WATU WENYE ULEMAVU WALIA NA SERIKALI NA WADAU KUTOKUWASHIRIKISHA KATIKA MASUALA YA KUTOA MAAMUZI.

NA AMINA AHMED MOH’D, PEMBA. 

WATU wenye ulemavu wa akili kisiwani Pemba wameiomba Serikali pamoja na wadau kuwaunga mkono katika shughuli zao  wanazozifanya ili waweze kujipatia kipato na kujikomboa na umaskini.

 Wakizungumza kwa  nyakati tofauti baadhi ya watu hao wamesema licha ya kujishughulisha na shughuli mbali mbali lakini bado serikali na wadau wamekuwa wakilisahau kundi hilo  katika kuwaendeleza  kiuchumi kama yalivyo makundi mengine ya watu wenye ulemavu.
 
"Najishughulisha na kilimo cha miche ya mivinje, miti ya kudumu na mboga mboga , Nishaepeleka barua wizara yakilimo juu ya kuja kunitembelea walau kuniongezea maarifa katika kilimo changu hicho lakini hakuna hata mmoja aiwahi kuja huku watu wakiiba miche na wengine wakitia ngo'mbe katika mashamba yangu ". 

Fursa za mikopo hazitufikii kama walemavu wengine tumekuwa tukiachwa nyuma  na jamii lakini na hata serikali  katika mambo mengi, inatuona kama sisi  hatustahiki kuthaminiwa, hatushirikishwi kutoa maoni, hatushirikishwi  tunaoneka hatuna  uwezo wa kufikiria tunazidi kurudi nyuma". Omar Said Ali mweneye ulemavu wa akili  Vikunguni Chake Chake. 

Aidha Omar ameiomba jamii  kuepuka kuwaita majina yasiostahiki yenye kuleta mawazo  pamoja na kuwabambikizia makosa  ambayo hayawahusu, kwa malengo ya kuwasababishia matatizo zaidi. 

"Mtu anakuita zezeta, mara anakuita kiguu chechegu, mara kikono upande, mara faza  inafika hadi unasingiziwa makosa makubwa ya ubakaji sababu tu unaonekana utakosa mtetezi wa kukutetea  tunaumia na  tunachukizwa sana serikali itusaidie kupiga marufuku.".

Nae kwa upande wake  Salma  Ali Haji  Kutoka Msuka wilaya ya Micheweni   pamoja ma  Saumi Khamis Hamad kutoka Konde wamewaomba wadau pamoja na serikali  kuwasaidia watu wenye ulemavu wa akili kuepukana na udhalilishaji wanaoendelea kufanyiwa katika jamii ikiwa ni pamoja na kushambuliwa na kupuuzwa wanapofanya shughuli zao  . 

 " Bado jamii haituoni kama ni watu wenye ulemavu wanatulinganisha na watu wenye akili pindi tunapokosea, tukiwa katika harakati zetu za kufanya biashara  tunaonekana kama  vichekesho ukiwa katika harakati   njiani mara tunalengwa mawe bila sababu " Alisema Saum. 

"  Niliacha skuli baada ya kuona napumbwaza mara hujaolewa , watu wanatuona kama sisi wanawake wenye ulemavu wa akili ni watu wakuolewa, wapo wanatukopa biashara zetu hawatulipi pia serikali itusaide kutuwekea  usawa ili na sisi tuepukane na madhila hayo". 

Aidha  Rashid Habib Salum Kutoka Kengeja  ameiomba serikali kuweka masharti maalum kwa watu wenye ulemavu wa akili wanaposhirikishwa  kufanya kazi  za kijamii ili kuweza kupata haki zao  wanaposhiriki katika kazi hizo.

"Tunakuwa tunafanya kazi bila kuchoka wala kuhurumiwa   na malipo yetu tunayakosa binafsi nililetwa chake chake kufanya kazi ya ujenzi lakini sijalipwa hata senti wenzangu wamelipwa wanajua sina uwezo wa kusema popote nikaaminika kwa sababu ya uleavu wangu". 

 "Sisi pia tuna haki ya kuwa na familia lakini jamii hailiangalii ilo unaweza ukawa na familia lakini ukapokonywa kutokana na kukosa kuhudumia. "

 Akizungumza juu ya Changamoto hizo zinazowakumba watu hao Halfan Amour Muhammed  ambae ni Katibu Jumuia ya watu wenye  ulemavu wa akili Pemba amesema taasisi imekuwa ikizipatia ufumbuzi changamoto zinazowakabili watu wenye ulemavu  kwa kuwapa elimu ya kujitambua na kuweza  kuzisemea. 

 "Changamoto ni nyingi ambazo zinawakabili kama ambazo wamezitaja  kudhalilishwa, kuitwa majina mabaya, kukosa fursa za kushiriki na kushirikishwa katika kutoa maamuzi, kuonekana sio watu wa maana katika jamii kutengwa na mengineyo sisi kama Jumuia  jambo la kwanza tumekuwa tukiwapa elimu ya kujitambua". 

" Tunawajenga waweze kuzisemea wenyewe  na kwa sasa ndani ya jumuia   tumeanzisha  vikundi  kwa wanachama vikundi ambavyo  ni vya utetezi binafsi  hivi kazi yake kubwa ni kuwasaidia wao wenyewe wanachama wetu kuweza kuzisemea   changamoto  zao zinapowatokea". 

" Na jambo hili limefanikiwa kwa kiasi kikubwa  wapo ambao wameshapata changamoto na wakaweza kusimama wenyewe kujitetea katika vyombo vya maamuzi  mahakamani na wakafanikiwa". 

"Aidha amesema jumuia hiyo imekuwa ikifanya mikutano  na wanajamii, kutoa mafunzo namna ya kuishi na kuwashirikisha watu wenye ulemavu wa akili kufuatilia  wanapopata  changamoto ili kuizipatia ufumbuzi". 

Hata hivyo  Katibu huyo ameiomba serikali pamoja na wadau  kuwaangalia vyema watu wenye ulemavu wa akili kwa kutambua haki zao  . 

"Wadau na Serikali iwaangalie watu wenye ulemavu wa akili kwa jicho la pili, kuwapa mashirikiano, wao ni watu wenye mawazo mazuri pia wanapopewa fursa, haki ya kuwalinda na udhalilishaji kuwapa mashirikiano  kutambua haki zao kama watu wengine wenye ulemavu . 

 Mazungumzo haya maalumu  kati ya watu wenye ulemavu wa akili pamoja na mwandishi wa habari  hizi  ni katika kuelekea siku ya afya ya akili duniani ambayo  kikele  chake ni oktoba  10  ya kila mwaka lengo ni kusaidia kupaza sauti zao kuona changamoto zinazowakabili zinapatiwa ufumbuzi. 

Mwisho 




 
 

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI