WAKULIMA WA KARAFUU WAIOMBA SERIKALI YA AWAMU YA NANE KUWAANGALIA ZAIDI

NA AMINA AHMED MOH’D, PEMBA. 
WAKULIMA  wa zao la karafuu kisiwani  Pemba wameiomba Serikali  ya Mapinduzi ya Zanzibar Kuwasaidia kupata mikopo  itakayosaidia  kuAimarisha  kilimo cha zao hilo na kusimamia mashamba ya zao hilo  ha ili kuweza kupata mavuno mengi msimu unapowadia.

 Wakizungumza na  habari hizi maalum baadhi ya wakulima   hao waliofika katika banda la kuuzia karafuu Madungu Chake Chake Mkoa wa kusini Pemba   Akiwemo  Ayoub Muhamed pamoja na  Hamad Habibu Sultan Habibu   wamesema  kuwa licha ya Kujishughulisha na zao  hilo   bado manufaa kwa wakulima yamekuwa madogo kutokana na kuvuna  mazao kidogo  kutokana na ukosefu wa fedha za kusimamia  na kuendeshea shughuli za kilimo hicho.

 Walisema kuwa   Licha ya zao hilo kuwa ni miongoni mwa mazao yenye tija kwa taifa lakini bado wakulima   wamekuwa wakikosa msaada  katika kuendesha harakati hizo kwa kukosa mkopo kama ilivyokuwa awali  jambo ambalo kwa upande wao limekuwa changamoto .

 Aidha  wakulima hao wameiomba Serikali kuiangalia tena bei ya  zao hilo  na kuongeza ili kuendana  na gharama za ushughulikiaji wa  mikarafuu wanaofanya .

wamesema bei  wanayoendelea kuuza karafuu  kwa sasa haikidhi haja zao kutokana na kutumia gharama kubwa katika kulima zao hilo. 

Katika hatua nyengine wakulima  hao wameliomba shirika la biashara ZSTC kutowacheleweshea  malipo yao wanapofanya mauzo  ya karafuu sambamba na kupunguza makato ya tozo . 

 Akizungumza juu ya  maoni hayo yaliotolewa na  baadhi ya wakulima hao   Afisa dhamana wa shirika la biashara la taifa ZSTC Pemba Abdalla Ali Ussi    amesema  ugawaji wa  miche ya mikarafuu kwa wakulima wote   bado  haukidhi  haja kwa wakulima wote hivyo ni vyema wakulima kuendelea kupanda  miche  kwajili ya kukuza zao hilo.

 Aidha   kuhusu suala la  fedha kutolewa  Kwa wakulima Kwa njia ya benki  mdhamini huyo amesema  shirika linafanya hivyo kwajili  ya usalama wa fedha za wakulima  .

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI