii  ya kisiwa cha Pemba lakini bado hazijaanzishwa kutokana na sababu mbali mbali ikiwemo  upatikanaji wa uhakika wa vifaa   kutoka nje ya nchi. 

"Ni vyema kuzichangamkia Fursa za kuanzisha biashara zenye tija ambazo zinaumuhimu na zinahitajika  na jamii kabla ya fursa hizo kuja kuchukuliwa na wageni, mfano kuanzisha  vituo vya  GYM maenwo mbali mbali ". 
  MATTAR  ZAHOR MASSOUD, RC - KUSINI PEMBA. 

Kuagiza vifaa kutoka nje   ya nchi kwa kampuni hii yenye vijana wazawa na wazalendo wanapenda maendeleo   ya wajasiriamali na wafanya biashara wadogo ambao kutokana na  mitaji yao bado uwezo wa kuagiza moja kwa moja kutoka viwandani ni mdogo niwaase muitumie hii fursa adhimu kwenu  ya MUNIMS CARGO ".

 Tayari vijana wanauzoefu wa muda mrefu kuagiza kusafirisha na kufuatilia bidhaa mbali mbali kutoka viwanda vya china kuja Tanzania" Alisema Mattar.

 Aidha mkuu huyo ameipongeza kampuni hiyo  ya MUNIMS CARGO kwa kuonesha uzalendo wa kuisadia serikali katika kurahisisha lengo la  kuwainua wafanya biashara na wajasiriamali wadogo kiuchumi  kwa kushirikiana nao katika kuagiza bidhaa mbali mbali  kwa usalama .

 Hata hivyo amewataka vijana  kujenga imani kampuni mbali mbali za kizalendo  ambazo zinalengo la kusaidia serikali  na taifa   katika kutimiza malengo yaliowekwa na Serikali.

 Afya, Viwanda, Uwekezaji, Uchumi wa buluu, Kilimo, Michezo, Ufugaji, na mengi mengineyo ni miongoni mwa  vipaumbele  vya Dk Hussein Ali Mwinyi Rais wa Zanzibar  wa awamu hii ya 8  kwa wananchi wake, tunapowaona vijana wazawa wanakuwa bega kwa bega  na serikali yao kwa kuunga mkono  na kuonesha njia kwa wengine kufanikisha malengo hayo ni jambo la  faraja kwetu, niwatake ndugu wajasiriamali na wafanya biashara kutoiwacha fursa hii badala yake  muitumie ipasavyo kuagiza bidhaa  mbali mbali .
   MUNIR SAID  SLEIMAN-MKURUGENZI MUNIMS CARGO. 

Nae Mkurugenzi wa kampuni hiyo  Munir Said Sleiman   amesema lengo la kuwafikia  wajasiriamali kuwapa elimu juu ya namna bora ya kuagiza bidhaa zenyw tija na fursa kupitia kampuni hiyo ni  kusaidia kupunguza changamoto zinazowakabali wafanya biashara hao ikiwemo kutapeliwa  na kukosa uhakika wa kufika salama  biashara zao  wanapoagiza kutoka nchini china sambamba na kuunga mkono juhudi za serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuwainua wajasiriamali na wafanya biashara wadogo kwa ushirika na mmoja mmoja .

Aidha  mkurugenzi huyo amefafanua fursa hizo  za kuagiza bidhaa kwa wajasiriamali wadogo wadogo  ni pamoja na vifaa vya kisasa vya  ujenzi, vifaa, vya majumbani, vifaa vya michezo, biashara, vifaa vya matibabu, ufugaji, Pembejeo za kilimo, pamoja na uvuvi ambapo amesema kuwa uhakika kuagiza vifaa hivyo kutoka China kuja Tanzania   ni wenye kuaminika na kutambuliwa kisheria.

 Nao Baadhi ya wajasirimali waliofika katika mkutano huo akiwemo Asha Omar, Pamoja na Omar Hamad Kombo wameishukuru Kampuni hiyo kwa kuwapa  uwelewa juu ya kuagiza na kununua bidhaa kutoka china kuja Tanzania ambapo wamesema uwepo wa kampuni hiyo kutasaidia  kupunguza changamoto sambamba na kurahisisha uagizaji wa  bidhaa  mbali mbali na kupatikana kwa urahisi. 

 Aidha wameiomba Serikali kupunguza baadhi ya gharama wanapiagiza bidhaa kutoka nje ya nchi ili kuzidisha ufanisi katika  biashara zao.

 MUNIMS CARGO INTERNATIONAL TRADING COMPANY LIMITED ni Kampuni ya kusafirisha na kuagiza bidhaa kutoka nchini china kuja Tanzania  yenye uzoefu  na  watendaji wazawa wa Zanzibar ambapo miongoni mwa Bidhaa zinazoagizwa kupitia kampuni hiyo ni pamoja na  vifaa vya hospitali, vifaa vya kilimo, Uvuvi, vifaa vya majumbani, maofisini, biashara  na nyenginezo.


Mwisho

 "

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI