ZRA KUDHAMINI MGENI NDONDO CUP MSIMU UJAO WAASWA KUHAMISHA ULIPAJI KODI NA MATUMIZI YA RISITI ZA KIELECTRONIKI.

NA, AMINA AHMED MOHD, PEMBA. 
KATIKA kuhamasisha ulipaji wa kodi, kudai risiti za kielectroniki  wakati wa kununua bidhaa  katika maduka mbali mbali Kamishna wa mamlaka ya mapato Zanzibar ZRA  Yussuf Juma Mwenda  akiambatana na wasaidizi wa mamlaka hiyo wamefika katika uwanja wa shaame mata  Wilaya ya Micheweni  kuzungumza na wadau wa mpira wa miguu kutoa elimu juu ya suala hilo. 

Kamishna mwenda amewataka  wanamichezo kuendelea kuisaidia serikali suala la risiti za kielectroniki pamoja na ulipaji kodi ili kuendeleza shughuli mbali mbali za maendeleo ikiwemo  uimarishaji wa viwanja vya michezo.

 Sisi Peke yetu bila mashirikiano hatutweza kuishinda hii vita  kila mmoja wetu kwa nafasi yake akumbuke kuwa wajibu wake ni kusaodia serikali juu ya suala zima la kodi.

 Aidha kamishna ameahidi udhamini  wa mashindano ya kombe la Mgeni ndondo cup linalowakutanisha vijana wa michezo katika wilaya ya micheweni pamoja na wilaya jirani katika msimu ujao wa mashindano hayo ikiwa ni sehemu ya kuongeza nguvu katika kuuinua michezo wilayani humo kupitia kodi zinazokusanywa na mamlaka hiyo.

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI